Wednesday, January 22, 2014

B ENKI KUU YA TANZANIA YATOA SARAFU YA SH 50,000....ANGALIA HAPA



Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa sarafu maalumu ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye thamani ya sh 50,000.
Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, alisema jana kuwa sarafu hiyo iliyotengenezwa kwa madini ya fedha kwa asilimia 92.50, imetolewa kwa ajili ya kumbukumbu tu na haitaingizwa katika mzunguko wala kutumika kwa kulipia malipo ya aina yoyote.


Sarafu hii imetolewa maalumu kama maadhimisho ya miaka 50 ya mapinduzi ya Zanzibar, haitatumika kwa manunuzi.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki ya BoT ilimnukuu Profesa Ndulu akisema sarafu hiyo imetolewa kwa idadi ya vipande 3,000 kwa ajili ya tukio hilo na kuwahimiza wananchi kuinunua kwa ajili ya kumbukumbu hiyo.

Kwa mujibu wa Gavana, kutolewa kwa sarafu hiyo kunakwenda sambamba na utaratibu wa Benki Kuu kutoa sarafu maalumu za aina hiyo kama sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya matukio mbalimbali muhimu ya kitaifa na kimataifa.

Kwa kawaida, baada ya muda, thamani ya sarafu kama hizi huongezeka na kuwa na faida zaidi kwa wanaozimiliki,” alisema Profesa Ndulu.
Gavana Ndulu alieleza sarafu hizo zitapatikana Januari 5 kwa bei ya sh 50,000 katika matawi ya benki za biashara zitakazokuwa zimepata sarafu hizo kutoka Makao Makuu ya Benki Kuu, Dar es Salaam na matawi ya Benki Kuu yaliyoko Zanzibar, Arusha, Mbeya na Mwanza.
Benki za biashara zinaweza pia zikasambaza sarafu hizi kupitia matawi yake,” alisema gavana na kuongeza taarifa za usambazaji zitatolewa na benki hizo.
Katika sarafu hiyo, upande wa mbele unaonyesha sura ya hayati Sheikh Abeid Aman Karume na maandishi yanayosomeka: ‘Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi’. 
Upande mwingine wa sarafu unaonyesha nembo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, maandishi yanayosomeka: “Miaka Hamsini ya Mapinduzi”, thamani ya sarafu na miaka 1964-2014.
-Tanzania daima

Zile mali za mastaa, mwimbaji Barnaba nae katuonyesha hii ndio nyumba aliyojenga.

Screen Shot 2014-01-22 at 1.38.10 AMSio kwamba mastaa wa zamani wa bongofleva hawakuwa wanapata chochote kwenye malipo kutokana na kazi zao bali  imefahamika kwamba mipangilio na matumizi mazuri ya fedha havikuzingatiwa sana kwa baadhi ya Wasanii wachache ambao walibahatika kuzipata pesa nyingi zilizotokana na mauzo ya kanda na show.
Wasanii wengi wa bongoflevani sasa hivi wameshtukia mchezo ndio maana wengi wao wanaingia kwenye headlines za kuonyesha mali zao kama nyumba na magari siku kadhaa tu baada ya kusikika kwenye chati za bongofleva ambapo hii kwa kiasi kikubwa ni kutokana na malipo ya show zao, wengine mauzo ya nyimbo kwenye miito ya simu, dili za makampuni na ishu nyingine.
Barnaba ni miongoni tu mwa waimbaji wenye talent zao na amekua akifanya showz mbalimbali hata nje ya Tanzania pamoja na kupata dili za mashirika/taasisi mbalimbali na kufanya nao kazi zikiwemo za ubalozi mfano Pepsi, Barclays Bank na wengine kama unavyoweza kuona moja ya stori zake za mwaka 2013.

Picha mpya za Rihanna zinazo-make headline kwenye internet hivi sasa

0Rihanna ame-share picha zake akiwa kwenye mapumziko huko Brazil ambazo zinasambaa sana hivi sasa kwenye mtandao.
Rihanna akiwa Brazil ametumia muda huo pia kupiga picha kwa ajili ya cover ya Vogue Magazine.
Hizi picha amezipiga akila good time kwenye yatch.
6
5
4
3
2
1

Ajali nyingine yatokea asubuhi hii Mtwara.


lattestTaarifa iliyotufikia hivi punde ni kuhusu ajali ambayo imetokea asubuhi hii ya leo majira ya sa 12 huko Mtwara ambayo imehusisha wanafunzi wa Shule ya Secondary ya Mustapha Sabodo ambao walikua wanakimbia mchaka mchaka.
Chanzo cha ajali hiyo kinasema kuwa kuna Gari ndogo aina ya Benzi ilimgonga mwanafunzi mmoja aliyekuepo kwenye mchamchaka huo baada ya wanafunzi kuona hali hiyo katika hali ya taharuki ndipo bila kuangalia nyuma lori lingine likaja kuwagonga wengine.
Taarifa mpaka sasa ni kwamba mwanafunzi mmoja amefariki pale pale na wengine watatu wamefariki hospitali,idadi ya majeruhi mpaka sasa ni zaidi ya 20,Dereva wa Benzi amejisalimisha kwenye kituo cha polisi Mtwara,ingawa dereva wa lori amekimbia.
Millardayo.com inaendelea kufatilia taarifa hizi.

Ya huyu Mwanamke wa Russia kukalia hiki kiti chenye umbo la Mwanamke wa Kiafrika umeiona?


Screen Shot 2014-01-22 at 9.57.10 AM
Russian Socialite ambae ni muhariri wa jarida la Garage magazine, Dasha Zhukova akiwa pia ni patner wa mmiliki wa club ya Chelsea Roman Abramovich, ameingia kwenye maporomoko ya matusi na maoni mengine mazito ya watu mbalimbali mtandaoni baada ya kusambaa kwa picha inayomuonyesha akiwa amekaa kwenye kiti kilichotengenezwa kwa mfano wa Mwanamke wa Kiafrika.
Mwanamke huyu ambae anasema ana mapenzi na fashion pamoja na usanii wa vitu kama hivi amekosolewa na wengi ambapo baadhi ya Wanawake hata wenye ngozi kama ya Dasha, wamemkosoa huku wengine wakiuliza ‘bado tunafanya vitu hivi mpaka huu mwaka wa 2014?’
Screen Shot 2014-01-22 at 9.38.20 AMKiti hiki kimedizainiwa na msanii raia wa Norway Bjarne Melgaard ambapo baada ya kupostiwa kwa picha hii kwenye mitandao akiwa anafanyiwa interview na tovuti ya Buro 24/7 , muda mfupi baadae waliitoa hii picha na kuomba radhi kwa kitendo hicho.
Sehemu ya maelezo yao ilisema ‘sio nia yetu kuendeleza au kufanya ubaguzi kwa binadamu yeyote’

Unataka kuwaona wanaotuhumiwa kushambulia Westgate? tazama walipokwenda eneo la tukio chini ya ulinzi

2Ripota wangu wa nguvu Julius Chemitei kutoka Nairobi anaripoti kwamba Hakimu na pande husika dhidi ya washukiwa wa shambulio la Westgate wametembelea eneo la tukio kutekeleza amri iliyotolewa na hakimu mkuu Daniel Ojenja wiki iliyopita kabla ya kesi hiyo kuahirishwa.
Hakimu Daniel Ochenje alizungumza na waandishi kwenye hii ziara na kusema umuhimu wa ziara hiyo ni kuwezesha pande husika kupata taswira ya eneo hilo wakati Mashahidi wanapolihusisha eneo la tukio kwenye ushahidi wao Mahakamani.
Mawakili wa washukiwa wanaendelea kusimamia kwamba wateja wao hawana hatia yoyote na baada ya ziara hiyo walikua tayari kuendelea na kushirikiana na Mahakama wakati wakisubiri uamuzi kutolewa.
Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa tarehe 27 & 28 January 2014 wakati upande wa mashtaka ukitarajiwa kuwasilisha mashahidi wengine 28 ambapo hata hivyo kumekuwa na malalamiko kutoka kwa mawakili wa upande wa Washukiwa kwamba viongozi wa mashtaka hawajawapa taarifa za polisi zilizoandikishwa na mashahidi.
3
1
6Hawa ni baadhi wa washukiwa wenyewe wanaotuhumiwa kuhusika na shambulio la Westgate.
5
4

Loga akesha, kisa Yanga SC



 

Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic.
Na Hans Mloli
POINTI tatu katika mechi nne za mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, zimemfanya Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, akose usingizi.
Logarusic, raia wa Croatia, maarufu kama Loga, amesema kati ya pointi hizo 12, tatu ni zile dhidi ya Yanga na amekuwa akipiga hesabu atazipata vipi kwa kuwa wakikutana anatambua ‘patachimbika’.
Akizungumza na Championi Jumatano, Logarusic amesema anajua mechi dhidi ya Yanga itakuwa ngumu sana lakini anazihitaji pointi zao tatu.
“Ndiyo pointi za Yanga ni muhimu sana, lakini jumla pointi 12 za mzunguko wa pili ndiyo zinaninyima usingizi.
“Mechi dhidi ya Yanga, Coastal Union, Mtibwa Sugar na Azam FC. Najua itakuwa kazi ngumu kuzipata, lakini nazitaka, ni muhimu sana kwetu kimahesabu,” alisema Loga.
Katika timu nne anazozihofia, mbili kati ya hizo, Loga ameishacheza nazo katika mechi ambazo si za mashindano.
Loga alikutana na Yanga katika mechi ya Nani Mtani Jembe na kuifunga mabao 3-1 wakati alipocheza na Mtibwa Sugar katika mechi ya kirafiki, kikosi chake kililala bao 1-0.
Tangu aanze kuifundisha Simba, haijawahi kucheza na Azam FC wala Coastal Union ambayo imefunga safari hadi nchini Oman kujiandaa na Ligi Kuu Bara.
Iwapo Logarusic atafanikiwa kukusanya pointi hizo 12 za timu hizo vigogo, maana yake atakuwa katika nafasi ya kutwaa ubingwa.
Simba inafungua dimba la mzunguko wa pili Jumapili, wakati watani wao Yanga na vinara wa ligi hiyo watatangulia dimbani Jumamosi.
Kuhusiana na mechi ya Jumamosi, Loga ametabiri kwamba wapinzani wao Yanga watashinda kirahisi.

ANGALIA ALAMA HIZI, ANZA MWAKA NA FIKRA MPYA!-4

KUTAMBUA alama za nyakati na kuangalia maisha yako ni jambo la msingi sana rafiki zangu. Kwa majuma matatu mfululizo yaliyopita, tumeona alama nyingi za wenzi ambao siyo sahihi kutokana na tabia zao.
Tulianza kwa kuwaangalia wanawake, tukaingia kwa wanaume ambapo tunaendelea pale tulipoishia kabla ya kugeukia katika ushauri kwa wote. Wiki iliyopita tuliishia pale ambapo mwanamke humshusha mwanaume waziwazi kwa matendo yake.
Mfano kusifia wanaume wengine mbele ya mwenzi wake au kufanya jambo lolote linaloashiria kuwa yupo naye lakini si kwa malengo ya muda mrefu.
Hebu sasa tuendelee kujifunza...
HATAOLEWA NA WEWE!
Mwanamke huyu anaweza kuzungumzia kuhusu kuolewa lakini siyo na wewe. Mathalani, anaweza kusema: “Duh! Mwanaume atakayenioa atakuwa na kazi sana.”
Kauli hiyo ni tata na mara zote haina maelezo mengine yoyote mbele yake.
Ni kweli anajua kwamba ataolewa siku moja, lakini wewe huna chako. Anamuwaza mwanaume mwingine kabisa. Hata hivyo, hawezi kukuambia mojamoja, atatumia tenzi, ngano na methali katika kufikisha ujumbe huu kwako.
MASHARTI KIBAO
Mwanamke huyu ni mjanja sana, anaonekana ana mambo mengi, ni kama hataki mapenzi yajulikane, lakini mbaya zaidi kwa kuwa anajua wazi kwamba hana mapenzi na wewe hataki umharibie!
Ana masharti kibao ambayo hayaeleweki. Hapendi muongozane, hasa kwenye sehemu zenye watu wengi. Hata kama ikilazimika kufanya hivyo, hukuchagulia mahali pa kupita.
HANA WIVU...
Hafikirii sana kuhusu kusalitiwa, hana muda na simu yako na wala haonyeshi dalili zozote za kujali sana penzi lako. Hafikirii kwamba siku moja unaweza kumsaliti. Hana muda huo.
Anaweza kukudhihirishia hili moja kwa moja, hata pale utakapokuwa umepanga kutoka naye, halafu ghafla akakuambia amepata dharura lakini atakupa rafiki yake uende naye kwenye pati. Hili ni tatizo na ni lazima uwe nalo makini kwa kiwango cha mwisho.
Mwanamke ambaye hana wivu, kuna mapenzi kweli hapo? Hana shida na wewe ndiyo maana basi hafikirii sana kuibiwa. Iache akili yako itafakari hili kwa makini, mwisho wa siku utajua cha kufanya.
RATIBA ZISIZOELEWEKA
Ana mambo mengi sana ambayo hayaeleweki, pengine ana ratiba zake kabisa, lakini hakuweki! Yeye anawaza mipango yake kama yeye na inawezekana kabisa hujui ratiba zake na hajakuambia.
Hata kama alikuambia, siyo ratiba yake kamili. Kimsingi hataki ufahamu kabisa juu ya mambo yake. Hii nayo ni alama tosha ambayo itakufanya uelewe kwamba upo katika penzi la wizi. Hakuna anayekupenda hapo.
USHAURI KWA WOTE
Mapenzi siyo kitu cha mchezo, umakini ni jambo la kwanza kabisa ambalo unatakiwa kuwa nalo katika uhusiano. Siku zinazidi kwenda mbele, sasa hakuna sababu ya kuendelea kupoteza muda kwa mtu ambaye umeshagundua kuwa hakupendi.
Hana ‘future’ na wewe, hawazi kwamba unaweza kuwa wake wa maisha siku moja, wakati wewe ukiwaza hayo, mwenzako anawaza mambo mengine. Upo naye kwa ajili ya mapenzi ya dhati, mwenzio yupo kwa sababu ya kustarehe tu.
Tafakari kwa makini, lakini kuna sifa zaidi za kuziangalia ili kuona kama mwenzi uliyenaye ni kweli anafaa kuwa wako wa maisha au unapoteza muda wako. Hata kama anakupenda lazima uwe na sababu zako za kumfanya awe wako wa maisha.
Mambo yafuatayo ni muhimu zaidi kuzingatia wakati ukiwa katika uhusiano ambao unahitaji uwe wenye malengo. Tuendelee kujifunza...
NI WA NDOTO ZAKO?
Jambo kubwa kuliko yote ambalo unatakiwa kuliangalia kwa jicho la tatu ni kama mwenzi huyo ni wa ndoto zako. Je, yukoje? Siku zote kabla ya kuamua kufanya chochote lazima ujiulize kama ndicho ulichokuwa ukikifikiria.
Hata kwa upande wa mwenzi wako, lazima ujiridhishe, ni kweli ni yule uliyekuwa unamtarajia? Ana sifa unazohitaji? Acha tabia ya kujifariji kwamba utampenda taratibu ndani ya ndoa, hicho kitu hakipo.
Hakuna kujifunza kupenda katika ndoa, lazima ujihakikishie mwenyewe kuwa mwenzi wako ni yule mwenye sifa ulizokuwa ukizitarajia. Hili ni la msingi, maana unaweza kuwa naye siku mbili, ukatamani mwingine nje. Kwa  nini? Kwa sababu si yule mwenye sifa ulizotarajia.

MMILIKI WA YANGA AIBUKA, ATAKA KWENDA KWA KIKWETE


Juma Mwambelo.
Na John Joseph
ALIYEJITANGAZA kuwa mmiliki wa klabu ya Yanga, Juma Mwambelo, amesema yu tayari kukabidhi nyaraka zinazotafutwa na uongozi wa klabu hiyo kwa Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga, alitangaza kwenye mkutano wa Yanga kwamba Mwambelo anashikilia hati za umiliki wa klabu ya Yanga kimakosa na anatakiwa kuzikabidhisha haraka iwezekanavyo kabla ya kuchukuliwa hatua.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mwombelo alisema yupo tayari kumpa Rais Kikwete naye aukabidhi uongozi wa Yanga chini ya Yusuf Manji.
“Kweli hati hizo ninazo kwa kuwa mimi ni mmiliki wa Klabu ya Yanga, ila Rais Kikwete pekee ndiye naweza kumkabidhi, hata mwanaye Ridhwani nimewahi kumueleza kuhusiana na hili,” alisema.
“Mimi ndiye mmiliki wa Klabu ya Yanga, nina hati miliki halali ya klabu, hii hapa (anaonyesha), nina hati miliki ya jengo la Jangwani, pia ninayo ya jengo la Mafia, lakini hiyo waliiba na tayari nilisharipoti polisi.
“Kuhusu hati ya jengo la Jangwani ipo benki na yenyewe sijailipia kwa kuwa kuna deni, deni hilo ni zile fedha ziliyotumika kujenga Uwanja wa Kaunda. Hivyo,
deni likilipwa benki itakubali kutoa hati kisha kuirudisha wizarani na kutolewa rasmi.
“Nashangaa Yanga wanapodai wanatumia katiba mpya, hii siyo halali, katiba halali ya Yanga ni ile ya mwaka 1967 ambayo nakala yake hii hapa (anaonyesha),” alisema.
Alipoulizwa juu ya uhalali wa wanachama wa sasa wa klabu hiyo, alisema: “Wanachama wengine wote ni feki, mpaka unatokea mgawanyiko mwaka 1975, wanachama halali wa Yanga walikuwa 400, kuanzia hapo hakuna wanachama halali tena, hata akaunti zinazotumika siyo za klabu.
“Hapa nilipo nimekuja polisi (Magomeni) ili kutoa taarifa ya kujihami, nahofia kupigwa kutokana na walichokisema kwenye mkutano,” alisema.
Katika mkutano mkuu wa Jumapili, uliofanyika kwenye Ukumbi wa Karume, PTA Sabasaba jijini Dar es Salaam, uongozi wa Yanga ulimtaja mzee Juma kuwa ndiye aliyeiiba hati ya jengo la klabu hiyo tangu Juni 24, 2009.
“Mimi nilipigwa na watu mwaka 1987 nikapoteza fahamu kwa siku tano, tangu pale sijawahi kwenda klabuni wala uwanjani kuitazama Yanga, hata huyo Mrisho Ngassa simjui, namuona tu kwenye magazeti, kikubwa ninachotaka ni utaratibu ufuatwe ndani ya Klabu ya Yanga,” alisisitiza huku akitabasamu.

WAZIRI JOHN MAGUFULI, NOMA

Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Ujenzi, John Pombe Magufuli, wikiendi iliyopita alidhihirisha yeye si mtu wa kubabaika, badala yake anachapa kazi kulingana na kauli mbiu ya ari, nguvu na kasi zaidi.
John Pombe Magufuli akikagua ujenzi wa Daraja la Kigamboni.
Jumapili iliyopita, wakati Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Yohana Sefue, akitangaza mabadiliko ya nafasi za mawaziri na manaibu wao kama Rais Jakaya Kikwete alivyoteua, Magufuli alikuwa ‘bize’ akikagua ujenzi wa Daraja la Kigamboni.
Magufuli akiendelea na ukaguzi wa daraja hilo.
Kutokana na kitendo hicho, baadhi ya waliomshuhudia walisema: “Huyu ndiye kamanda, aisee ni noma sana!”
Kauli hiyo, ilitokana na ukweli kwamba Magufuli hakuwa na wasiwasi wala mchecheto kuhusu nafasi za mawaziri na kuonesha kwamba anajiamini na yupo kikazi zaidi, ndiyo maana aliamua kuzipa kisogo taarifa kutoka ikulu na badala yake kusimamia ujenzi wa daraja hilo ambalo linatajwa kuwa la kihistoria.

Daraja la Kigamboni.
“Muda ambao Magufuli alikuwa anakagua ujenzi wa Daraja la Kigamboni, mawaziri na manaibu wengi walikuwa wakifuatilia taarifa ya Balozi Sefue kwenye vyombo vya habari kuhusu mabadiliko yaliyofanywa na Rais Kikwete.
“Magufuli hakujali kabisa hilo, ndiyo maana alichokifanya ni kwenda kukagua daraja hilo ambalo likikamilika, litaacha heshima kubwa kwa Rais Kikwete,” alisema Mwisege Kimbati katika maoni kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter.

Rebecca Mwizarubi katika maoni yake Facebook, alisema: “Ni Jumapili, ni wikiendi, watu wapo kwenye mapumziko, wengine wanastarehe kama siyo na familia basi katika viwanja mbalimbali lakini Magufuli yupo kazini anachapa kazi. Tunahitaji viongozi wa aina yake. Magufuli ni hazina ya nchi hii.”

Daraja la Kigamboni linaloendelea kujengwa.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa mitandao mingi ‘iliposti’ picha hizo za Magufuli na wachangiaji wake walimsifu Magufuli kwa kupiga kazi bila kujali kwamba ilikuwa Jumapili, vilevile kwa kutokuwa na wasiwasi kuhusiana na taarifa ya mabadiliko ya mawaziri.

MUONEKANO MPYA WA MREMBO WEMA SEPETU

Pichani juu ni taswira za Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu alizotupia katika ukurasa wake wa Instagram ambapo mojawapo aliandika hivi "For my baby... yes you...". Mrembo huyu kwa sasa yupo na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz'.

Monday, January 13, 2014

PUB YA AUNT EZEKIEL CHALI

Stori: Shakoor Jongo
PUB iliyoibuka kwa muda mchache na kukamata ‘taito’ kubwa Bongo ya mwigizaji Aunt Ezekiel, Demonte imefungwa ghafla, haitoi huduma tena.
Aunt Ezekiel.
Imedaiwa kuwa, pub hiyo iliyopo maeneo ya Mwananyamala, jijini Dar, imefungwa kutokana na mhusika kushindwa kuiendesha.
“Imefungwa, nasikia gharama za vinywaji na wafanyakazi aliowaajiri zilikuwa juu akaona bora afunge,” alisema rafiki wa Aunt aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Paparazi wetu alishuhudia pub hiyo ikiwa imefungwa kwa zaidi ya miezi kadhaa, alipomtafuta Aunt, hakupatikana hadi tunakwenda mitamboni.

MBOTO: SIJAWAHI KUTOKA NA AUNT EZEKIEL

KAMA kawa, kama dawa, wiki iliyopita tulimleta kwenu ‘komediani’ kiraka Bongo, Haji Salum almaarufu Mboto ambaye mulimuuliza maswali magumu ambayo wiki hii anayajibu na kuchambua moja baada ya lingine. UNGANA NAYE…
ATAOA LINI?
Mboto wewe ni mchekeshaji mahiri kunako kiwanda cha maigizo Bongo, je, unategemea kuoa lini? Salim Liundi, Dar, 0658110395
MBOTO: Asante, suala la kuoa siyo la kukurupuka kwa hiyo inahitaji utulivu na kuoa kwangu siyo leo wala kesho.
FILAMU
Hivi Mboto ulishawahi kutoa filamu yako mwenyewe na kama umewahi kutoa inaitwaje? Kama hujawahi kutoa tatizo ni nini? Muddy Madiley, 0652672805
MBOTO: Nimefanya filamu yangu inaitwa Bana Kongo nimeigiza kama Mkongomani lakini bado haijatoka, inatarajiwa kutoka ndani ya mwezi huu.
USHAURI
Haina ubishi una kipaji kikubwa katika uigizaji ila nakukumbusha usimsahau Mungu kwani ndiye kila kitu na ambaye amekuwezesha kufika hapo ulipo. Amiri Salumu, Dar, 0653252416
MBOTO: Asante ila mimi ninamwamini sana Mungu na kabla sijaanza kufanya kazi lazima nimuombe Mungu kwanza.
TAHADHARI
Mboto upo juu sana, mimi binafsi nakukubali mzee, kikubwa jitahidi usije ukawa na skendo. Pia muangalie Kinyambe (mchekeshaji) anakuja juu sana. Msomaji, 0716089050
MBOTO: Nashukuru, ni kweli na siyo Kinyambe tu kuna wasanii chipukizi wengi wanaokuja kwa kasi lakini mimi ninaendelea kupigana zaidi ili niendelee kufanya vizuri.
PONGEZI
Kaka Mboto nakukubali sana kunako gemu la uigizaji kama Filamu ya Kibajaji, hongera ila ningependa kujua umeoa na una watoto wangapi? Naika, Dar, 0657433268
MBOTO: Bado sijaoa ila nina mtoto mmoja.
Aunt Ezekiel.
AUNT EZEKIEL?
Mboto nafurahi sana kila nikikuona. Je, wewe ni Mpemba kweli? Je, ni kweli ulishawahi kutoka kimapenzi na Aunt Ezekiel? Sarha, Dar, 0653358681
MBOTO: Mimi siyo Mpemba bali ni Mzaramo wa Mtanga, sijawahi kutoka na Aunt Ezekiel na sijawahi kufikiria kwa sababu tumeshakuwa kama ndugu yeye ananiita kaka na mimi namuita dada.
NJE YA FANI
Nje na fani ya uchekeshaji unajishughulisha na kazi gani nyingine? Msomaji, 0755708366
MBOTO: Mimi ni mfanyabiashara
HISTORIA
Nakukubali sana Mboto, ningependa kujua historia yako japo kwa kifupi. Bahati, Mbeya, 0753280224
MBOTO: Nimezaliwa Temeke na kusoma hukohuko, sanaa nimeanza nikiwa sekondari na nilijiunga rasmi na Kundi la Kaole Sanaa mwaka 1999.
Baada ya hapo nikiwa na wasanii wengine tuliunda kundi letu lililoitwa Katavi ambalo tulitengeneza mchezo wa kwanza uliokuwa ukirushwa na Runinga ya ITV ulioitwa Jabali. Pia tulitengeneza Tamthiliya ya Tunduni iliyokuwa ikirushwa na Star TV.  Baada ya michezo hiyo ndipo nikaingia kwenye filamu mpaka sasa.
MIPANGO
Kaka Mboto wewe ni mahiri na mchekeshaji bora wa filamu, je, una mipango gani hapo baadaye katika filamu? Stella Maeda, Dar, 0653648869
MBOTO: Nina mpango wa kuanzisha kampuni yangu ya filamu nifanye kazi na wasanii chipukizi.
ANAJISIKIAJE?
Mboto wewe ni msanii mkubwa uko juu sana katika sanaa ya uigizaji  hongera kwa hilo, unajisikiaje pale unapocheza muvi na Aunt Ezekiel na Monalisa? Msomaji, 0652952688
MBOTO: Huwa najisikia faraja sana kwa sababu ni watu ambao wanaielewa sanaa hawana nyodo, hakuna kuwaelekeza sana tofauti na wengine ambao wana majina makubwa lakini unawaelekeza mpaka unachoka.
MAFANIKIO
Mboto ni mafanikio gani umepata tangu ulipoanza sanaa? Fredy, 0786930888
MBOTO: Nimejuana na watu wengi na kuwa na marafiki wengi ambao wamenipa ushauri kama hivi ninafanya biashara na miradi ambayo sitaki kuiweka wazi kwa sasa.

MONALISA HOFU YA JUJU

Stori: Mayasa Mariwata
STAA wa filamu Bongo, Yvone Cherry ‘Monalisa’ amesema anaogopa kuweka wazi mambo yake kwa kuhofia kupigwa juju hivyo anaishi kwa siri.
Yvone Cherry ‘Monalisa’.
Akipiga stori na paparazi wetu, Monalisa alisema amejifunza maisha ya usiri na ndiyo maana huwa haaniki hata tarehe, mwezi au mwaka wa kuzaliwa kwani watu wabaya hutumia nafasi hiyo kukuangamiza.
“Asikudanganye mtu ukishaanika tu hivyo vitu mtu akajua na majina yako yote kuna nini tena hapo zaidi ya kukufanyia ndumba uharibikiwe anavyojisikia yeye, huwa inaniwia vigumu sana kuweka hadharani vitu vyangu,” alisema Monalisa.

MAN CITY YAKWEA KILELENI ENGLAND

London, England
NEWCASTLE United jana walishindwa kuuzuia muziki wa Manchester City kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-0 kwenye Uwanja wa St James.
Ushindi huu umewafanya City kuongoza ligi hiyo kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya Chelsea inayoshika nafasi ya pili baada ya kujikusanyia pointi 47 kati ya 46 za Chelsea.
Hata hivyo, Arsenal ambayo inacheza leo Jumatatu na Aston Villa inaweza kuzishusha timu zote hizo kama itaibuka na ushindi.
Bao la kwanza la City liliwekwa kimiani na mshambuliaji hatari Eden Dzeko, katika dakika ya nane tu ya mchezo baada ya mabeki wa Newcastle kushindwa kuuokoa mpira uliopigwa katikati ya lango lao.
Katika dakika za nyongeza wakati Newcastle wakishambulia kwa nguvu kubwa, Negredo aliambaa na mpira na kuifungia timu yake bao la pili.
Newcastle walionyesha kiwango kizuri kwenye mchezo huo lakini walijikuta wakipoteza nafasi nyingi za wazi.
Hata hivyo, mchezo huo umekuwa pigo kwa City baada ya wachezaji wake wawili, Samir Nasri na Yaya Toure kuumia na kutolewa uwanjani.
Nasri alitolewa kwa machela baada ya kugongwa na Yanga-Mbiwa, huku Toure akitoka mwenyewe baada ya kugongwa na Cheikh Tiote.
Newcastle wapo katika nafasi ya nane wakiwa na pointi 33 baada ya kucheza michezo 21.

WAANDISHI MAHIRI WA HABARI WANAHITAJIKA HARAKA


Global Publishers & General Enterprises LTD, kampuni inayoendelea kukua katika tasnia ya habari nchini, kwa mwaka 2014 ina nafasi za kazi za uandishi mahiri wa habari kwa wenye elimu, ujuzi na sifa zifuatazo:
ELIMU NA SIFA:
Wanahitajika waandishi mahiri wenye elimu ya Degree, Advanced Diploma au Diploma ya uandishi wa habari, wenye ufahamu wa kutosha kuhusu masuala ya habari za michezo na burudani ndani na nje ya Tanzania.
Kwa wasiokuwa na ujuzi lakini wenye vipaji, elimu ya kutosha na mapenzi ya dhati na tasnia ya uandishi, watapewa nafasi ya kujifunza ili kujipatia uzoefu.
Aidha, mtarajiwa awe kijana aliye tayari kuanza kufanyakazi wakati wowote. Awe anajua kutumia kompyuta. Awe na uwezo wa kufanyakazi bila kusimamiwa, mwenye ubunifu, aliyetayari kufanya kazi usiku na mchana. Mwenye kumiliki na uwezo wa kutumia kamera ana nafasi nzuri ya kuchaguliwa kwanza.
Mwisho:
Kama unafikiri unakidhi vipengele vyote vilivyoainishwa hapo juu, tuma barua yako ya maombi ya kazi haraka, iliyoandikwa kwa mkono wako ukiambatanisha na maelezo yako ya kikazi (CV) na nakala ya cheti/vyeti
vyako, kwa:
MENEJA MKUU
S.L.P 7534
DAR ES SALAAM
Wasilisha mwenyewe ofisini kwetu, Sinza Bamaga (Nyuma ya TSN
Petrol Station). Simu: 2773356/7. Mwisho wa kupokea maombi ni
Januari 15, 2014.

OPERESHENI TOKOMEZA YA PILI KUANZA KARIBUNI

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.
WAKATI hatua zaidi zikisubiriwa kuchukuliwa kwa watendaji waliohusika na ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa Operesheni Tokomeza, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kutangaza kuanza kwa awamu ya pili ya Operesheni hiyo wakati wowote kuanzia sasa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, alisema wakati wowote Rais Kikwete atatangaza kuanza kwa Awamu ya Pili ya Operesheni Tokomeza na itazingatia haki zote ikiwemo haki za binadamu.
Nyalandu alisema ingawa awamu ya kwanza kulikuwa na kasoro zilizojitokeza, awamu hii ya pili kasoro hizo zitafanyiwa kazi ili kuhakikisha rasilimali za Taifa zinalindwa.
Kusitishwa kwa operesheni hiyo kulikosababisha uteuzi wa mawaziri watatu kutenguliwa na waziri mmoja, kujiuzulu kwa mujibu wa Nyalandu, kulisababisha pia tembo 60 kuuliwa.
Mawaziri ambao uteuzi wao ulitenguliwa na Rais Kikwete mwishoni mwa mwaka jana ni Dk Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani ya Nchi), Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa) na Dk David Mathayo (Maendeleo ya Mifugo) huku Balozi Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), akijiuzulu.
Katika hatua nyingine, Nyalandu amemsimamisha kazi Ofisa Wanyamapori Mwandamizi wa Pori la Akiba la Maswa, Lawrence Kileo, ambaye anatuhumiwa kupokea rushwa na kuwatoza faini wafugaji wanaoingiza mifugo ndani ya pori la akiba bila kuwapa risiti halali ya Serikali.
Pia, ameamuru mamlaka husika kukamilisha uchunguzi na kuchukua hatua za kinidhamu haraka dhidi ya Ofisa Wanyamapori wilayani Kasulu mkoani Kigoma, Benjamin Mkasamali. Ofisa huyo anatuhumiwa kuwatorosha majangili ambao waliwinda wanyamapori wasioruhusiwa kuwindwa katika kibali kinachotolewa na Serikali.
Nyalandu alisema Kileo amesimamishwa kazi, kutokana na makosa ya kupokea rushwa na kuwatoza faini wafugaji wanaoingiza mifugo ndani ya pori la akiba bila kuwapa stakabadhi ya Serikali, kinyume na Kifungu 116(2) (c) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Namba 5 ya 2009.
Mkasamali anachunguzwa baada ya Wizara kutumia njia za kiintelijensia na kubaini kuwa aliingilia kati na kuwaachia huru majangili, waliokamatwa na kikosi cha doria cha Kampuni ya Friedkin Conservation Fund.
Majangili hao wanadaiwa kuwinda wanyama aina ya tohe 12, madume watano na majike saba, ambao hawakuwepo katika orodha ya leseni yao ya uwindaji namba B59921, iliyotolewa na ofisa huyo Novemba 29 /2013. Pia majangili hao waliua wanyamapori wengine wanne aina ya oribi.
Alisema baada ya Mkasamali kuwaruhusu majangili hao kuondoka, ambao tayari walishakamatwa na kikosi cha doria, kiongozi wa kikosi hicho aliwasiliana na RPC Kigoma, Freiza Kashai.
Inadaiwa Kamanda Kashai alitoa ushirikiano kwa kumwagiza OC CID Kasulu, Athuman Namba ambaye alishirikiana na Ofisa Usalama Taifa Kasulu, ambao kwa pamoja waliweka kizuizi sehemu ya Kibagwe njia ya kwenda Kigoma na kukamata majangili hao na kurudishwa Kasulu, ambako wamefunguliwa kesi.    


MIRROR, MASTAA BONGO MUVI WACHENGUA CLUB 71 TEGETA

Wema na Kajala wakishindana kunengua jukwaani.
Wema Sepetu akiimba na Mirror.
Mastaa wa Bongo Muvi, wakiwa jukwaani pamoja na msanii Mirror.
Jacqueline Wolper akikamua.
Msanii Mirror akimchombeza Wolper.
Baadhi ya mashabiki wakifuatilia onyesho hilo.
Paparazi wa Global Publishers  Shakoor Jongo (mwenye fulana  nyekundu) akiwa katika picha ya pozi na Kalala Junior (kulia) na mashabiki waliohudhuria onyesho hilo.
UKUMBI wa Club 71 ulioko Tegeta, jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamikia leo ulirindima kwa show bab’kubwa ya msanii Mirror kutoka kampuni ya Endless Fame aliyesindikizwa na madiva katika Bongo Muvi kina Wema Sepetu, Kajala Masanja na Jacqueline Wolper.