Chanzo cha ajali hiyo kinasema kuwa kuna Gari ndogo aina ya Benzi ilimgonga mwanafunzi mmoja aliyekuepo kwenye mchamchaka huo baada ya wanafunzi kuona hali hiyo katika hali ya taharuki ndipo bila kuangalia nyuma lori lingine likaja kuwagonga wengine.
Taarifa mpaka sasa ni kwamba mwanafunzi mmoja amefariki pale pale na wengine watatu wamefariki hospitali,idadi ya majeruhi mpaka sasa ni zaidi ya 20,Dereva wa Benzi amejisalimisha kwenye kituo cha polisi Mtwara,ingawa dereva wa lori amekimbia.
Millardayo.com inaendelea kufatilia taarifa hizi.
No comments:
Post a Comment