Saturday, July 19, 2014

Azam, Mtibwa kunogesha Tamasha la Matumaini

Kikosi cha timu ya Azam, FC
Na Khadija Mngwai
TIMU za Azam FC na Mtibwa Sugar, zinatarajiwa kunogesha Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Agosti 8, mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa kushuka dimbani siku hiyo kuonyeshana ubabe.
Tamasha hilo litahusishwa na burudani kibao ikiwa ni pamoja na mechi za Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Simba na Yanga ambao wataonyeshana ubabe kwa kujua nani mkali.
Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar,
Mwaka jana, Rais Jakaya Mrisho Kikwete, alipuliza kipenga kuashiria mtanange huo kuanza kati ya wabunge ambapo safari hii wataonyeshana uwezo wa hali ya juu kufuatia kila upande kutaka kuibuka na ushindi.
Mechi hiyo ya Azam na Mtibwa itaanza mapema kabla ya mechi ya waheshimiwa. Mtanange wa timu hizo za ligi kuu, utachezwa kwa dakika 90 na kutoa fursa kwa timu hizo mbili kuonyesha vikosi vyao vipya kwa ajili ya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment