WIKI
iliyopita mwigizaji Jennifer Kyaka ‘Odama’ alifafanua mambo mbalimbali
aliyopitia maishani likiwemo suala la kuficha ujauzito na mambo mengine
ambayo yawezekana ulikuwa huyajui juu yake.
Leo tunamalizia makala haya kwa kutazama majibu ya maswali mbalimbali ambayo nilimuuliza na kuyatolea ufafanuzi. UNGANA NAYE…
Mwigizaji wa filamu za kibongo Jennifer Kyaka ‘Odama’
Mwandishi: Wasanii mnatajwa sana kwenye masuala ya ushirikina ili mng’ae kisanii, kwa nini msimtegemee Mungu?
Odama: Uchawi upo, huwezi kuukwepa lakini inategemea
na mtu anaundekeza kiasi gani. Binafsi siamini katika hayo mambo.
Namtegemea Mungu zaidi.
Mwandishi: Malengo yenu kama kampuni ni nini katika gemu la filamu za Kibongo?
Odama:
Kama kampuni malengo yetu makubwa ni kuvuka mipaka ya Tanzania na
kufanya vizuri zaidi ya Wanigeria ambao wanaonekana kututangulia
kimaendeleo.
Mwandishi: Kila mtu kwenye sanaa huwa anakuwa na mtu aliyemvutia hadi kuingia, kwa upande wako, ni nani alikufanya uingie kwenye sanaa?
Odama: Msanii ambaye alikuwa akinivutia kabla
sijaanza uigizaji ni Monalisa (Yvonne-Chery Ngatwika). Uhalisia wake
katika uigizaji ndiyo kitu kilichokuwa kikinivutia kwake ndiyo maana
nikaamua kuingia kwenye sanaa.
Mwandishi: Wasanii wengi mnatajwa kuwa mnakwenda nchi za nje kujiuza, hili unalizungumziaje?
Odama:
Kila mtu ana uhuru wa kusema kile anachojisikia lakini kwa upande wangu
sina ‘comment’ (maoni) kwa sababu mimi huwa nikienda nje ya nchi
nafuata ishu maalum.
Mwandishi: Ishu maalum ndiyo ipi maana hata wewe uliwahi kutajwa katika sakata hili.
Odama:
Weee, uniache kabisa. Mimi mara nyingi nakwenda kwa kazi maalum. Kwa
mfano safari yangu ya mwisho kwenda (China) nilifuata vifaa vya ofisi
kama kamera na vitu vingine.
Mwandishi: Tunafahamu huna muda mrefu
tangu ujifungue, lini sasa utaanza kuingia mzigoni au utabaki kama
mkurugenzi na hutaigiza tena?
Odama: Hobi yangu ni kuigiza, siwezi kuacha fani hii
kwa sababu naipenda. Nasubiri tu mtoto atimize miezi mitatu, nitaanza
kazi kama kawaida. Sasa hivi ana miezi miwili.
Mwandishi: Naona umekuwa bongenyanya, huoni kama inaweza kukuharibia ukapoteza mvuto wa kimwonekano utakapoanza kuigiza?
Odama: Ni kweli kwa sasa nimenenepa sana, lakini nafikiria kuanza mazoezi taratibu na nina imani mwili wangu wa kawaida utarudi tu.
Mwandishi: Kwa nini usianze sasa mazoezi, huoni kadiri muda unavyozidi kwenda na wewe unazidi kunenepa?
Odama: Siwezi kuanza mazoezi kwa sasa kwa sababu
nilijifungua kwa oparesheni hivyo lazima nikae kama miezi sita hivi
ndiyo nipige mazoezi ya nguvu kuepuka kufumua mshono bure.
Mwandishi: Wasanii kwa sasa mna makundi katika mitandao ya kijamii,
utakuta timu flani imemdiss flani, hivi unaona kuna umuhimu wowote kwa
msanii kuwa na hizo timu?
Odama: Mimi sioni ubaya wa kuwa na hizi timu kwa
sababu zinamfanya msanii azungumze kwa ukaribu na mashabiki wake ila
tatizo linakuja kwa wale ambao wanazitumia kwa kurushiana matusi, hapo
ndipo tatizo linapokuja. Tukizitumia vizuri, hazina madhara.
Mwandishi: Katika maisha yako ya sanaa, ulishawahi kukwazwa na jambo au msanii mwenzako ukateseka kila wakati.
Odama: Huwa napenda kufurahi na kusahau kila wakati, siwezi kukaa na dukuduku moyoni hivyo kama yalitokea nimeshayasahau. Sikumbuki.
Mwandishi: Msanii gani wa kiume anakuvutia jinsi anavyoigiza kwa sasa?
Odama:
Walikuwepo wengi huko nyuma ila kama ulivyosema kwa sasa namkubali
zaidi Gabo, ni msanii mzuri sana sema kama watu wengi hawajamshtukia.
Mwandishi: Mashabiki wako wangependa kumjua baba wa mtoto huyo na pengine mna mipango gani?
Odama: Mtoto wangu anaitwa Jason kuhusu baba yake
watamjua siku si nyingi, wasikonde! Mipango inakuja wakae mkao wa
kula.Mwandishi: Asante kwa ushirikiano wako tangu mwanzo hadi mwisho.
Odama: Karibu sana, nawapenda wote.