Sunday, September 22, 2013

AL SHABAAB WATHIBITISHA KUHUSIKA KATIKA MAUAJI YA KIGAIDI NAIROBI

Baadhi ya majeruhi katika shambulio la kigaidi jijini Nairobi.
-Wadai Kenya ilipuuza onyo lao
-Wasema ni kulipiza kisasi kwa Kenya kijihusisha katika vita ya Somalia
-Watu zaidi ya 30 wadaiwa kupoteza maisha wengine wakijeruhiwa
KUNDI la Alshabaab, limethibitisha kuhusika na shambulio la kigaidi lililotokea jana kwenye jengo la ghorofa nne lenye maduka la Westgate jijini Nairobi, nchini Kenya.
Alshabaab kupitia kwa afisa wake mmoja, imethibisha hilo na kueleza kuwa shabulio lilikuwa na kulipiza kisasi baada ya Kenya kujihusisha na vita ya Somalia.
Hali ilivyokuwa ndani ya jengo lililovamiwa na magaidi.
Walioshuhudia tukio hilo wanadai watu waliovalia magwanda yalioonekana kama ya kijeshi huku wengine wakiwa wamefunika nyuso zao walivamia jengo hilo huku wakifyatua risasi.
Maduka hayo ya Westgate hutendelewa sana na matajiri pamoja na wageni kutoka nchi mbalimbali.
Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al Shabaab imesema kuwa Kenya ilijidai kutosikia onyo hizo, na kuendelea kuwaua waislamu wasio na hatia nchini Somalia, na shambulio la Westgate ni tone tu katika bahari ya mfano wa yanayowakumba wasomali nchini Somalia.
Taarifa kutoka Ikulu ya nchini Kenya, zinadai kuwa mmoja wa watuhumiwa aliyekamatwa katika tukio hilo  alifariki kutokana na majeraha yake.
Magaidi wapatao kumi walivamia jengo la kifahari la Westgate jana mchana la kuwapiga risasi kiholela Wakenya waliokuwa wanaendelea na shughuli zao za kawaida.

MASOGANGE AANIKA YA JELA

Stori: Waandishi Wetu
JUZI jijini Dar es Salaam zilisambaa taarifa kuwa Video Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ amefutiwa mashitaka yaliyokuwa yakimkabili ya kukamatwa na madawa ya kulevya aina ya crystal methamphetamine yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8, Julai 5, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg, Afrika Kusini.
Kufuatia taarifa hizo, Risasi Jumamosi lilianza kuwatafuta watu wenye uhakika wa madai hayo ili kuujua ukweli. Miongoni mwa watu waliokuwa kwenye orodha ya kutafutwa ni pamoja na Balozi wa Tanzania Afrika Kusini, Radhia Msuya, mchumba wa Masogange aliyepo Bongo, Evans Komu na Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Afande Godfrey Nzowa.
ALIVYOSEMA AFANDE NZOWA
Wa kwanza kupatikana alikuwa Kamanda Nzowa ambaye  alisema:
“Ninachojua mimi, Agnes na mwenzake (Melisa Edward) bado wanashikiliwa. Kesi yao ilikuwa Jumatano (Septemba 18, 2013), itatajwa tena Novemba mwaka huu.”
Nzowa akapiga hatua zaidi kwa kusema kwamba aliwahi kwenda Afrika Kusini kwa lengo la kuwahoji akina Masogange kabla ya kupandishwa kizimbani Jumatano iliyopita lakini hawakumpa ushirikiano.

BALOZI WA TANZANIA, AFRIKA KUSINI
Baada ya Kamanda Nzowa, Risasi Jumamosi lilimtafuta Balozi wa Tanzania Sauzi, Msuya akasema:
“Mimi sina uhakika, ilimradi umeniambia nitafanya hivyo maana nimekuwa nikifuatilia sana maisha yao wakiwa jela. Lakini pia napenda muwaambie vijana wa Tanzania, wanapokuja huku wawe kamili, waje kwa uhalali, wawe na fedha za kujikimu wakiwa huku mpaka watakaporudi.”
MCHUMBA WA MASOGANGE SASA
Baada ya kuzungumza na balozi huyo, Risasi Jumamosi lilimtafuta Evans na kumuuliza kuhusu madai hayo ambapo alikiri Masogange kuwa huru, akasema:
“Ni kweli mchumba ‘angu Agnes yuko huru. Wasiomjua ndiyo walikuwa wanasema, wameniambia mambo mengi sana kuhusu yeye lakini nilivumilia. Namshukuru Mungu Agnes amerudi tena mikononi mwangu.”
Evans alikwenda mbele zaidi kwa kumuunganisha mwandishi wetu na Agnes kule Sauzi ambapo walizungumza kwa dakika ishirini na mbili.
Risasi: Mambo Eg?
Masogange: Poa, mzima wewe?
Risasi: Mi mzima bwana, pole, nasikia uko huru?
Masogange: Ee, namshukuru sana Mungu.
Risasi: Hivi hebu niambie kwa ufupi, hali ya magereza ya huko ikoje?
Masogange:  Ni balaa, nimekuwa nikiishi maisha magumu sana. Unajua kuishi na watu ambao si taifa lako ni tatizo kubwa, hakuna amani, inachosha akili na kila kitu.
“Ilifika mahali nilitamani ningepata matatizo haya nikiwa nyumbani lakini si ugenini.”
AFUNGA NA KUOMBA
Agnes alienda mbele zaidi kwa kusema amekuwa akifunga na kuomba kila siku kwa muda wote akimlilia Mungu amsaidie kutoka kwenye janga lake.
“Nilifunga sana, pia nilikuwa naomba maombi mazito kabisa. Nimekonda kwa sababu ya kufunga huko.”
USAGAJI
Kuhusu vitendo vya usagaji, staa huyo alisema kuwa askari wa Sauzi wako makini sana na hilo na wanatoa somo kila mara linalokataza tabia ya usagaji na kwamba mtu akibainika anaweza kufunguliwa shitaka jipya.
ALIWAHI KUTILIWA SHAKA
Alisema alishawahi kuitwa na Melisa na kuulizwa kuhusu uhusiano wao, akajieleza kuwa ni mama mkubwa kwa mdogo, ikawa nafuu yao lakini walihisiwa vibaya kutokana na ukaribu wao.
ADAI ALIWAHI KUTONGOZWA NA ASKARI
Risasi: Tuliwahi kusikia kwamba kuna askari wanakutongoza kutokana na wowowo lako. Je, madai haya ni ya kweli?
Agnes: (kicheko), watu wanachonga sana. Unajua mimi nina mchumba wangu jamani.
Risasi: Lakini kuna ukweli wa madai hayo?
Agnes: (akakata simu).
Swali hapa linaweza kuwa hivi, kama hajaachiwa huru kwa nini aliongea na simu akiwa gerezani? Jibu lipo. Masogange amekuwa akipatikana hewani mara kadhaa licha ya kuwa gerezani.
WATU WAMSOMA KWENYE INSTAGRAM
Kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambao hakuwa hewani tangu Julai mwaka huu, usiku wa Septemba 17, 2013 aliandika hivi:
“Thanks God nimeamini wewe ulikuwa pamoja na mimi katika maombi yangu na thanks kwa wote mliokuwa mkiniombea, Mungu kapokea maombi yenu.”
Halafu akaendelea: All praise and glory to the Lord almighty I thank you for my freedom, amen (Sifa zote ni kwa Bwana, nakushukuru kwa uhuru wangu, amen).
LINAVYOSEMA RISASI JUMAMOSI
Risasi Jumamosi linaweka wazi kwamba, Agnes awe ameachiwa au hajaachiwa, lakini watu wote waliotafutwa ili wazungumze walipatikana na walisema kama ambavyo imeandikwa.
VIPI KUHUSU REHEMA FABIAN?
Wakati tunakwenda mitamboni kuna habari zilisambaa kwamba, Miss Kiswahili 2009, Rehema Fabian anadaiwa kukamatwa nchini China.
Madai yamesema mengi, lakini hakuna mwenye kusema wazi kisa nini ingawa wengine walidokeza habari za unga.
MASOGANGE...
Stori: Waandishi Wetu

JUZI jijini Dar es Salaam zilisambaa taarifa kuwa Video Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ amefutiwa mashitaka yaliyokuwa yakimkabili ya kukamatwa na madawa ya kulevya aina ya crystal methamphetamine yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8, Julai 5, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg, Afrika Kusini.
Kufuatia taarifa hizo, Risasi Jumamosi lilianza kuwatafuta watu wenye uhakika wa madai hayo ili kuujua ukweli. Miongoni mwa watu waliokuwa kwenye orodha ya kutafutwa ni pamoja na Balozi wa Tanzania Afrika Kusini, Radhia Msuya, mchumba wa Masogange aliyepo Bongo, Evans Komu na Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Afande Godfrey Nzowa.

ALIVYOSEMA AFANDE
NZOWA
Wa kwanza kupatikana alikuwa Kamanda Nzowa ambaye  alisema:
“Ninachojua mimi, Agnes na mwenzake (Melisa Edward) bado wanashikiliwa. Kesi yao ilikuwa Jumatano (Septemba 18, 2013), itatajwa tena Novemba mwaka huu.”
Nzowa akapiga hatua zaidi kwa kusema kwamba aliwahi kwenda Afrika Kusini kwa lengo la kuwahoji akina Masogange kabla ya kupandishwa kizimbani Jumatano iliyopita lakini hawakumpa ushirikiano.

BALOZI WA TANZANIA,
AFRIKA KUSINI
Baada ya Kamanda Nzowa, Risasi Jumamosi lilimtafuta Balozi wa Tanzania Sauzi, Msuya akasema:
“Mimi sina uhakika, ilimradi umeniambia nitafanya hivyo maana nimekuwa nikifuatilia sana maisha yao wakiwa jela. Lakini pia napenda muwaambie vijana wa Tanzania, wanapokuja huku wawe kamili, waje kwa uhalali, wawe na fedha za kujikimu wakiwa huku mpaka watakaporudi.”

MCHUMBA WA
MASOGANGE SASA
Baada ya kuzungumza na balozi huyo, Risasi Jumamosi lilimtafuta Evans na kumuuliza kuhusu madai hayo ambapo alikiri Masogange kuwa huru, akasema:
“Ni kweli mchumba ‘angu Agnes yuko huru. Wasiomjua ndiyo walikuwa wanasema, wameniambia mambo mengi sana kuhusu yeye lakini nilivumilia. Namshukuru Mungu Agnes amerudi tena mikononi mwangu.”
Evans alikwenda mbele zaidi kwa kumuunganisha mwandishi wetu na Agnes kule Sauzi ambapo walizungumza kwa dakika ishirini na mbili.
Risasi: Mambo Eg?
Masogange: Poa, mzima wewe?
Risasi: Mi mzima bwana, pole, nasikia uko huru?
Masogange: Ee, namshukuru sana Mungu.
Risasi: Hivi hebu niambie kwa ufupi, hali ya magereza ya huko ikoje?
Masogange:  Ni balaa, nimekuwa nikiishi maisha magumu sana. Unajua kuishi na watu ambao si taifa lako ni tatizo kubwa, hakuna amani, inachosha akili na kila kitu.
“Ilifika mahali nilitamani ningepata matatizo haya nikiwa nyumbani lakini si ugenini.”

AFUNGA NA KUOMBA
Agnes alienda mbele zaidi kwa kusema amekuwa akifunga na kuomba kila siku kwa muda wote akimlilia Mungu amsaidie kutoka kwenye janga lake.
“Nilifunga sana, pia nilikuwa naomba maombi mazito kabisa. Nimekonda kwa sababu ya kufunga huko.”

USAGAJI
Kuhusu vitendo vya usagaji, staa huyo alisema kuwa askari wa Sauzi wako makini sana na hilo na wanatoa somo kila mara linalokataza tabia ya usagaji na kwamba mtu akibainika anaweza kufunguliwa shitaka jipya.

ALIWAHI KUTILIWA SHAKA
Alisema alishawahi kuitwa na Melisa na kuulizwa kuhusu uhusiano wao, akajieleza kuwa ni mama mkubwa kwa mdogo, ikawa nafuu yao lakini walihisiwa vibaya kutokana na ukaribu wao.

ADAI ALIWAHI
KUTONGOZWA NA ASKARI
Risasi: Tuliwahi kusikia kwamba kuna askari wanakutongoza kutokana na wowowo lako. Je, madai haya ni ya kweli?
Agnes: (kicheko), watu wanachonga sana. Unajua mimi nina mchumba wangu jamani.
Risasi: Lakini kuna ukweli wa madai hayo?
Agnes: (akakata simu).
Swali hapa linaweza kuwa hivi, kama hajaachiwa huru kwa nini aliongea na simu akiwa gerezani? Jibu lipo. Masogange amekuwa akipatikana hewani mara kadhaa licha ya kuwa gerezani.

WATU WAMSOMA KWENYE INSTAGRAM
Kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambao hakuwa hewani tangu Julai mwaka huu, usiku wa Septemba 17, 2013 aliandika hivi:
“Thanks God nimeamini wewe ulikuwa pamoja na mimi katika maombi yangu na thanks kwa wote mliokuwa mkiniombea, Mungu kapokea maombi yenu.”
Halafu akaendelea: All praise and glory to the Lord almighty I thank you for my freedom, amen (Sifa zote ni kwa Bwana, nakushukuru kwa uhuru wangu, amen).

LINAVYOSEMA RISASI
JUMAMOSI
Risasi Jumamosi linaweka wazi kwamba, Agnes awe ameachiwa au hajaachiwa, lakini watu wote waliotafutwa ili wazungumze walipatikana na walisema kama ambavyo imeandikwa.

VIPI KUHUSU REHEMA
FABIAN?
Wakati tunakwenda mitamboni kuna habari zilisambaa kwamba, Miss Kiswahili 2009, Rehema Fabian anadaiwa kukamatwa nchini China.
Madai yamesema mengi, lakini hakuna mwenye kusema wazi kisa nini ingawa wengine walidokeza habari za unga.

KIOJA KORTINI

Stori: Richard Bukos
KIOJA cha mwaka kilitokea Jumatano wiki hii katika Mahakama ya Jiji ya Sokoine Drive jijini Dar es Salaam, baada ya mkazi mmoja wa Buguruni, Hassan Omary kujisaidia haja kubwa kizimbani wakati akisomewa shtaka lake la uzururaji.Mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo, Richard Magodi alikuwa akimsomea shtaka hilo, mbele ya Hakimu Mfawidhi, William Mutaki na alipotakiwa kukiri au kukanusha kosa lake, mtuhumiwa huyo alibaki kimya akiwa amemtumbulia macho hakimu.Katika hali isiyotarajiwa, mtuhumiwa huyo alionekana akijikamua kama anayejisaidia na ghafla, harufu kali ya kinyesi ikatanda mahakamani hapo.Hakimu alitahayari kufuatia tukio hilo, kwani aliziba pua yake kwa kutumia koti lake na kuuliza chanzo cha mtuhumiwa kufanya kitendo hicho kortini, lakini katika hali iliyoashiria kama ni kiburi, kijana huyo hakujibu chochote zaidi ya kutazama chini, licha ya swali hilo kurudiwa zaidi ya mara tatu.Kutokana na kosa hilo ambalo liliharibu na kusimamisha karibu shughuli zote za mahakama kwa muda, Hakimu Mutaki alimhukumu kijana huyo kwenda jela kwa muda wa miezi sita ili kuwa fundisho kwa wengine wenye tabia hiyo.
Kana kwamba haitoshi, askari waliokuwepo mahakamani hapo walilazimika kumchapa bakora kijana huyo ili kumlazimisha kupiga deki baada ya eneo hilo kuchafuka vibaya kwa kinyesi kilichochanganyika na mkojo.

Friday, September 13, 2013

Huu ndio mjengo wa Madee uliopo Mbezi jijini Dar

Raisi wa Manzese, Madee anatarajia kuhamia Mbezi sasa, na huko sijui kama atakuwa Raisi au niaje niaje. Nasema hivyo kwasababu Madee ameonyesha picha ya mjengo wake uliokamilika kwa asilimia kubwa uliopo maeneo ya Mbezi jijini Dar.

kukamilika kwa mjengo huo kumetokana na mafanikio makubwa aliyoyopata baada ya kukubalika kwa single yake "Pombe Yangu"
hiki ndicho alichokiandika madee 
"siri ya utajiri ni ubahiriii#hahaha welkam white houze@mbezi dsm#"

H Baba na Flora Mvungi wapata mtoto wa kike wampa jina la Tanzanite

Msanii H Baba na mkewe Flora Mvungi wamefanikiwa kupata mtoto wa kike jana jioni majira ya saa 12:30 katika hospitali ya Maria Stope iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam.


Kama unakumbuka hapo awali H Baba alisema kama akifanikiwa kupata mtoto wa kike au kiume basi atampa jina 'Tanzanite' hatimaye amefanikiwa kupata wa kike na kumpatia jina la Tanzanite.

Hii ndio cake ya birthday ya Ommy Dimpoz na ujumbe aliouandika kwa familia marafiki na mashabiki wake

Tarehe 13 / 09 ni siku ya kuzaliwa hitmaker Omari Fereji Nyembo a.k.a Ommy Dimpoz, na huu ndio ujumbe wake kwa familia,marafiki na fans wake.

I would like to thank God for the blessings he has showered me with over the years and especially during my professional musical career!! Saying Allah is great it truly an understatement. Next to him is#TeamPozKwaPoz. Mad love to my fans cause truly without you I am Nothing. Fans, family & friends, you are the pillar of my success and you are irreplaceable... Happy Birthday to ME!! And I'm thankful for everything good or bad as they all have shaped me to be the man I am today. Come celebrate life health and music with me tonight at Elements Lounge. My brothers j martins, AY and FA will be there as well making sure it's more than a birthday!! Tupogo, ama nini?!!

Happy Birthday ommy Dimpoz

Unaambiwa huyu ni mwanasiasa mwenye umri mdogo kuliko wote duniani

4yearold_mayorb.jpgWRobert ‘Bobby’ Tufts hajaanza hata shule ya  Nursery ambayo huku Tanzania tunaifahamu kama chekechea au vidudu lakini tayari ameshajiwekea historia ya kuwa mwanasiasa mwenye umri mdogo kuliko wote duniani .
Dogo huyo ameweza kuwa meya wa mji mmoja huko Minesotta akiwa na umri wa miaka mitatu pekee, unaambiwa ni Meya wa mji mdogo wa Dorset ulioko huko Minesotta Marekani na hii ni mara yake ya pili kuchaguliwa kuwa meya wa mji huo baada ya kupigiwa kura siku ya jumapili ambapo aliweza kushinda kipindi chake cha pili cha uongozi .
Mstahiki Meya wa Mji wa Dorset Robert 'Bobby' Tufts.
Mstahiki Meya wa Mji wa Dorset Robert ‘Bobby’ Tufts.
Mji huo una serikali ndogo inayoongozwa na meya huyo mdogo ambaye anaongoza idadi ya watu 220 ambao ni wakazi wa mji huo ambapo kama ilivyo kwenye manispaa yoyote, meya Bobby anaongoza serikali ambapo hufanya maamuzi yanayohusu bajeti ya matumizi ya mji wa Dorsett pamoja na masuala mengine nyeti kama ya kodi na makusanyo mengine ya mapato.
Mama mzazi wa Meya Robert Tufts, Emma Tufts anasema kuwa moja ya agenda za uongozi wa mwanaye ni kukusanya fedha kwa ajili ya taasisi ya misaada ya Ronald McDonald iliyoko Dorset eneo la Red River Valley Fargo Dakota ya Kaskazini pamoja na ujenzi wa kibao kipya cha kuwakaribisha wageni huko Dorset kwenye barabara zinazopakana na miji mingine.
4yearold_mayorc.jpgWTaarifa za Meya huyo mdogo kuliko wote duniani zimefika mpaka ikulu kwa Barack Obama ambae amempa Robert Tufts mwaliko maalum kwenye ikulu yake na ana mpango wa kumfanya kuwa mshauri wake maalum kwenye mfuko wake unaofahamika kama ObamaCare Foundation.

Mama amnyonga mwanae wa miezi 9


111111111111111111111111 Mara nyingi huwa tunasikia mama kamtupa mwanae baada ya kumzaa, lakini hii imekua mbaya zaidi baada ya mama kumyonga mwanae wa miezi tisa. Habari kutoka KTN inaeleza zaidi kuhusu hiki kisa.




Ratiba nzima ya movie kuanzia 13 hadi 19 September kwenye theater za Dar na Arusha ipo hapa


687883034_2108327899001_pain-and-gain-trailer-still
Wiki hii movie mpya inayoonyeshwa wiki hii kwenye theaters za hapa Tanzania ni Pain and Gain. Movie hii ni true story ambayo ilitokea huko Miami, angalia hapa trailer yake na ukaangalie kwenye theater uipendayo


1185935_10151699887733842_997317895_n
1239831_505685009505787_531302041_n
1208707_576530562408211_53189326_n 1229971_10151699879423842_134378913_n 1230027_10151699885198842_554494605_n


SERIKALI YAANDAA MAPENDEKEZO YA KUTUNGA SHERIA MPYA YA KUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA

Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi akiwaeleza wanahabari (hawapo pichani) kuhusu mapendekezo ya serikali kutunga sheria mpya ya kudhibiti dawa za kulevya.
Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa akijibu baadhi ya maswali ya wanahabari.
Wanahabari wakifuatilia mkutano huo.
Serikali imeandaa mapendezo ya kutunga sheria mpya ya kudhibiti dawa za kulevya nchini. Tatizo la matumizi na biashara haramu ya dawa za kulevya limekuwa kero nchini hasa kumaliza nguvu kazi ya taifa.
Hayo yamesemwa  na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi  alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za tume ya kuratibu dawa za kulevya jijini Dar Salaam.
Aidha amesema kuwa Tanzania inakabiliwa na tatizo la matumizi ya dawa  za kulevya ambalo  huchangiwa na mambo mbalimbali yakiwemo; tamaa ya kutaka utajiri wa haraka na mmomonyoko wa maadili .
Amesema madhara ya dawa hizo ni makubwa  ikiwa ni pamoja na kuathiri afya za watumiaji , ongezeko la uhalifu na magonjwa ambukizi kama vile homa ya ini, kifua kikuu na UKIMWI.
Aliongeza kusema kuwa serikali imekuwa ikifanya jitihada za kupambana na tatizo hilo kwa muda mrefu sana ikiwemo kufuta baadhi ya sheria zilizokuwa zikitumika tangu wakati wa ukoloni ambapo mwaka 1995 Sheria ya Kuzuia Biashara Haramu ya dawa za kulevya [Sura 95] inayotumika hadi sasa ilitungwa.
Sheria hii ilianzisha Tume ya Kuratibu  Udhibiti wa  Dawa za Kulevya ambayo iko chini Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa lengo la kuratibu na kusimamia tatizo la Dawa za kulevya nchini
Tume hii imekuwa ikishirikiana na vyombo mbalimbali vya dola vinavyojihusisha na tatizo hili kama  vile Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa, Idara ya Uhamiaji, Idara ya Ushuru wa Forodha na Asasi za Kiraia.

Juma Kaseja atua Ndanda FC ya Mtwara

Juma Kaseja.
Na Nicodemus Jonas
KIPA namba moja wa Taifa Stars, Juma Kaseja dili lake la kwenda kuichezea FC Lupopo ya DR Congo halieleweki na kusisitiza kuwa ameamua kujiunga na timu ya Ndanda FC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza kwa ajili ya mazoezi ili kujiweka fiti kipindi hiki ambacho hana timu.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Kaseja ambaye alimaliza mkataba wake na Simba msimu uliopita, alisema kabla ya kusafiri na timu ya taifa, alikuwa akifanya mazoezi na timu hiyo, ingawa anaendelea kufanya mazoezi kwa manufaa ya afya yake.
Aliongeza kuwa, suala la usajili wa Lupopo hapendi kulizungumzia kwa sasa kwa kuwa yeye bado ni mchezaji huru, lakini baada ya Ndanda kuondoka kwenda Mtwara juzi Jumatano, amejikita zaidi kuendesha shughuli zake binafsi.
“Nimekuwa nikifanya mazoezi na Ndanda, lakini baada ya kuondoka, ninaendelea na shuguli zangu binafsi, siyo lazima kuzijua,” alisema Kaseja huku akiwa hayupo tayari kufafanua kwa undani juu ya usajili wake wa kwenda Lupopo.
Ndanda ilikuwa jijini Dar es Salaam ambapo ilicheza mechi za kirafiki dhidi ya Saigon ya Mwananyamala na Ruvu Shooting ya Pwani, ambapo itaanza kucheza mechi za Daraja la Kwanza keshokutwa Jumapili dhidi ya Friends Rangers kwenye Uwanja wa Nang’wanda, Mtwara.

HII NI BABA LAO!

Stori: Richard Bukos na Issa Mnally
MDOSI au Kanjibai aliyefahamika kwa jina moja la Milah ambaye ni bosi wa kampuni moja ya ujenzi yenye makao yake Mwenge jijini Dar alinaswa chooni akiwa na mfanyakazi wake, John Carlos ‘Shabani’ (watu walimpachika jina la Shabani kutokana na Kanjibai wa kwenye Komedi) ikidaiwa walikuwa katika mazingira ya ulawiti, Ijumaa ‘Kubwa’ lina sinema yote.
...Choo walipokuwa wamejifungia Milah 'Kanjibai' na John Carlos ‘Shabani’.
Ishu hiyo nzito ilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo wawili hao walikuwa chooni humo kwa zaidi ya nusu saa na kuwasababishia usumbufu watu waliokuwa wakitaka kutumia choo hicho.
KISA KILIPOANZA
Siku hiyo ya tukio, mtu mwenye sauti ya kiume alipiga simu kwenye chumba cha habari cha Global Publishers, Mwenge jijini Dar na kupasha juu ya tukio hilo. Alisema:
“Jamani hebu njooni haraka hapa kwenye hii kampuni ya ujenzi ya… (jina lipo) iko hapa Mwenge. Kuna bosi wetu mmoja amejifungia chooni na mfanyakazi mwenzetu kwa zaidi ya robo saa sasa, sijajua nini kinaendelea humo ndani. Sisi wengine hapa matumbo ya kuendesha yametushika sijui tufanyaje?!”
Mtoa habari huyo alikwenda mbele zaidi kwa kuwaambiwa mapaparazi wetu waliompokelea simu wachukue Bajaj au Bodaboda ili kuwahi.
Sosi huyo kabla ya kukata simu aliweka wazi ramani ya kufika kwenye choo hicho na kusisitiza kwamba muhimu kuwahi kwa sababu huenda wanagombana.
MAPAPARAZI WAWASHA PIKIPIKI
Kufuatia msisitizo huo, mapaparazi wetu makini  waliwasha pikipiki zao, kila mmoja na yake na kushika njia kuelekea eneo la tukio.
Hata hivyo, kwa kuamini wanaweza kukutana na lolote, waliona ni vyema kwanza kwenda kutoa taarifa kwenye Kituo Kidogo cha Polisi cha Mwenge ambapo walipewa askari wawili kuelekea eneo la tukio.

...Ndani ya choo walimokutwa.
ENEO LA TUKIO SASA
Timu hiyo iliwasili kwenye eneo la tukio. Mlango wa choo hicho ulikuwa umefungwa lakini kwa mara moja tu haikuwa rahisi kugundua kama ulifungwa kwa funguo au kawaida tu.
 Afande mmoja alijitolea kugonga mlango wa choo hicho ili kupima ushirikiano utakaotolewa na wawili hao au mmoja wao.
Sauti iliyoonekana ni ya Kanjibai kutokana na kushindwa unyoofu wa lugha ya Kiswahili ilisikika ikiuliza:
“Nani wewee… taka nini huku?”
...Wakiwa chini ya ulinzi.
Afande: Sisi ni askari polisi, fungua haraka tunajua mko wawili humo ndani, fungua.
Kanjibai: Subiri kidogo.
Baada ya dakika kadhaa ambazo mapaparazi wetu hawakuzifuatilia, mdosi huyo alifungua mlango na kukutwa akiwa na ‘Shabani’.
WALICHOKUWA WAKIKIFANYA CHOONI
Katika maswali ya harakaharaka nje ya choo hicho kila mmoja alisema la kwake ambalo aliliamini linaweza kumchomoa kwenye skendo hiyo mbaya.
‘Shabani’ alisema yeye aliingia kwenye choo hicho baada ya kuitwa na bosi wake huyo ambapo alishindwa kumkatalia kwa kuogopa kupoteza ajira yake na kama inavyojulikana maisha ya Dar bila kazi ni ngumu kuyamudu.
...Mafuta aliyokutwa nayo Kanjibai ambayo mtaani hujulikana sana kwa jina la ‘mlainisho’.
Alipoulizwa walichokuwa wakikifanya ndani ya choo hicho, Shabani alibaki akiwatumbulia macho maafande, wakati mwingine mapaparazi wetu.
Kwa upande wake Kanjibai alipotakiwa kujieleza kisa cha kuingia chooni na mfanyakazi wake, alisema alimuomba wazame humo ili akamnyoe. Yaani Kanjibai alitaka kunyolewa.
IKAFIKA ZAMU YA KUPELEKWA KITUONI
Afande mmoja aliamuru wawili hao wapelekwe kituo cha polisi, lakini kabla ya kuanza safari, mdosi huyo aliingiza mkono kwenye mfuko wa suruali na kutoa vitu vyake kadhaa na kuwakabidhi wadosi wenzake waliofika ‘kumsaidia’ muda mfupi baada ya kunaswa.
Halafu aliingiza mkono kwenye mfuko mwingine na kutoa mafuta aina ya KY (pichani) ambayo mtaani hujulikana sana kwa jina la ‘mlainisho’ lakini askari alimwambia mafuta hayo yanatakiwa kituoni kwa ajili ya ushahidi hivyo asiwape nduguze.
Breki ya kwanza ilikuwa kwenye Kituo Kidogo cha Polisi Mwenge ambapo baada ya mahojiano mafupi walihamishiwa Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’ ambapo walihojiwa zaidi kuhusiana na tukio hilo.

Monday, September 2, 2013

Uzuri wako Jux (Official Video)



MZEE GURUMO: DIAMOND MUNGU ATAKULIPA

MZEE GURUMO: DIAMOND MUNGU ATAKULIPA

Makala: Shakoor Jongo na Musa Mateja
Habari ya mjini wikiendi iliyopita ilikuwa ni juu ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kumzawadia gari nguli wa muziki wa dansi aliyestaafu muziki hivi karibuni, Mzee Muhidin Gurumo aliyekuwa akiitumikia Msondo Music Band.
Tukio hilo lililoibua maneno kibao lilijiri ndani ya Serena Hotel, Posta jijini Dar wakati Diamond au Sukari ya Warembo akizindua video ya wimbo wake mpya wa My Number One na kuhudhuriwa na raia wa kada mbalimbali wakiwemo mastaa wa muziki, filamu, wakurugenzi wa makampuni na watu wa kawaida.
Wakati Diamond akimkabidhi Mzee Gurumo ufunguo wa gari hilo aina ya Fan Cargo lenye thamani ya Sh. milioni 6 alisema:
“Nikikutajia jina la Muhidin Gurumo, basi utajua namzungumzia nani. Ni nguli wa muziki wa dansi nchini Tanzania.
“Takriban wiki imepita tangu kusikika kwa habari za kweli kuhusu kustaafu muziki kwa Mzee Gurumo, binafsi sikuwahi kukutana naye hadi leo hii nilipokutana naye kwenye uzinduzi wa video yangu.
“Nilimualika mzee huyu kwa mapenzi yote, nilisikia juzi pia akisema amekuwa akipendezwa na staili ya muziki wangu na kucheza pia, hayo ni mojawapo ya mambo yaliyonivutia kutaka kumuona mzee huyu.
“Nilipitia kwenye mitandao mingi huku ikiandikwa kuwa kutokana na kazi ya Mzee Gurumo ameweza kuwa kwenye fani zaidi ya miaka 50 lakini hakuwahi kubahatika hata kuwa na baiskeli.
“Jambo hili lilinigusa na kuniumiza moyoni, kuona nguli kama huyu wa muziki ananena vile na kuomba msaada, binafsi leo usiku nimemtunuku gari jipya mzee Gurumo kwenye uzinduzi wa video yangu.
“Nimeamua kutoa kwa moyo mmoja na kwa mapenzi yangu yote kwa mzee wangu.”
Baada ya kukabidhiwa funguo hizo na kutoa shukrani zake kwa kumuombea Diamond baraka kwa Mungu, wanahabari wetu walitaka kusikia anazungumziaje tukio hilo ambapo alisema: “Diamond Mungu atamlipa. Ni kweli nimestaafu bila baiskeli lakini yeye kanipa gari. Mungu ambariki sana.”

GARAMA
Kwa mujibu wa Diamond, video hiyo ambayo itaanza kuruka hewani leo, imetengenezwa na Ogopa Djs nchini Afrika Kusini na imegharimu dola za Kimarekani 30,000 (zaidi ya Sh. milioni 48) huku uzinduzi huo ukigharimu Sh. milioni 18. Haijawahi kutokea Bongo!

WEMA HASIKII kwa Rommy Jonson.

WEMA HASIKII

Na Gladness Mallya
LICHA ya kunaswa katika matukio tofauti, Wema Sepetu hasikii. Safari hii imenaswa picha inayomuonesha akimshushia busu motomoto jamaa anayefahamika kwa jina la Rommy Jonson.
Wema Sepetu akimbusu Rommy Jonson.
Picha hiyo ambayo inamuonesha Wema akiwa anambusu jamaa huyo katika pozi lenye hisia kali za kimalovee, imenaswa juzikati katika mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo wadau mbalimbali walioiona kwa mara ya kwanza, walitoa maoni yao.
“Mh! Jamani Wema sasa amezidi hata huyu naye? Kama ni picha ya kawaida kwa nini aoneshe hisia za kimalovee kiasi hiki? Kuna kitu,” alihoji mdau mtandaoni ingawa Wema hakujibu chochote.

NI KWELI WANAWAKE WAMEWAZIDI WANAUME KWA MAMBO HAYA 10?

NI KWELI WANAWAKE WAMEWAZIDI WANAUME KWA MAMBO HAYA 10?

1. Wana Nguo Nyingi Kuliko Wanaume.
2. Wanafahamu Nani Ni Baba Halisi Wa Watoto Wao.
3. Ni Wepesi Kupenda Na Wakipenda Hupenda Kweli.
4. Wanaoga Mara Nyingi Zaidi Kwa Siku.
5. Wana Huruma Sana Ingawa Mara Nyingi Huwa Inawaponza.
6. Wana Uwezo Wa Kubadilisha Tabia Ya Mwanaume Muda Wowote.
7. Wana Uwezo Wa Kuishi Na Kupendeza Bila Kuwa Na Kazi Wala Biashara Yoyote.
8. Kwao Nywele Na Kucha Ndo Vitu Vya Kwanza Kufikiria Wakitaka Kutoka.
9. Wana Uwezo Wa Ku-Pretend Kwa Muda Mrefu Zaidi Hasa Kwenye Mapenzi.
10.
Wanaujua uchungu wa mwana sana.
    
Tupia Nyingine Unayodhani Nimeisahau...