Friday, August 29, 2014

RAIS KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA MBANDE-KONGWA 16.5KM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakwanza kushoto akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi pamoja na Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai wakifurahia mara baada ya Rais kuweka jiwe la Msingi Ujenzi wa Barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km .
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi, Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma pamoja na kikundi cha ngoma za asili cha Kibaigwa kabla ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuhutubia mamia ya Wakazi wa Kibaigwa.
Sehemu ya barabara Mbande-Kongwa 16.5Km ambayo ujenzi wake umewekwa jiwe la Msingi.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kulia akizungumza na Mbunge wa Kibakwe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa George Simbachawene huku Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai akishuhudia kushoto.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katikati akizungumza na Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya(kulia) kabla ya uzinduzi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya uzinduzi na ufunguzi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zake wakimsubiri Rais Dkt. Jakaya Kikwete kuzindua rasmi mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km. Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi

RATIBA YA MAKUNDI YA MABINGWA ULAYA



CRISTIANO RONALDO MCHEZAJI BORA ULAYA


Mchezaji nyota wa Ureno na Real Madrid, Cristiano Ronaldo akibusu tuzo yake ya Mwanasoka Bora wa Ulaya baada ya kukabidhiwa usiku wa kuamkia leo mjini Monaco, Ufaransa.
Cristiano Ronaldo akifurahia.
Wachezaji wa Bayern Munich, kipa Mjerumani Manuel Neuer (kushoto) na winga Mholanzi Arjen Robben (kulia) pamoja na Ronaldo (katikati) akifurahia baada ya kushinda tuzo hiyo.

MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM LA KATIBA AVITAKA VYOMBO VYA HABARI KUANDIKA HABARI BILA KUPOTOSHA UMMA


Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta akiongea na waandishi wa Habari huku akiwaasa kuacha chuki katika masuala yanayohusu mchakato wa Katiba.
Mjumbe wa Kamati Namba Nne ya Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Christopher Ole Sendeka akiongea na wandishi wa Habari kuhusu kazi na majukumu ya Kamati yake jana 28 Agosti, 2014.
Mjumbe wa Kamati Namba Tatu ya Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Dkt. Francis Michael akiongea na wandishi wa Habari kuhusu kazi na majukumu ya Kamati yake jana 28 Agosti, 2014.
Mjumbe wa Kamati Namba Moja ya Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Ummy Mwalimu Ally akiongea na wandishi wa Habari kuhusu kazi na majukumu ya Kamati yake jana 28 Agosti, 2014.
Mjumbe wa Kamati Namba Kumi na Moja, Mhe. Hamad Massauni akiongea na wandishi wa Habari kuhusu kazi na majukumu ya Kamati yake jana 28 Agosti, 2014. (Picha zote na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma).

KAMPUNI YA MATANGAZO YANAYOTEMBEA (TRIA) YAZINDULIWA RASMI TANZANIA

1q
DIANA LAVENDER Meneja Mauzo na Masoko kampuni ya CONICA MINOLTA akisoma risala yake wakati wa uzinduzi wa matangazo hayo.
2q
TRUSHAR KHETIA Mkurugenzi Mtendaji wa TRIA akikata utepe wakati akizindua rasmi matangazo hayo nchini Tanzania, wa pili kulia ni ZULFIKAR MOHAMED Meneja Mkuu wa kampuni ya TRANSPAPER EXPRESS na mwisho kulia ni DIANA LAVENDER Meneja Mauzo na Masoko kampuni ya CONICA MINOLTA na kushoto ni AZDA AMANI Meneja wa Huduma Shirika la ndege la PRECISION AIRLINE ambao ni wateja wa kampuni ya TRIA.
Kampuni ya matangazo kwa kutumia vifaa tembezi yaani matangazo yanayotembea imezinduliwa rasmi jijini Dar esSalaam.
Akiongea na waandishi wa habari pamoja na wageniwengine waliohudhuria katika hafla hiyo ya uzinduzi ulifanyika katika hanga la shirika la ndege la Precision yenye makao makuu yake eneo la uwanja wa ndege jijini Dar esSalaam, mkurugenzi mtendaji na muasisi wa TRIA bw. Trushar Khetia amesema kuwa TRIA ni kampuni ya kimataifa inayojishughulisha na matangazo yawekwayo juu, nje au ndani ya fifaa safirishi kama mabasi ya kusafiria ndani na nje ya miji, ndege na usafiri wa majini maarufu kama boti au meli.
“Tumezoea kuona ama kusikia matangazo malimbali ya kibiashara nay ale ya kijamii yaani matangazo yasiyo ya kibiashara yakifanyika kupitia kwenye TV REDIO magazeti na majarida hapa nchini lakini leo TRIA inawathibishia wafanya biashara wa Tanzania na wengine kuwa matangazo yanaweza kufanyika popote wakati wowote tena kwa gharama ndogo” alisema bwana Trushar na kuongeza kuwa TRIA ina lenga kuwainua watanzania hasa vijana wadogo na kuwafanya watambue fursa zao katika maisha sambamba na kuwaongezea matumaini makubwa wamiliki wa mabasi, ndege, daladala namakapuni ya usafirishaji katika kunufaika kutokana na biashara zao za usafirishaji.
Aidha bwana Trushar amesema kuwa kampuni yake pamoja na kwamba haitegemi kufanya biashara kwa hasara hailengi pia kutengeneza faida tu bali kuleta ufanisi na changamoto endelevu katika sekta ya masoko na matangazo ambapo vijana wadau na wateja wa huduma hiyo wataweza kupiga hatua za kimaendeleo kibiashara sambamba na kuongezeka kwa soko la ajira hususana kwa vijana wa kitanzania “TRIA Tanzania hailengi kutengeneza faida tu bali pia kuleta maendeleo yenye tija kibiashara kwa wale watakaokuwa wateja wetu na wadau kwa ujmla, lakini pia ajira kwa vijana wenye uwezo tofauti tofauti wa kufanya kazi pamoja na wale wenye utaalamu wa kuandaa na kutengeneza matangazo haya” alisema Khetia.
Kwa upande wake mwakili wa Conica katika hafla hiyo Bi Diana Lavender amesema Conoca imekuwa mteja mkubwa wa TRIA nchini Kenya na kwakutambua ubora wa kazi zinafanywa naTRIA Conica imeamua kuunga na TRIA kwakuendelea kufanya matangazo yake hapa chini “tumekuwa wateja wa hii kampuni mda mrefu sasa huko nchini Kenya na kutoka na mafanikio makubwa tumeweza kupata kupitia matangazo yetu yanayofanywa na TRIA tumeonelea kuwa ni vizuri kuja kufanya hayo matangazo hapa Tanzania hasa pale tuliposikia kwamba TRIA inaanzisha tawi hapa nchini” alisema Lavender na kuongeza kuwa kufanya matangazo kupitia mabasi, ndege, daladala, treni, vyombo vya usafiri wa majini ni sehemu ya mapambo ya mji na njia zake kwani matangazo haya hutengenezwa vizuri na kufanya kuvuta macho ya wengi kila ipitapo “ni ma mabasi yetu huko Kenya maarufu kama matatu ukipita ukiona vile inavutia lazima utafurahia na kwamba lazima unaweza kutaka kupanda hiyo basi” aliongeza.
Naye mwakilishi kutoka shirika la ndege la precision hapa nchini ambao ni moja kati ya wadau wa karibu kabisa na TRIA Bi Azda Amani amesema kuwa uwekezaji wa biashara mbalimbali hasa biashara ngeni kama hayo ni sehemu ya kuongeza na kukuza pato la taifa na kupitia kodi kwa kampuni husika lakini pia kwa wamiliki wa mabasi, ndege na vinginevyo pamoja na wale wamiliki wa matangazo yatakawekwa kwenye magari haya watalipia kodi “ni furaha kuona wawekezaji wakubwa na wadogo wakiingia kila siku hapa nchini kuwekeza kibiashara na kwakufanya hivi nchi yetu ina kuwa pia kiuchumi kupitia kodi kutoka kwa watoa huduma na wahudumiwa wa huduma hii muhimu kwa maendeleo ya uchumi na biashara nchini” alisema Amani
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Zulfikar Mohamed kutoka Transpaper ameisifia TRIA kwa hatua iliyofikia na kuwataka watanzania kuiga mfano huo muhimu na kwenda kuwekeza pia katika nchi jirani hata kimataifa “ mimi nipewa fursa ya kuzindua tawi la TRIA hapa Tanzania na kwakweli nimefurahia fursa hii.
Naomba kuwapongeza sana wahusika wote waliokaa na kuona kwamba mimi naweza kuwa mgeni rasmi wa kuzindua mradi huu muhimu lakini pia nawasifia watanzania kwa kuwa waungwana wakubwa sana kuwapokea wawekezaji kutoka pande zote za dunia bila kujali rangi kabila wa udini, kwa hili mko vizuri sana na nawapongeza sana niwaombe tu kwamba igeni huu mfano mzuri na nyinyi mkawekeze biashara zenu katika nchi nyingine kwa manufaa ya watoto wenu na watanzania wote” alisema Mohamed nakuongeza kuwa maendele ya kiuchumi katka taifa lolote huletwa na wenye nchi kupitia biashara yenye tija na inayovuka mipaka na kuleta fedha za kigeni.

WAPIGANAJI WA ISIS WATOA ONYO LINGINE KWA MAREKANI



Mateka 15 wa Kikurd wanaoshikiliwa na wapiganaji wa ISIS.
SAA chache baada ya kuuwa wanajeshi 300 wa Syria, Kundi la wapiganaji wa ISIS limetoa onyo lingine kwa Marekani likiachia video inayowaonyesha mateka 15 wa Kikurd ambao nao watauawa iwapo Marekani haitaondoa majeshi yake.

ISIS wamesema wataendelea kuwachinja mateka hao mpaka Marekani itakapoondoa majeshi yake.
Katika video hiyo, Kundi la ISIS linaonekana likimchinja mmoja wa mateka hao wa Kikurd waliokamatwa wakati wa mapigani nchini Iraq.

Wapiganaji wa ISIS wakiwaswaga wanajeshi zaidi ya 200 waliokamatwa katika ngome ya anga ya Tabqa nchini Syria katika jangwa kuelekea eneo la mauaji.

Tuesday, August 12, 2014

Bunge kutumia zaidi ya Tsh milioni 142 kukodi vipaza sauti


mic
Wakati kukiwa na malalamiko kwamba Bunge la maalumu la Katiba linagharimu fedha nyingi za walipakodi, uongozi wa taasisi hiyo umetumia Sh142.56 milioni kukodi vipaza sauti kutoka kituo cha mikutano cha kimataifa Arusha (AICC).
Katibu wa Bunge maalumu Yahya Khamis Hamad alithibitisha kukodiwa kwa vipaza sauti hivyo kwa ajili kamati zote 12 na kwamba kila gharama ya chumba kimoja kwa siku ni Dola 450 za Marekani (Dola moja ni wastani wa Sh1,650).
Kwa maana hiyo Bunge hilo linatumia Dola 5,400 sawa na Sh8.91 milioni kwa siku kugharimia vipaza sauti katika vyumba 12 vinavyotumiwa na kamati hizo na kwa siku 16  ambazo kamati zitakutana, jumla gharama hizo zitafikia Sh142.56.
“Vifaa vya sauti tulivyokuwa navyo vinalalamikiwa vilikuwa siyo standard (viwango) hasa vya mazungumzo, tumekodi kutoka ukumbi wa mikutano wa AICC na tumekuwa nao usiku mzima kuvifunga,” alisema katibu wa bunge.

Ushahidi mwingine wa Chris Brown na Rihanna wapo karibu kurudiana


chrisBaada ya siku moja tu Chris Brown ku-post poster la tour ya Rihanna na Eminem kwenye instagram, Chris Brown ameonekana kuendelea kuongeza ukaribu zaidi na Rihanna.
Japokuwa picha haipo clear sana lakini inaonyesha Chris Brown alivyokwenda back stage ambapo alikuwepo Rihanna kwenye moja ya show za tour hiyo.
Picha haionyeshi vizuri lakini kuna mashahidi wengi wanasema kwamba Chris Brown alikuepo backstage akiwa na Tyga na welienda kwa ajili ya Rihanna.brown

NAY NDIYE ‘MDUDU’ NDOA YA WEMA


Stori: Shakoor Jongo
IMEVUJA kwamba Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ndiye aliyemshauri Nasibu Abdul ‘Diamond’ asioe kwa sasa ili asishuke kimuziki.
Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’
Ushauri huo umekuwa mwiba kwa mpenzi wa Diamond, Wema Sepetu ambaye amekuwa na ndoto ya kuolewa na staa huyo anayekimbiza kitaani na wimbo wake wa Mdogomdogo.
Wema Sepetu akiwa na mpenzi wake 'Diamond Platinum'.
Akifafanua zaidi kuhusiana na ushauri huo, Nay alisema: “Kuna mifano mingi sana nimeiona kutoka kwa wasanii ambao wameoa, wengi wao wameshasanda sasa mdogo wangu (Diamond) na yeye alipoleta hoja ya kutaka kuoa nikaona sasa anatafuta shimo la kwenda kujifukia, nikamshauri aache.”

MATUKIO 9 YALIYOFURAHISHA


MAKALA: gladness mallya
Ijumaa iliyopita ni siku ambayo haitasahaulika kwenye kumbukumbu za wengi kutokana na kufanyika kwa tamasha kubwa la Usiku wa Matumaini ndani ya Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yafuatayo ni mambo tisa yaliyotingisha kwenye tamasha hilo.
Ali kiba wa Bongo Fleva akimtoka 'Cloud' wa Bongo Muvi.
MECHI YA BONGO MUVI  VS BONGO FLEVA
Timu hizo zilipoingia uwanjani kupasha misuli, watu walisimama na kuanza kushangilia kwa nguvu huku wakilitaja jina la Ali Kiba na zaidi walifurahi walipomuona Jacob Stephen ‘JB’. Matokeo ya mechi hiyo, Bongo Fleva waliwalaza Bongo Muvi kwa  bao 1-0.
Wasanii wa Bongo Muvi wakicheza kiduku.
VIDUKU VYA BONGO MUVI
Japokuwa walifungwa, wanawake wa Bongo Muvi walionekana wakicheza kiduku huku mashabiki wakiwashangilia kwa nguvu na kuleta shangwe za aina yake.
'Sir Nature' akifanya makamuzi.
SHOO KALI YA ROMA, JUMA NATURE
Wakali hawa wa muziki wa Bongo Fleva waliwafurahisha sana mashabiki ambapo uwanja mzima ulisimama na kucheza huku wakiimba nyimbo za wasanii hao wakati wakipafomu.
'Cloud' akimbwaga 'JB' ulingoni.
NDONDI ZA JB, CLOUD
JB na Cloud 112 walionekana kama wanaigiza kwani walikuwa wanadondoka mara kwa mara wakati pambano baina yao likiendelea, baadaye JB aliibuka na ushindi.
Mashabiki wakifuatilia shoo uwanjani.
MASHABIKI KUSHANGILIA KWA STAILI MBALIMBALI
Ukweli ilikuwa ni siku ya matumaini na furaha kwani mashabiki kila mmoja alikuwa akishangilia kwa staili yake, wapo waliovua mashati na kubaki tumbo wazi huku wakicheza, wapo mashabiki wa kiume waliokuwa wanakata mauno kama wanawake na kuwa kivutio kikubwa uwanjani hapo.
Shilole 'akiangusha mauno'.
SHILOLE KUTAKA KUVUA NGUO
Hii ilikuwa ni hatari kwani mwanadada wa muziki wa mduara , Zuwena Mohamed ‘Shilole’ alifanya shoo ya nguvu lakini wakati anataka kufika mwisho akataka kuvua nguo kutokana na mzuka aliokuwa nao kwani alikuwa akiimba ‘nivue muone’ mashabiki nao wakawa wanaitikia ‘vua’, watu walipiga kelele za furaha kutokana na kufurahishwa na shoo ya mwanadada huyo.
Shabiki aliyejipenyeza uwanjani na kumganda mheshimiwa Mwigulu Nchemba kwa shangwe nyingi.
SHABIKI KUMGANDA MBUNGE
Ukiwa na mapenzi na kitu hutaona aibu! Baada ya wabunge kumaliza mechi shabiki mmoja alipenyeza uwanjani na kumganda mheshimiwa Mwigulu Nchemba huku akiwa amevua shati na alipokuwa akizunguka naye uwanjani alikuwa akifika sehemu anapiga magoti kwenye miguu ya mheshimiwa huyo na kunyoosha mikono juu na kuwa kivutio kwa watu waliokuwepo uwanjani hapo.
Yemi Alade akiulizia uwepo wa Johnnny kabla ya 'kupafomu'.
SHOO YA KIBA, YEMI FUNGA KAZI
Baada ya msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Kiba kufanya shoo ya nguvu alifuatiwa na mwanadada huyu kutoka Nigeria, Yemi Alade ambapo mashabiki walifurahia kwani walikuwa wamemsubiri kwa muda mrefu.
Alikiba akipafomu huku Steve Nyerere akisindikiza shoo kwa kiduku.
ALI KIBA KUBEBWA
Kutokana na kufanya shoo nzuri, Ali Kiba alijikuta katika mikono ya msanii wa muziki na filamu, Simon Mwapagata ‘Rado’ ambaye alimbeba na kumzungusha uwanjani hapo huku akiimba, ukweli ilikuwa noma sana!

MWIGULU, RIDHIWANI KIKWETE MZUKA 100%


Stori: Gladness Mallya
KWELI raha jipe mwenyewe! Usemi huo ulidhihirika wikiendi iliyopita ndani ya Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini (Night of Hope) ambapo wabunge mashabiki wa Yanga walikipiga na wabunge mashabiki wa Simba na kutia fora kwa kushangiliwa wakati wa mtanange huo.
Katika mchuano huo, wabunge wa Yanga waliwagaragaza wa Simba kwa mabao 3-2 hali iliyosababisha uwanja ulipuke kwa kelele za kushangilia kutoka kwa mashabiki na wapenzi halisi wa Yanga waliokuwepo  uwanjani hapo.
Mbunge za Chalinze kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete (kulia) akiwa uwanjani.
Kama vile hiyo haitoshi, baada ya kipyenga cha mwisho, wabunge wa Yanga walipanda mzuka na kuanza kuuzunguka uwanja wakisherehekea ushindi wao.
Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba akiwa na mshabiki wao mkubwa kwa upande wa Yanga.
Wabunge waliotia fora zaidi kwa kushangilia huku wakionesha hisia kali ni Mbunge za Chalinze kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete ambaye baada ya ushindi huo alikimbilia kwa mashabiki wa timu hiyo na kuvua jezi yake ya juu na kuwatupia, hali hiyo iliyomfanya kubaki tumbo wazi.
Ridhiwani Kikwete akirusha T-shirt yake kwa mashabiki wa timu yake.
Naye Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba alikuwa sanjari na Ridhiwani ambapo yeye aliwarushia mashabiki wake ‘skafu’ aliyokuwa amejifunga shingoni, hali ambayo ilimfanya shabiki mmoja kuchomoka alikokuwa na kumfuata mheshimiwa huyo uwanjani na kuungana naye kushangilia.
Wakati huo, shabiki huyo alikuwa amevua shati na kuonekana kutoamini macho yake kwani kila wakati alikuwa akipiga magoti na kumshika miguu mheshimiwa huyo.
Baadhi ya wabunge wa Simba waliochezea kichapo kutoka kwa wabunge wa Yanga.
Matukio ya wabunge hao yaliwafurahisha mashabiki waliokuwa uwanjani hapo na shangwe kuwa kubwa kupindukia.
“Jamani sijui niseme nini, najiona kama naota hivi kwa sababu nampenda sana Mwigulu na leo nimemuona na nimemshika na kushangilia naye.
Nina raha sana na sijutii kuja kwenye tamasha hili,” alisikika akisema shabiki huyo.
Mwanadada kutoka Nigeria, Yemi Alade alikonga nyoyo za mashabiki wake.
Hata hivyo, hali ilikuwa tofauti kwa wabunge wa Simba ambao baada ya kipigo hicho, walianza kulalamika kuwa wamehujumiwa na refarii wa mchezo huo, Othman Kazi.
  Kwa upande wa muziki, mwanadada kutoka Nigeria, Yemi Alade aliwakonga nyoyo mashabiki na baadaye akakiri kwamba alifikiri itakuwa ni shoo ndogo, kumbe ni kubwa kiasi hicho, akaeleza jinsi alivyofurahi na kutamani kualikwa tena Tanzania.

AUNT EZEKIEL: NITAHAKIKISHA NAMPA PENZI MUME WA MTU


Stori: Musa Mateja
Makubwa! Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson amefungukia madai ya kutoka na dansa wa Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ aitwaye Moze Iyobo ambaye ni mume wa mtu akisema hakuna ukweli wowote zaidi ya kutaka kuchafuliwa.
Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda wikiendi iliyopita, Aunt ambaye gazeti ndugu la hili, Risasi Mchanganyiko liliripoti tukio la kutaka kufanyiziwa na mke wa dansa huyo aitwaye Mwengi Ally, alisema anamshangaa mwanamke huyo lakini ili kumkomoa atahakikisha anafanya kweli ili kama ni kunuka, kinuke kihalali.
Alisema kwamba yeye ni mke wa mtu asiyeweza kujirahisi kwa kutembea na kijana huyo na kwamba kama ni kujuana ni kwa sababu ya Diamond ambaye ni shemeji yake kwa Wema.
“Amenichafulia sana, siwezi kutembea na Moze, najiheshimu. Lakini kwa kuwa ameamua kunipakazia, nitahakikisha namtega mumewe na nikimnasa nampa penzi ili kama ni hizo vurugu azifanye kihalali,” alisema Aunt na kusisitiza:
Dansa wa Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ aitwaye Moze Iyobo (kulia).
“Siwezi kuwa na uhusiano na Moze, yule mwanamke alikuwa na nia ya kuifanya jamii inifikirie vibaya lakini amenoa.” Hivi karibuni kundi la watu likiongozwa na  Mwengi lilifika nyumbani kwa Wema Sepetu likimsaka Aunt ili kumshikisha adabu kutokana na madai ya kutoka na mume wa mtu huyo.

JOKATE, DIAMOND WAONEANA AIBU!


Mayasa Mariwata
Kwa mara ya kwanza tangu walipomwagana, mastaa wawili Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wanadaiwa kuoneana aibu walipokutana laivu.
Mastaa wawili Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ pichani.
Akiwa na mtangazaji mwenzake, Edzen Jumanne, wikiendi iliyopita Jokate alidaiwa kushindwa kumbana Diamond kwa maswali wakati akimhoji kwenye kipindi kitakachoruka hewani hivi karibuni kupitia TV1.
Jokate  na ‘Diamond Platnumz’ wakipata ukodaki pamoja.
Baadaye Diamond alitupia mtandaoni picha akiwa na zilipendwa wake huyo hivyo kuibua mjadala mzito kuwa huenda bado wanapendana huku wenyewe wakipiga kimya.