Friday, September 13, 2013

SERIKALI YAANDAA MAPENDEKEZO YA KUTUNGA SHERIA MPYA YA KUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA

Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi akiwaeleza wanahabari (hawapo pichani) kuhusu mapendekezo ya serikali kutunga sheria mpya ya kudhibiti dawa za kulevya.
Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa akijibu baadhi ya maswali ya wanahabari.
Wanahabari wakifuatilia mkutano huo.
Serikali imeandaa mapendezo ya kutunga sheria mpya ya kudhibiti dawa za kulevya nchini. Tatizo la matumizi na biashara haramu ya dawa za kulevya limekuwa kero nchini hasa kumaliza nguvu kazi ya taifa.
Hayo yamesemwa  na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi  alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za tume ya kuratibu dawa za kulevya jijini Dar Salaam.
Aidha amesema kuwa Tanzania inakabiliwa na tatizo la matumizi ya dawa  za kulevya ambalo  huchangiwa na mambo mbalimbali yakiwemo; tamaa ya kutaka utajiri wa haraka na mmomonyoko wa maadili .
Amesema madhara ya dawa hizo ni makubwa  ikiwa ni pamoja na kuathiri afya za watumiaji , ongezeko la uhalifu na magonjwa ambukizi kama vile homa ya ini, kifua kikuu na UKIMWI.
Aliongeza kusema kuwa serikali imekuwa ikifanya jitihada za kupambana na tatizo hilo kwa muda mrefu sana ikiwemo kufuta baadhi ya sheria zilizokuwa zikitumika tangu wakati wa ukoloni ambapo mwaka 1995 Sheria ya Kuzuia Biashara Haramu ya dawa za kulevya [Sura 95] inayotumika hadi sasa ilitungwa.
Sheria hii ilianzisha Tume ya Kuratibu  Udhibiti wa  Dawa za Kulevya ambayo iko chini Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa lengo la kuratibu na kusimamia tatizo la Dawa za kulevya nchini
Tume hii imekuwa ikishirikiana na vyombo mbalimbali vya dola vinavyojihusisha na tatizo hili kama  vile Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa, Idara ya Uhamiaji, Idara ya Ushuru wa Forodha na Asasi za Kiraia.

No comments:

Post a Comment