Sunday, February 16, 2014

Magazetini leo February 16 2014


.
.
Kila siku hapa millardayo.com huwa naweka magazeti ya siku husika, kuanzia udaku michezo na hardnews nikiamini kwamba wakati mwingine unaweza kuwa mbali na yanakopatikana au yakawa yanachelewa kukufikia asubuhi.
Lengo la millardayo.com ni kuhakikisha kila Mtanzania anaweza kusoma stori kubwa za Magazeti kabla ya saa mbili kamili asubuhi ambapo kwa mwaka 2014 lengo ni kuhakikisha Magazeti yanakuepo hapa millardayo.com hata kabla ya saa moja asubuhi.
Unaweza kujiunga na familia ya Millard Ayo kwenye facebook, twitter na instagram kwa jina la Millard Ayo ili kuwa karibu zaidi ya habari zote zinazowekwa hapa ambazo huwa link zinawekwa kwenye mitandao hii ya kijamii muda mfupi tu baada ya habari kupandishwa hapa.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Kwa wale walio-miss vitu vya Lil Wayne, hii ni habari nzuri kwenu.


weezyLil Wayne alikuwa na Drake kwenye show ambapo Drizzy ametoa taarifa nzuri kwenda kwa mashabiki wa Wayne.
Wakiwa katikati ya show hiyo Drake alitangaza ujio mpya wa album ya Lil Wayne ambayo itakuwa ni ya tano katika mfululizo wa album za Carter.
Tha Carter III ni moja ya album yenye mafanikio makubwa kwenye muziki wa Lil Wayne na Drake amesema May 5 itakuwa siku ya kutoa Tha Carter V.
“If you want to hear Lil Wayne at his best, if you wanna hear Young Money at they best..Carter V, May 5”, alisema Drake akiwa kwenye stage pamoja na Lil Wayne.

Ni kweli Lil Kim ni mjamzito, wengi walitaka kumjua baba… ndio huyu


kim2Baada ya taarifa za Lil Kim kuwa mjamzito swali lililobakia ni kujua nani ndio baba wa mtoto huyo atakayezaliwa mwaka huu?
Jibu ni kwamba rapper Mr. Papers ndio baba wa mtoto huyo ambaye ni wa kwanza kwa Lil Kim na wa pili kwa Mr. Papers kwasababu ana mtoto mmoja ambaye ana miaka 4.
Mr. Papers alisema Kim anategemea kujifungua kwenye mwezi wa tano au wa sita na ni mtoto wa kiume ambae bado hawajachagua jina la kumpa.
Inaaminika Lil Kim atatimiza miaka kati ya 39 au 40 July 11 mwaka huu.
mr-papers-lil-kimScreen Shot 2014-02-15 at 6.22.00 PM

Meno ya Tembo bado ni ishu, haya ni mengine yamekamatwa ya milioni 700.


1Stori za kukamatwa kwa meno ya tembo zimekua zikitoka kwa mfululizo nchini Tanzania ambapo kwenye post hii tunajiunga na Jeshi la Polisi 88.4 Mtwara ambalo lina taarifa za kukamatwa kwa watu wenye nyara za serikali alfajiri ya February 14 saa 11 katika kijiji cha Chungu kata ya Nanyumbu, tarafa ya Nanyumbu Mkoa wa Mtwara.
4Taarifa inasema kuwa watu hao walikamatwa na polisi wakiwa kwenye kizuizi cha barabara ya Mtambaswala-Mangaka ambapo waliokamatwa ni pamoja na Hamidu Abdallah Ngunde (40), Dereva wa gari Geraldat Lukas (36) na Boniphace Kosan (29) wote wakazi 88.5 Dar es salaam.
2Watuhumiwa hao walikua na jumla ya meno 58 yenye uzito wa jumla ya kilo 130.6 ambayo yana thamani ya shilingi Milioni mia saba za Kitanzania wakiwa wameyapakiza kwenye gari aina ya  Toyota Land cruiser T208 AGC.
Unaambiwa mbinu waliyoitumia jamaa ni kukata floor ya chini ya Gari na kutengeneza tank la bandia na kuweka meno hayo kisha kuweka kapeti juu yake chini ya kiti cha kukalia abiria wa nyuma ya dereva, Jeshi la polisi Mtwara linawashikilia watuhumiwa wote watatu.
Taarifa kutoka Jeshi la Polisi Mtwara.

Kuhusu kunusurika ajali Kala Jeremiah siku ya Valentine.

kala-ajaliLeo Kala Jeremiah kupitia ukurasa wake wa Instagram amepost picha inayoonyesha ajali aliyoipata wakati akitokea kwenye show yake iliyokuwa ikifanyika Club East 24 ambayo alikua akifanya show pamoja The B Band ya Banana Zoro.
kalaHiki ndicho alichokipost Kala Jeremiah kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Screenshot_2014-02-15-14-35-32Chini ya Post ya picha ya gari yake Kala aliandika maneno haya>>nIMEPATA AJALI USIKU HUU NIKIWA NATOKEA CLUB EAST 24 AMBAKO NILIKUWA NAFANYA SHOW NA B BAND WAKATI NARUDI NYUMBANI GHAFLA KUNA MTU WA PIKIPIKI AKAWA ANATAKA KUINGIA NIKAJARIBU KUMKWEPA GARI ILIKUA MWENDO KASI KIDOGO IKAYUMBA KWENDA KULIA NIKAIRUDISHA IKARUDI ZAIDI KUSHOTO NIKAIRUDISHA TENA KULIA IKAWA INATAKA KWENDA MTARONI NIKAIRUDISHA TENA KUSHOTO AMBAKO ILIGEUKA ILIKUKUA INATOKA NA KUINGIA MTARONI AMBAKO ILIKITA NA KUVUNJA MLANGO WA UPANDE WANGU.SIJAAMINI KAMA NIMETOKA BILA HATA JERAHA MGUUNI WALA MAUMIVU ZAIDI YA YALE UA KICHWANI KIDOGO NILIYOJIGONGEA KWENYE MLANGO KWA JUU.AHSANTE SANA MUNGU UMENIOKOA.ASANTE SANA MUNGU WANGU.

Saturday, February 1, 2014

Mambo sita usiyoyafahamu kuhusu wimbo wa Msambinungwa wa Tundaman.


msambiNi mara chache sana inatokea watu kuelewa maana ya misamiati kadhaa inayotumika sehemu tofauti mfano kwenye mashairi ya nyimbo,nahau au hata misemo kwa mfano mtu akikuuliza nini maana ya Msambinungwa unaweza kosa jibu la haraka haraka,tuitumie nafasi hii kumsikiliza Tunda Man akiuelezea wimbo huu alipoongea na millardayo.com.
Swali la kwanza lilikua ni kujua maana halisi ya Neno Msambinungwa,Tundaman alijibu Msambinungwa ni mtu Fulani hivi asiyeeleweka na hafai katika jamii yaani anaweza kuwa muongo,mtu mbaya mtu mwenye vitendo visivyofaa.
Swali la pili tulitaka kufahamu mpaka sasa wimbo wa Msambinungwa peke yake umemfikisha wapi kwenye hili Tundaman alijibu kwanza anamshukuru Mungu kwa mashabiki wake kwa kuipokea vizur huku akitoa mfano kuwa kuna siku moja hivi alikua anashuka kwenye gari anaenda kwa Maneck akawasikia watoto wanaimba walivyomuona wakaanza kupiga kelele.
Kuhusu jumla ya show alizofanya toka aachie wimbo wa Msambinungwa Tunda anadai amefanya show mbili tu kubwa ya kwanza ilikua ya bungeni na nyingine kwa President’Kikwete’ pale kwenye harusi ya Miraji iliyofanyika Mliman City.
Swali lingine lilikua linahitaji kujua Utofauti kati ya wimbo wa Msambinungwa na nyimbo zake zilizopita kwa hili Tunda alijibu>’Msambinungwa ni usemi ambao nimeuleta kwenye ulimwengu wa muziki maana siku hizi mtaani hata ukizingua kidogo tu unasikia watu wanakuita ‘We Msambinungwa’ usizingue so naona Msambinungwa nimefanya vitu vikubwa sana,ukisikiliza Msambinungwa utagundua’
Kingine ni kuhusu video ya Msambinungwa tunda alijibu>’Video ya Msambinungwa niliambiwa wimbo ni mkubwa so na video inabidi iwe kubwa kwa hiyo nilifikiria maana kuna kampuni niliilipa Kenya nikafikiria kufanya nao lakini nikahisi hawatoiweza wale wakenya nikaona video ya wimbo huu nifanye na Abbykazi,mpaka sasa nishashoot vipande kadhaa nimepanga mwezi wa pili kabla ya Valentine niizindue’
Kwa uchache ufahamu wimbo wa Msambinungwa ulivyokuwa>’Idea ya wimbo huu aliitoa mama yake mzazi na Tundaman na aliomba wimbo huo afanye na Marehemu Dr.Remmy Ongala bahati mbaya Dr.Remmy alifariki,baada ya hapo Tundaman alimtajia wasanii 5 wanaofanya vizuri ndipo mama yake akamwambia afanye na Ally Kiba.

Javier Hernandez Chicharito atakiwa na vilabu sita, lakini anabaki Man United


chicharito_0
Wakala wa mchezaji Javier Hernandez amethibitisha kwamba mshambuliaji huyo anaendelea kubakia Old Trafford pamoja na kutakiwa vilabu sita barani ulaya.
Chacharito, 24, amekuwa akihusishwa na suala la kuondoka Manchester United ili kuweza kupata timu atakayokuwa akicheza muda mwingi.
Wakala wake Eduardo Hernandez mapema leo alikaririwa na ESPN Deported akisema: “Nilikuwa na mikutano na vilabu kadhaa, siwezi kuvitaja vyenyewe wala ofa walizotoa, wanavutiwa mno na Chicharito. Moja timu kubwa kabisa iliyopo katika Top 10 ya timu bora duniani ilikuwa moja ya vilabu sita vinavyomtaka Javier.
“Kulikuwa na klabu kutoka Germany, moja kutoka France, mbili kutoka Spain na Italy, kila timu kati ya hizo inamtaka. Lakini, mteja wangu bado yupo kwenye mkataba na Man Utd na ataendelea kuuheshimu mkataba huo.”

Kuhusu kupigana kwa wachezaji wa Yanga Cannavaro na Niyonzima – Yanga wakanusha


17
Benchi la Ufundi la klabu ya Young Africans limesikitishwa na taarifa zilizoenea kwenye baadhi ya vyombo vya habari kwamba wachezaji wa Young Africans kiungo Haruna Niyonzima na nahodha Nadir Haroub “Cannavaro” walipigana katika mchezo dhidi ya Coastal Union siku ya jumatano jijini Tanga kuwa hazina ukweli wowote bali ni katika kutaka kuharibu taswira ya timu.
Akiongea na mtandao rasmi wa klabu www.youngafricans.co.tz , kocha msaidizi wa Young Africans Charles Boniface Mkwasa amesema wao benchi la ufundi wameshangazwa na taarifa hizo baada ya kuziona na kuzisoma leo na kusisitiza walioandika wamefanya hivyo kwa ajili ya maslahi yao tu.
Kila mtu alikuwepo uwanjani na aliweza kushuhudia mchezo huo, hakuna aliyeona Cannavaro na Niyonzima wakipigana katika kipindi chote cha dakika 90 za mchezo, nashikwa wasi wasi na waandishi waliokuwepo uwanjani kama walikua makini kufuatilia mchezo na kuandika kitu tofauti na walichokiona.
“Sheria za soka zipo wazi, mchezaji au wachezaji wapigana ndani ya uwanja mwamuzi anawatoa nje ya uwanja kwa kuwapa kadi nyekundu, sasa tumeshangazwa na taarifa hizo zilioripotiwa leo kuwa kuwa kuna wachezaji wetu walipigana ili wachezaji wote walicheza kwa dakika 90 “alisema Mkwasa.
Nadhani imefika wakati tuisaidie jamii kuelewa uhalisia wa jambo husika liliotokea, kwani kuandika tofauti na kilichotokea kunasababisha jamii kuamini/kuelewa jambo ambalo silo lililotokea.
Katika mchezo wowote wachezaji kuelekezana/kukumbushana majukumu ni jambo la kawaida na ndicho kilichotokea katika mchezo dhidi ya Coastal kati ya Cananavaro na Yondani na Niyonzima na Cannavaro na si kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
“Hata mara baada ya mchezo wachezaji wote walikuwa pamoja na kupeana pole kutokana na ugumu wa mechi, kisha wote kuondoka kuelekea hotelini kupumzika, na sisi kama viongozi hatujaona wachezaji kutofautiana kitu chochote hata kufikia hatua ya kusuruhishwa kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari “aliongeza Mkwasa .
Kuhusu maandalizi ya mchezo wa jumapili Mkwasa amesema vijana wake leo wamefanya mazoezi asubuhi kujiandaa na mchezo huo, na hakuna mchezaji majeruhi hata mmoja kwani Hamis Kiiza, Hassana Dilunga waliokuwa wagonjwa wameshaungana wenzao kambini na Athuman Idd “Chuji”  aliyekua amesimamishwa kurejeshwa kundini.

Unataka kujua alichosema Okwi kuhusu Sakata lake lililopo sasa hivi,kipo hapa.



okwi9Baada ya headline mbalimbali zilizokuwa zikimhusisha Kiungo mshambuliaji wa timu ya Yanga Emmanuel Okwi hatimae amezungumza kuhusu taarifa hizo ambapo amesema hataki kuzisikia wala kuzungumzia habari za Simba na Etoile du Sahel kwa kuwa hana mpango wa kurejea alikotoka.
okwi8
Emanuel Okwi ametoa tamko hilo ikiwa ni siku chache mara baada ya kusimamishwa kwa muda,huku uongozi wa Yanga ukisisitiza kuwa utamtumia mchezaji huyo katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Komorozine ya Comoro inayotarajiwa kuchezwa wiki ijayo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Okwi ambaye ni raia wa Uganda amesema yeye ni mchezaji wa Yanga na mapenzi yake yapo klabu hiyo ndiyo maana hataki kuzungumzia suala la mgogoro wa usajili wake, kwa kuwa hana mpango wa kurudi alipotoka.
Okwi alianza kwa kusema>>’Najua baada ya muda TFF itaniruhusu kucheza,sitaki kurudi nilipotoka kwa kulizungumzia suala la Etoile (du Sahel), pia sitaki kuizungumzia Simba kwa kuwa siyo klabu yangu’
‘Naipenda Yanga na mapenzi yangu yote yapo hapa, ndiyo maana leo hii nipo klabuni nikiwa mchezaji wao. Nilikuwa tayari kuanza kuichezea Yanga katika ligi hii (mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara) na Ligi ya Mabingwa Afrika’.
Kuhusu suala la sakata la kuzuiliwa kucheza Okwi,Katibu Mkuu wa Yanga Beno Njovu amesema kuwa watamtumia Okwi katika mechi dhidi ya Komorozine kwa kuwa wamepata ruhusa ya kumtumia kutoka Shirikisho la Soka la Afrika (Caf).

MZEE GURUMO AFUNGUKIA SKENDO ZA DIAMOND

Mayasa Mariwata na Shani Ramadhan
MSANII mkongwe wa muziki wa dansi Bongo, Muhidini Gurumo ambaye kwa sasa amestaafu, amefungukia skendo ya kuwa na mademu wengi inayomuandama Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni maeneo ya Ilala jijini Dar, Mzee Gurumo alisema: “Diamond ana nidhamu sana ila vile anavyotamba jukwaani na kudatisha mashabiki hapo ndipo balaa linapokuja, watoto wa kike wenyewe wanaanza kujisogeza kwake.
Mzee Muhidini Gurumo.
“Pamoja na skendo za mademu zinazomuandama, siwezi kumshusha thamani, ana haki ya kujiopolea mwanamke yeyote anayempenda, yeye kama mwanaume rijali wakati mwingine ni vigumu kujizuia na vishawishi hivyo.”

USALITI HAUNA NGUVU, SHETANI WA USALITI NI AKILI ILIYOKOSA MALENGO-10

Tunaendelea na mada yetu ambayo tumeianza wiki kadhaa zilizopita, inahusu fundisho la usaliti. Endelea...
Sikumtaka mume wangu wala Paul, wote niliwaona wana matatizo, yaani hawajakamilika. Saa 4 usiku ndiyo nilikwenda kulala.
“Niliamka saa 3 asubuhi, muda huo mume wangu alikuwa ameshakwenda kazini. Mtoto wangu mkubwa naye alishakwenda shuleni, maana huondoka asubuhi pamoja na baba take. Nilikwenda chumba cha watoto na kumkuta mtoto wangu akiwa bado kalala, kama kuhakikisha nilikwenda chumbani kwa Paul nikamkuta amekaa kitandani kwake anasoma kitabu cha mapenzi.
“Baada ya salamu, nilimuuliza sababu ya kutokwenda kazini mpaka muda huo, akanijibu alikuwa ananisubiri mimi niamke. Aliniambia asingeweza kufanya kazi zake ipasavyo kama hatatimiza lengo la kucheza ‘kikwetukwetu’ faragha na mimi. Nilicheka, kisha nikamuuliza kama anaweza.
“Akaniambia anaweza. Kusema ule ukweli pale nilikuwa nimeshamuona Paul kama mgonjwa asiye na jeuri yoyote kitandani. Nilicheka kama kumsanifu halafu nikaenda bafuni kuoga. Nilimuamsha mtoto wangu, nikamuogesha halafu nikampa chai anywe, alipomaliza kunywa chai nilimpeleka kwa mama mdogo.
“Nilirudi nyumbani nikiwa najiuliza mengi lakini kubwa ni kama Paul ataweza. Nilijua ni mbovu tu, anayetaka kunichezea lakini nilimpa nafasi ya mwisho, ndiyo maana nilihakikisha pale nyumbani tunakuwa wawili tu ili akishindwa asiwe na kisingizio kingine.
“Nilipofika nyumbani nilifunga mlango mkubwa, nikaenda moja kwa moja chumbani kwa Paul. Nilimkuta amelala anasoma kitabu, nilikaa jirani yake, nilimwambia awe na uhakika kama ataweza, siyo nasaula halafu hakitokei chochote.
“Kweli ni aibu, maana mimi kwa umri namzidi Paul miaka sita, ukichangia na umbile langu, halafu nisaule nguo zote naye anione kama nilivyozaliwa nikiwa na matarajio ya kupata penzi ambalo silipati, ni aibu iliyoje? Paul alionekana kujiamini sana, akanihakikishia kwamba hataniangusha.
“Paul aliachana na kitabu chake, akanifuata pale nilipokaa. Nilikuwa nimevaa kanga na blauzi, kwa ndani ni kufuli kama kawaida, juu ni ‘brazia’. Alinitoa kanga nilimkubalia, vilevile kabati langu aliliondoa, alipotaka kuhusika na blauzi nilimgomea, nilimwambia ingewezekana vilevile.
“Kiukweli nilikuwa simuamini ndiyo maana sikutaka aguse blauzi yangu. Siku hiyo sikuwa mfuatiliaji sana kwa sababu nilihofia kwamba atashindwa. Mwanzoni kama alihangaika, yaani gari lake lilianza kuleta mgogoro kwenye kuwaka lakini baadaye stata ilikubali, mambo yakawa safi kabisa.
“Ni dereva mzuri, anaendesha vizuri gari lake, nilimkubali. Nilimuuliza mbona usiku alishindwa, akanijibu hata yeye anashangaa. Ubora wake anaposhika usukani, ndiyo uliofanya nisichoshwe naye, ilipoisha safari moja, iliendelea nyingine. Paul alinifikisha nilipotaka, alinikata kiu yote.
“Kuanzia siku hiyo nilichanganyikiwa kabisa kwa Paul. Nikawa namdharau mume wangu, kwani hata alipotaka huduma chumbani sikumpa. Mume wangu aliposafiri nililala na Paul. Hatukujali matumizi ya kinga wala kujali mzunguko wa siku, basi ikawa napata mimba natoa.
“Penzi la Paul lilinitia wazimu, kila alichoniambia nilikisikiliza bila kuhoji. Neno lake likawa sheria. Tukadanganyana tutaoana, nami nikavimba kichwa. Mgogoro na mume wangu ukawa mkubwa, kila siku vikao kwa wazazi, nikawa nasisitiza nipewe talaka.
“Nilipoona anakuwa mgumu kunipa talaka, ikabidi nimwambie kwamba nina uhusiano na Paul, nilifanya vile achukie anipe talaka yangu. Kumbe nikawa nimechokoza moto, ulitokea ugomvi mkubwa kati ya mume wangu na Paul, waligombana mpaka kufikishana polisi.
“Huwezi kuamini, pamoja na ugomvi huo lakini hatukuacha. Mimi na Paul tuliendelea na mapenzi yetu. Hata nilipogombana na mume wangu, nami kurudi kwetu, niliwasiliana na Paul akiwa nyumbani, nami nilikwenda, tukajifungia chumbani kwake na kufanya ya kwetu. Tulipomaliza nilirudi kwetu, yaani kwa mama mdogo.
“Baada ya wazazi kuona mgogoro ni mkubwa ndani ya ndoa, huku ikiwa wazi kwamba tatizo ni Paul, waliamua kunisafirisha kwenda kwa shangazi yangu Dodoma ili nikae huko, angalau niwe mbali na Paul. Hiyo safari ndiyo iliyonisaidia kujitambua.
“Nikiwa Dodoma, kwanza hisia zangu kwa Paul zikapungua, halafu nikaja kusikia sifa zake za kubadili wanawake kama nguo, halafu analala nao chumbani kwake, niliona amenidhalilisha sana. Nikaanza kukumbuka mazuri ya mume wangu, nikajuta kwa kila kitu.
“Uzuri ni kuwa mume wangu hakunipa talaka, kwa hiyo nilimuomba msamaha. Tulimaliza mgogoro wetu, tulihama ile nyumba ili kuwa mbali na Paul. Kwa hiyo kumbukumbu kuhusu Paul ikawa historia tu. Itaendelea wiki ijayo.
Sioni nguvu kubwa iliyonituma kusaliti ndoa yangu, isipokuwa yale mazoea na ukaribu ndiye Shetani wa usaliti.
“Kilichonifanya nijione siwezi kuishi bila Paul hayakuwa mapenzi makubwa, isipokuwa ni yale mazoea. Nawaasa wanawake wenzangu waheshimu ndoa zao, maana kama mume wangu angekuwa siyo mvumilivu, leo ningekuwa sina ndoa.”
HITIMISHO
Siku zote, uaminifu ni nguzo. Mtu mwenye malengo yake hawezi kuteleza kwa kiwango kikubwa mpaka kutoka nje ya ndoa. Shikilia hapo ulipo, vishawishi vya hapa na pale visikuyumbishe.
Lauryn ametufundisha kwa mfano. Jambo lenye faida kwako ni kutambua thamani ya mwenzi wako kisha umlinde kwa hali yoyote ile. Kumsaliti ni kumaanisha hujitambui, hujielewi, akili yako haina malengo.
Mantiki ni kuwa unaposaliti, maana yake unaliweka rehani penzi lako. Mtu mwenye malengo hawezi kufanya hivyo. Nikutakie kila la heri katika maisha yako ya sasa na yajayo. Daima penzi lenu liwe imara.

SIRI 7 ZA KUVUNJA NDOA NA MBUNGE MZEE!

Stori: Imelda Mtema na Ojuku Abraham
YULE ‘hendsam’boi’ Michael Christian (28) ambaye mwaka jana aliitikisa medani ya siasa Bongo kufuatia kufunga ndoa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Rukwa, Rose-Sweeter Kasikila (60) na miezi michache mbele ndoa ikavunjika, ameibuka na kuanika siri 7 zilizomfanya aamue kuivunja ndoa hiyo na mheshimiwa huyo.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Rukwa, Rose-Sweeter Kasikila.
Akizungumza na gazeti hili jijini Dar, juzi, Michael alibainisha mambo hayo huku akisema anajuta kwa tukio lile ambalo bado halijamtoka kichwani hadi sasa.
Michael Christian‘hendsam’boi’ aliyevunja ndoa na ndoa hiyo na mheshimiwa huyo ndani ya Ofisi za Global.
SIRI YA KWANZA
Kijana Michael aliianika siri ya kwanza kwamba ni kuchekwa na marafiki zake wa Bagamoyo mara baada ya kugundua amefunga ndoa na mbunge huyo ‘mzee’.
“Marafiki zangu walianza kunicheka, walisema nimefunga ndoa na mbunge mzee, mama mtu mzima. Nikaanza kujisikia vibaya jambo ambalo sikulipenda hata kidogo,” alisema kijana huyo ambaye ni yatima.

SIRI YA PILI
Akizungumza kwa hisia kali, Michael aliye na taaluma ya uuguzi, aliiweka wazi siri ya pili ya kuamua kuivunja ndoa yake na mheshimiwa huyo kuwa ni kitendo cha kutokuwepo kwa tangazo la ndoa la siku 21 kama sheria ya nchi inavyotaka.
Kuna kifungu cha sheria kinachotaka wachumba wanapotaka kufunga ndoa kutolewa tangazo la siku 21 kwenye mamlaka za kufungisha ndoa hiyo ili kama mmoja wa wahusika ana ndoa inayoishi (halali) aweze kuwekewa pingamizi la kufungishwa ndoa.
SIRI YA TATU
Kijana huyo aliendelea kwa kuifunua siri ya tatu kuwa ni kitendo cha kufungishwa ndoa bila kuwepo na mashahidi wa pande zote mbili (matroni na patroni) walioandaliwa zaidi ya kuitwa papohapo.
Alimtaja kwa jina moja Mchungaji Mtetumo wa Kanisa la Mikocheni ‘B’ Assemblies of God ‘Mlima wa Moto’ kuwa ndiye aliyesimamia kufungwa kwa ndoa hiyo, Septemba Mosi, 2011 ndani ya ofisi huku milango ikiwa imefungwa.
Alisema pia kwamba, suala la ndoa aliligundua siku hiyohiyo baada ya kufika kwenye kanisa hilo ambapo maandalizi mengine yote yalishafanyika akiwa hajui.

SIRI YA NNE
Siri zilizidi kubanjuliwa, Michael alisema sababu ya nne ambayo pia ilimsukuma kuamua kubatilisha ndoa yake na mama Kasikila ni baada ya kubaini kwamba, hataweza kupata uzao kwa mke huyo kwa sababu ana watoto wakubwa kiumri kuliko yeye.
“Nilijua sitapata watoto, hakukubali kuzaa na mimi kwa sababu tayari ana watoto wakubwa, mimi mdogo, ingekuwa vigumu. Kifupi haikuwa ndoa halali kwangu,” alisema kijana huyo.

SIRI YA TANO
Michael: “Alianza kunibana sana, kila hatua ya miguu yangu alitaka kujua inakwenda mpaka wapi! Hii hali nikaiona inanipiga pingu, nikagundua kuwa kumbe mimi sijaoa, bali nimeolewa. Yule mama alinioa mimi, si kwamba mimi nilimuoa yeye, nikasema ili niwe na amani ya moyo ni lazima ndoa ivunjike.”
SIRI YA SITA
Kijana huyo hakuona sababu ya kubakiza siri hata moja, akaendelea kuzianika:
“Jambo jingine ambalo pia lilichangia kuamua kuivunja ndoa ile ni baada ya kukumbuka historia ya kukutana kwetu.
“Wakati nipo Hospitali ya Bagamoyo na yeye akiwa pale kama muuguzi mkuu, tulizoeana. Kuna siku aliniita kwake akasema anasafiri anaomba nimwangalizie nyumba, nilikuwa na rafiki yangu tukawa tunalala pale mpaka aliporudi.
“Kuzoeana kuliendelea, mwishowe tukawa wapenzi mpaka ndoa. Nilipokumbuka hivyo tu nikagundua kuwa aliniingiza mapenzini kwa hila au mbinu, hilo pia sikulipenda,” alisema Michael. 

SIRI YA SABA
Michael alisema sababu ya saba ambayo pia ilimshinikiza kuivunja ndoa hiyo ni kupwaya ndani ya nyumba.
Alisema kutokana na umri wake, ndani ya nyumba alijiona ni mtoto na si mume kama wanaume wengine walivyo.
“Hata uwezo wangu wa mawazo kwake haukuwa wa mume na mke, ni wa mtoto na mama. Kifupi haikuwa ndoa halali,” alisema.

SIKU ALIPOIVUNJA NDOA
Kijana huyo alisema ndoa yake na mheshimiwa huyo aliivunja mbele ya Mchungaji wa Kanisa la Mikocheni ‘B’ Assemblies of God, Dk. Getrude Rwakatare walipokwenda kusuluhishwa ili waende wakaishi kwa amani.
Alisema kabla ya usuluhishi alimfungukia mama Rwakatare kuhusu manyanyaso anayoyapata ndani ya ndoa hiyo ndipo aliposimama na kuivua pete kisha kuitupa chini huku akisema katu hawezi kurudi kwa mkewe huyo na ndoa imevunjika, akaondoka zake.

ANATAKA KILIO CHAKE KIFIKE KWA JK
Kijana Michael alisema kilio chake kikubwa kwa sasa ambacho angependa kifike hadi kwa Rais Jakaya Kikwete ni kitendo cha mkewe huyo kuzuia vyeti vyake ambavyo vingemsaidia kutafutia kazi sehemu mbalimbali.
“Amezuia vyeti vyangu vyote, kila nikimwambia navitaka nikienda ananifanyia visa, nawaomba Watanzania wanisaidie kwa hili.
“Mimi kwa sasa nataka vyeti tu, sitaki cha ndoa wala nini? Lakini hataki kunipa,” alisema Michael.

MSIKIE MBUNGE SASA
Akijibu tuhuma hizo, Mheshimiwa Kasikila alikiri kuwa na vyeti vinavyolalamikiwa na mumewe huyo, lakini alikanusha kwa nguvu zote juu ya maneno kuwa yeye ameoana na mtoto mdogo, akirejea vifungu vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, vinavyomtaja mtoto kama ni mtu wa namna gani.
Mbunge: “Mwandishi, unafahamu mtoto kwa katiba yetu ni mtu wa namna gani?”
Mwandishi: “Ni mwenye umri wa chini ya miaka kumi na nane.”
Mbunge: “Sasa Michael ni mtoto? Ana miaka 28 unamuita mtoto?”
AWAWEWESEKEA WANASIASA
Alisema anajua suala hilo lina shinikizo la kisiasa, kwani hivi karibuni baadhi ya wanasiasa walikwenda jimboni kwake wakiwa na nakala ya gazeti moja lililoandika habari zake na kijana huyo na kuwaambia wapigakura wake kuwa mbunge wao ameoa kitoto, lakini wapigakura wake waliwapuuza kwa kuwaambia hilo haliwahusu kwani wanachojua anawawakilisha vizuri bungeni.
“Kama kweli ninyi mnampenda huyo Michael, muelekezeni sehemu sahihi ya kwenda kupeleka madai yake. Ngoja nikupe mfano, mimi nikiwa wizara ya afya, mtu akija na malalamiko kuhusu pembejeo za kilimo, kwa kumsaidia, nitamuelekeza aende wizara ya kilimo, kwa kuwa pale (afya) siyo sehemu yake, sasa nyinyi muelekezeni huyo sehemu sahihi ya kupata haki yake, siyo huko magazetini,” alisema mama huyo.

MAMA RWAKATARE BWANA
Kwa upande wake, Mchungaji Rwakatare alipopigiwa simu kwa lengo la kumsikia chochote kuhusu ishu hiyo, alianza kulalamikia habari iliyoandikwa miezi miwili nyuma na kukata simu.  

ROMANI KATOLIKI WAWASHUKIA BONGO MOVIE

Stori: Jelard Lucas
KANISA la Romani Katoliki limeishukia tasnia ya filamu Bongo (Bongo Movies) kutokana na matendo maovu yanayofanywa na wasanii katika sinema zao hususan suala zima la kuheshimu imani za watu.
Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza, Thadeus Ruwa’ichi.
Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza, Thadeus Ruwa’ichi amewaonya wasanii kuwa maigizo yao yasilenge kuchafua umma ama kikundi chochote kwani wanaweza kuleta mgawanyiko katika taifa.
Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Akizungumzia msimamo wa kanisa kuhusiana na filamu ya Sister Maria ya mwigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’ ambayo kanisa hilo liliipinga kutokana na madai ya kukiuka maadili, Askofu Ruwa’ichi alisema hawakubalini nayo kwani mavazi ya masista yaliyotumiwa na wasanii hao, yalitumika vibaya hivyo hawakubaliani nayo.
Cover la filamu hiyo ya Sister Marry.
Akifafanua zaidi kuhusiana na filamu hiyo, kiongozi huyo wa kiroho alisema alisononeshwa na kazi hiyo ambayo ilikuwa na dosari za kuingilia imani ya kikatoliki kwani mavazi ya kanisa yalitumika kuvaliwa bila staha.
“Ile filamu ilikuwa na lengo la kuhatarisha jamii, kamwe isiendelee kwani ni hatari kwa watu ama mtu binafsi anayechukizwa na tatizo hilo,
“Maigizo yanayofanywa yanaweza kuwa na lengo la kutumbuiza, lakini kutumbuiza kokote kule, hakupaswi kuhatarisha lengo la kulea ama kuvuruga mambo ya watu fulani, kulinda heshima ya watu binafsi ama taasisi, nidhamu inahitajika kwa kila jambo wanalolifanya,” alisema.
Baadhi ya vipande vilivyomo katika filamu hiyo.
Askofu huyo alisema taifa lina mambo mengi na linajivunia kwa amani ya muda mrefu, hivyo waigizaji hao wanapoigiza maigizo ambayo yanagusa imani au jamii ya watu wengine linaweza kuwa tatizo kubwa huko mbele.
“Hakuna haja ya maigizo kuchafua watu wengine, heshima kwa wote ni jambo jema ambalo linaweza kuongeza upendo kwa kila jambo ufanyalo kwa jamii nyingine.
“Wakifanya kazi zao kwa ufasaha bado taifa litawaheshimu, hakuna mtu ama kundi ambao wangependelea kutokee vurugu eti kwa sababu ya maigizo ya mtu fulani, haiwezi kuungwa mkono,” alisema askofu huyo.

PENNY; CHAGUA BEGA, CHAPA ILALE!

Stori: Anko Nangale
LEO nabonga naye mwanadashosti anayeuza nyago kwenye kichupa cha DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Nianze kwa kukupa gwala kiroho safi. Juzikati umefunguka kuwa umepiga chini kiaina malovee na Diamond, mzuka mwingi. Umetisha sana.
Mtangazaji wa DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Unajua laifu la malavidavi ndivyo lilivyo siku hizi. Mizinguo inakuwa mingi na wengi huwa wanatambua kuna taimu inafika unalazimika kupiga chini ili michongo mingine iendelee.
Nikiwa katika mingo zangu za kusaka chambi, nilipata bahati ya kuchonga na masela f’lani hivi ambao walikuwa wakizimikia penzi lenu, walipenda kuliona linakimbiza kitaa deile lakini wakasema umechagua bega sahihi, kubwaga manyanga kwa pisi.
“Ni uamuzi mzuri sababu mchizi akiwa hasomeki huna haja kufosi kingi wakati unaona hivihivi chombo kishaenda mrama, halafu mbona mtoto mwenyewe full mauzo, shepu anayo na ameumbika kinoma?” alifunguka mwana mmko.
Kwa wale ambao hatuko pamoko, msiogope. Ishu ilikuwa hivi, mapema wiki hii Penny alibonga na midia na akafunguka kuwa hamchukii ex wake huyo lakini wameamua kupeana spesi kiaina ili kila mmko wao aweze kufanya yake bila kupeana bugdha.
Penzi lao lilikuwa na tensheni ya kufa mtu, mingo zao za kimahaba zilikuwa zinasanuka kila kukicha. Baadhi ya wana walikuwa hawazimiki na skendo zako, ziliwaboa kinoma lakini hawakuwa na sehemu ya kufikisha meseji zao, waliamua kupiga kimya kimtindo.
Kwenye midia ulifunguka kuwa kama ikitokea umepata doni mpya, hutamaindi awe mtu maarufu, hicho ndicho wana wengi walichokitolea saluti. Wameona mafahari wawili hamuwezi kuishi kwenye zizi moko.
Kabla sijamaliza, nikupe salamu za watoto wa kishua kule kipande cha Oysterbay, Masaki na Mikocheni. Nao walizimika sana na yai lako, walipenda unavyodondosha ung’eng’e katika mahojiano yako ya mtandaoni.
Kimsingi ulienda nao sawa, walikuelewa kinoma. Ulipokuwa ukitema yai, wengi walikuwa wakiwatonya matha zao, si unajua zile za; “dadi, yu noo, shi izi andastendi…!” walifunguka kwa matha zao.
Walizimikia msimamo wako na kutamani wakupe tano hata la mbali.
Siyo kesi, chapa ilale umeshachagua bega. Spesi mmepeana, kamata kiburudisho kipya na muvi jipya liendelee.

MUUNGANO WA UTEPE MWEUPE WAKUTANA WAZIRI MKUU PINDA, KUJADILI NAMNA YA KUPUNGUZA VIFO VYA WAJAWAZITO

Wajumbe wa Mkutano kati ya Utepe Mweupe na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo Ikulu.
Mkutano wa Waziri Mkuu na wajumbe kutoka Muungano wa Utepe Mweupe ukiendelea. Mkutano wa Waziri Mkuu na wajumbe kutoka Muungano wa Utepe Mweupe ukiendelea.
David Lyamuya kutoka Muungano wa Utepe Mweupe akimvisha utepe Mweupe Waziri Mkuu, Pinda.
*Ni kujadili namna ya kupunguza vifo vya wajawazito

FORBES MAGAZINE REVEALS MO AND MAKAMBA JR AMONG 10 POWERFUL MEN IN AFRICA 2014‏

Mohammed Dewji, Tanzania, Group Chief Executive Officer of Mohammed Enterprises Tanzania Limited
Dewji is the Group Chief Executive Officer of Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL) and at 39 is the youngest member of the Forbes’ Africa’s 50 Richest list with an estimated net worth of USD $500 million.
The MeTL Group began as a family business, a small trading company which Mohammed transformed into one of the largest industrial conglomerates in East Africa, with interests ranging from real estate, agriculture, finance, distribution and manufacturing.
The company employs more than 24,000 people across Tanzania and according to Dewji, generates annual revenues of USD$1.3 billion.
Dewji has been a Member of Parliament in the National Assembly of Tanzania since 2005. Dewji graduated from Georgetown University with a degree in International Business and Finance with a minor in Theology.
January-Makamba1
January Makamba Tanzania, Deputy Minister of Communication, Science & Technology.
January Makamba Tanzania, Deputy Minister of Communication, Science & Technology and Member of ParliamentMakamba is one of Tanzania‘s rising stars in government. He is currently the Deputy Minister of Communication, Science and Technology and is rumored to run for President in 2015.
Makamba is a Member of Parliament for Bumbuli constituency in the National Assembly of Tanzania. Before running for the Bumbuli parliamentary seat, Makamba was aide to Tanzanian President Jakaya Kikwete for 5 years.
Named Young Global Leader class of 2012 by the World Economic Forum, Makamba comes from a political family; his father, Yusuf Makamba was Secretary General of the ruling CCM party under Julius Nyerere.

Wednesday, January 22, 2014

B ENKI KUU YA TANZANIA YATOA SARAFU YA SH 50,000....ANGALIA HAPA



Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa sarafu maalumu ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye thamani ya sh 50,000.
Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, alisema jana kuwa sarafu hiyo iliyotengenezwa kwa madini ya fedha kwa asilimia 92.50, imetolewa kwa ajili ya kumbukumbu tu na haitaingizwa katika mzunguko wala kutumika kwa kulipia malipo ya aina yoyote.


Sarafu hii imetolewa maalumu kama maadhimisho ya miaka 50 ya mapinduzi ya Zanzibar, haitatumika kwa manunuzi.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki ya BoT ilimnukuu Profesa Ndulu akisema sarafu hiyo imetolewa kwa idadi ya vipande 3,000 kwa ajili ya tukio hilo na kuwahimiza wananchi kuinunua kwa ajili ya kumbukumbu hiyo.

Kwa mujibu wa Gavana, kutolewa kwa sarafu hiyo kunakwenda sambamba na utaratibu wa Benki Kuu kutoa sarafu maalumu za aina hiyo kama sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya matukio mbalimbali muhimu ya kitaifa na kimataifa.

Kwa kawaida, baada ya muda, thamani ya sarafu kama hizi huongezeka na kuwa na faida zaidi kwa wanaozimiliki,” alisema Profesa Ndulu.
Gavana Ndulu alieleza sarafu hizo zitapatikana Januari 5 kwa bei ya sh 50,000 katika matawi ya benki za biashara zitakazokuwa zimepata sarafu hizo kutoka Makao Makuu ya Benki Kuu, Dar es Salaam na matawi ya Benki Kuu yaliyoko Zanzibar, Arusha, Mbeya na Mwanza.
Benki za biashara zinaweza pia zikasambaza sarafu hizi kupitia matawi yake,” alisema gavana na kuongeza taarifa za usambazaji zitatolewa na benki hizo.
Katika sarafu hiyo, upande wa mbele unaonyesha sura ya hayati Sheikh Abeid Aman Karume na maandishi yanayosomeka: ‘Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi’. 
Upande mwingine wa sarafu unaonyesha nembo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, maandishi yanayosomeka: “Miaka Hamsini ya Mapinduzi”, thamani ya sarafu na miaka 1964-2014.
-Tanzania daima