Monday, September 2, 2013

MTANDAO WA UNGA WANASWA

Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akionesha picha ya kijana Leonard Jeremiah Monyo aliyekamatwa na kete 86 za madawa ya kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Stori: Makongoro Oging’ na Haruni Sanchawa
MTANDAO hatari wa unga nchini Tanzania umeshanaswa, kwa sasa unafanyiwa kazi kwa kasi na Kitengo cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya, chini ya kamanda wake, Godfrey Nzowa.
Habari njema kuhusu kunaswa kwa mtandao wa unga, zinakuja baada ya Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe kufanya kazi nzuri na kuwataja watu ambao inadaiwa walihusika katika kupitisha madawa ya kulevya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam.
Madawa ya kulevya.
Sekeseke kuu ni kukamatwa kwa Watanzania wawili, Agnes Gerald ‘Masogange’ ambaye ni mwanamitindo na Melisa Edward, nchini Afrika Kusini, wakiwa na madawa ya kulevya aina ya Crystal Methamphetamine, yenye uzito wa kg 120, Julai 5, mwaka huu.
Swali kwamba walipitaje JNIA lilijibiwa na Mwakyembe Jumamosi iliyopita, akafafanua namna Mfumo wa Kamera za Usalama (CCTV), zilivyonasa ‘uhuni’ uliofanyika, hivyo akawataja watumishi wa Mamlaka ya Uwanja wa Ndege (TAA), Yusuf Daniel Issa, Jackson Manyonyi, Juliana Thadei na Mohamed Kalungwana kuhusika, akaagiza wafukuzwe kazi na polisi kuwakamata.
Baada ya Mwakyembe, moto unaendelea kuwaka na uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa mtandao ulionaswa na Kitengo cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya, unagusa mikoa yote nchini.
Agnes Gerald ‘Masogange’.
Katika mtandao huo, siri kubwa iliyovuja ni majina na jinsi biashara hiyo haramu inavyoendeshwa mkoa kwa mkoa, wilayani mpaka mitaani, vilevile wanamichezo na wasanii mbalimbali ambao imeshabainika kwamba wengi wao wanatumika kusafirisha unga.
Imebainika kwamba mtandao huo, uligundulika baada ya watu 2,075 kukamatwa katika kipindi cha Januari hadi Juni mwaka huu (baadhi yao, picha zao zinaonekana ukurasa wa mbele).
“Watu tuliowakamata kimsingi ni wale wanaotumwa tu. Sasa wale ndiyo wamewataja mabosi wao, wameeleza siri kubwa,” alisema Kamanda Nzowa na kuongeza:
Baadhi ya watuhumiwa wa dawa za kulevya.
“Haikuwa kazi rahisi, tulitumia mbinu za kiaskari kuwafanya waeleze ukweli. Wamesimulia biashara hiyo inavyofanyika, jinsi watu wenye fedha wanavyowatumia vijana kusafirisha mizigo.
“Tulichobakiza sasa ni kuwakamata wahusika na kuusambaratisha mtandao wenyewe. Hata sasa tunachokifanya ni kupambana na huo mtandao wenyewe, mwisho tutausambaratisha kabisa.”
NI MWAKA WA VITA NZITO
Nzowa, alisema kuwa mwaka huu umeonekana kuwa na vita nzito kwa sababu kuna lindi kubwa la watu ambao wamejiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya licha ya wengi kukamatwa na hata baadhi yao kunyongwa katika nchi za China na Pakistan.
Alisema madawa ya kulevya yenye uzito wa kilo 16,824 (tani 16.8) yamekamatwa kati ya kipindi cha Januari na Juni, mwaka huu, idadi ambayo ni kubwa kuliko vipindi vyote vilivyopita.
Melisa Edward
Alifafanua kwamba wingi huo usitafsiriwe tu kwamba biashara ya madawa ya kulevya inatanuka nchini, isipokuwa itazamwe kwa jicho la pili kwa upana wake jinsi mapambano dhidi ya biashara hiyo yalivyochochewa makali.
“Udhibiti umekuwa mkubwa sana. Isichukuliwe tu kwamba biashara inazidi kushika kasi, hapana, haya ni matunda ya kazi ya udhibiti ambayo inafanyika. Pengine huko nyuma walikuwa wanapishana kwa wingi zaidi lakini mapambano yalikuwa dhaifu, kwa hiyo wafanyabiashara hiyo haramu walikuwa wanajitanua tu.
“Ni wajibu wa kila mtu kumwambia mwenzake aachane na hii biashara, tunapomkamata na ushahidi, hapo anakuwa amekwenda na maji,” alisema Nzowa.
Akichambua zaidi, Nzowa alisema takwimu za madawa ya kulevya aina ya heroin zilizokamatwa katika kipindi hicho ni kilo 30 na washitakiwa ni 45, kati yao wanawake ni wanne.
Alisema, cocaine walikamata kilo nne na watuhumiwa ni 18 ambao ni wanaume watupu na dawa aina ya ephedrine walikamata kilo 12 mshitakiwa ni mmoja mwanaume na bangi ilikamatwa kilo 9,999 na watuhumiwa ni 1,478,  kati yao wanawake ni wawili.
Aliongeza kuwa licha ya kukamata bangi, polisi waliweza kuharibu ekari 300 za mmea huo katika mikoa ya Arusha, Tanga na Mara wilayani Tarime.
Baadhi ya watuhumiwa wa madawa ya kulevya
Kamanda Nzowa akaongeza kwamba polisi wanafanya kazi hiyo nzuri kwa kushirikiana na raia wema.
“Hivi sasa tuko makini sana kwa wasanii na wanamichezo wanaotaka kusafiri kwenda nje ya nchi kwa sababu tumegundua kuwa wanatumika kutokana na umaarufu wao,” alisema Nzowa.
Akifafanua zaidi, kamanda huyo alisema wana taarifa kwamba hivi sasa kuna dawa za kulevya za majimaji, hivyo wanaofikiria kusafirisha hizo kwa njia hiyo wanapaswa kujua kuwa watagundulika.
“Hii ni vita ambayo kila anayelitakia mema taifa hili anapaswa kushiriki kupambana na dawa za kulevya,” alisema Kamanda Nzowa.
KWA NINI VIJANA WENGI WANAKIMBILIA UNGA?
Mtafiti maarufu na mwelimishaji wa maisha ya vijana na jamii kwa jumla, James Mwang’amba, alisema kuwa vijana wengi wanaingia katika wimbi la biashara ya madawa ya kulevya kwa sababu ya kukata tamaa.
“Ukifuatilia maisha ya vijana kwa sasa, utagundua kwamba wengi wao wamekata tamaa. Wanahisi hawana njia ya kutoka kimaisha ndiyo maana wanaona fursa yoyote inayokuja mbele yao inafaa hata kama ni hatari.
“Kila mtu anatamani sana maisha ya juu, awe na kipato kikubwa, sasa kwa vile haoni njia nzuri za kufikia ndoto zake, anaamua kujiingiza kwenye usafirishaji wa madawa ya kulevya ili apate fedha za haraka ili naye awe mtu fulani,” alisema Mwang’amba na kuongeza:
“Tatizo kubwa ni hii tofauti ya kipato. Kuna tofauti kubwa sana kati ya wenye nacho na wasio nacho, hii ni hatari sana. Sasa jamii kwa vijana ni hatari zaidi kwa sababu damu inachemka na kuona kila kitu ni rahisi kufanya.
“Hakuna sababu nyingine kwa nini vijana wengi wanakuwa wauza unga, ukweli ni tamaa ambayo inachochewa na hasira ya kuwa na maisha duni wakati wanawaona wengine wakiwa matajiri wakubwa.”

AJILIPUA KWA PETROLI BAADA YA MUME KUOA MKE WA PILI

Na Victor Bariety, Geita
MWANAMKE mmoja ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Nyankumbu, Kata ya Kalangalala mkoani  Geita amenusurika kifo baada ya kujimwagia mwilini mafuta ya petroli kisha kujilipua baada ya mumewe kuoa mke wa pili.  
Imeelezwa kuwa mwanamke huyo, Anastazia Kubezya (28) Agosti 8 mwaka huu aliamua kujimiminia petroli mwili mzima kabla ya kuchukua kiberiti na kujilipua, hali iliyosababisha  akimbizwe katika Hospitali ya Geita alikolazwa katika wodi namba saba kwa matibabu.
Akizungumza na gazeti hili, Consolata Raphael ambaye ni dada wa majeruhi huyo alidai kuwa chanzo cha mdogo wake huyo kufikia hatua ya kutaka kutumia njia hiyo ya mkato kwa lengo la kujiua ni wivu wa mapenzi.
Consolata alisema: “Siku ya tukio shemeji yangu George Kubezya (mume wa majeruhi), alifika nyumbani kwa mdogo wangu wa kiume akidai kuwa mkewe huyo anatishia kujiua baada ya kuoa mke wa pili.
“Tukiwa tunaendelea kujadiliana mara alitokea mkewe Kubezya akiwa na viatu vya mwanaye mdogo akamkabidhi mdogo wetu mwingine aitwaye Rozalia akamwambia mpatie mwanaye kwa kuwa anaondoka na hajui atarudi lini.
“Baada ya kutamka maneno hayo aliondoka na niliwasiliana na ndugu yetu mwingine aitwaye Elizabeth aliyesema Anastanzia alipita kwake akiwa na chupa ikiwa na petroli na walipojaribu kumkimbiza alipotelea gizani.
“Kati ya saa 4 na saa 5 usiku Eliza na wenzake walisikia mtu akilia nje ya nyuma yao na baada ya kutoka nje walikuta Anastanzia akiwa tayari amekwisha jilipua moto, walipomhoji alidai amefanya hivyo ili afe kutokana na mumewe kumuolea mke mwenza na kumleta kwenye nyumba waliyoijenga yeye na mumewe,”alisema Consolata.
Hata hivyo juhudi za kumpata mumewe kuzungumzia sakata hilo hazikuzaa matunda baada ya kile kilichoelezwa kuwa alitoroka muda mfupi baada ya kumfikisha mkewe hospitalini.
Gazeti hili lilifika hospitalini hapo na kukuta mwanamke huyo aliyelazwa wodi namba nane akiwa anauguzwa chini ya ulinzi wa polisi ili akipona afikishwe mahakamani kwa kosa la kujaribu kujiua.
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Geita, Dk. Adam Sijaona akizungumzia hali ya majeruhi huyo alisema bado si nzuri na wanafanya mpango wa kumhamishia katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyopo jijini Mwanza.




Number one - Diamond (Official Video)


MARLAW BESTA WAPATA MTOTO

Lawrence Marima ‘Marlaw’ na mkewe Besta Prosper.
BAADA ya kuishi kwenye ndoa kwa muda mrefu hatimaye wasanii wa muziki wa kizazi kipya, Lawrence Marima ‘Marlaw’ na mkewe Besta Prosper wamejaaliwa kupata mtoto wa kiume.
Kikizunguza na Ijumaa kwa sharti la jina lake kutoandikwa gazetini, chanzo makini ambacho kiko karibu na wanandoa hao kilisema kuwa wamekuwa wakiweka usiri mkubwa wa maisha yao hasa katika hilo la mimba na hatimaye Agosti 27, mwaka huu Besta alifanikiwa kuitwa mama.
Baada ya kuzinyaka habari hizo paparazi wetu alimtafuta Marlaw ambapo alikiri kupata mtoto wa kiume lakini hakuwa tayari kuelezea zaidi akidai muda wa kufanya hivyo bado.
“Kwa sasa bado ni mapema sana kuzungumzia suala la mke wangu kujifungua kwa undani lakini ni kweli tumepata mtoto wa kiume. Mengine muda ukifika nitaongea,”alisema Marlaw.


WANAWAKE WOTE SOMENI HABARI HII...


Pili alijifungua mapacha hao saa 1:00 asubuhi ya Agosti 18, 2013, nyumbani kwake na baadaye kupelekwa kwenye Hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar baada ya watoto kuonekana si wa kawaida.
Kufuatia matukio kama hayo, Ijumaa Wikienda lilichimba kwa undani ili kubaini nini husababisha wanawake kubeba ujauzito wenye matokeo ya mapacha walioungana au mtoto mmoja kulemaa kiungo chochote cha mwili.
Mtaalam mmoja aliyesomea mambo ya afya ya uzazi ambaye aliomba hifadhi ya jina, ndiye aliyefunua siri hii nzito ambayo wanawake wengi nchini hawaijui isipokuwa kwa kusoma habari hii leo.
Mtaalam huyo alivitaja vidonge maarufu kwa matibabu ya tumbo la kuendesha viitwavyo Flagyl au Metronidazole kuwa ndivyo vinavyosababisha matatizo hayo.
Alisema vidonge hivyo ni hatari mno kwa afya ya mama mjamzito, hasa kwa mtoto aliye tumboni ambaye anatarajwa kukua na kutoka akiwa amekamilika.
“Wanawake wajawazito, hasa wakiwa wa miezi mitatu ya mwazo, hawatakiwi kabisa kutumia vidonge hivi aina ya Flagyl.
“Hivi vidonge ndivyo husababisha tatizo hili la watoto mapacha kuzaliwa wameungana, kitaalam tunaita Siamese Twins.
“Unajua kwa kawaida mimba huanza kuwa binadamu kamili miezi mitatu tu ya mwanzo, kitaalam tunaita First Trimester ambapo kila kitu kinachopaswa kuwa kiungo cha mwilini hufanyika.
“Baada ya hapo mpaka mwezi wa tisa ni kukua kwa viungo hivyo.
“Katika kipindi hiki cha miezi mitatu ya mwanzo kuelekea miezi mingine hadi tisa, mwanamke akitumia Flagyl kwa sababu viungo vinakuwa, ni rahisi kwa watoto kuungana au kuzaliwa wakiwa na ulemavu wowote,” alisema mtaalam huyo.
Mtaalam huyo alisema vidonge hivyo ambavyo hupatikana kirahisi kwenye maduka ya madawa (famasi) hutumiwa zaidi kwa matatizo ya tumbo, hasa la kuendesha.
“Kwa nchi za wenzetu (zilizoendelea), ili mtu auziwe vidonge ambavyo vinaweza kuleta madhara lazima awe na karatasi ya maelekezo ya matumizi kutoka kwa daktari.
“Hakuna daktari wa kweli hata mmoja atakayekubali kumpa Flagyl mwanamke mjamzito, kwa sababu anajua madhara yake,” alisema.
Kuhusu Pili Hija, mapacha wake walifanyiwa upasuaji Agosti 29, 2013 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Kitengo cha Tiba ya Mifupa (Moi) chini ya daktari wa upasuaji wa watoto, Dk. Zaituni Bokhary.
Mtoto aliyebaki ni yule aliyezaliwa akiwa na kichwa, ilibidi kumuondoa asiye na kichwa kwa sababu asingeweza kuwa binadamu kamili.
Dokta Bokhary alisema hii ni mara ya kwanza kwa jambo hilo kutokea katika miaka ya hivi karibuni. Mara ya mwisho lilitokea mwaka 1984.


Sunday, September 1, 2013

GIROUD APELEKA KILIO TOTTENHAM

 Santi Cazorla wa Arsenal akikwaana na Paulinho (kushoto).
 
MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Olivier Giroud leo amepeleka kilio Tottenham baada ya kuipatia timu yake bao la ushindi katika dakika ya 23 ya mchezo. Giroud aliunganisha krosi safi kutoka kwa Theo Walcott na kuwafanya vijana wa Wenger kuibuka kifua mbele na pointi tatu dhidi ya mahasimu wao Tottenham Hotspur. Mechi hiyo imepigwa katika Uwanja wa Emirates jijini London na Arsenal wameshinda bao 1-0.
Katika mtanange huo, vikosi vilikuwa kama ifuatavyo:
Arsenal: Szczesny, Jenkinson, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Ramsey, Wilshere (Flamini 43), Rosicky (Monreal 78), Cazorla, Walcott (Sagna 90)
Tottenham: Lloris; Walker, Dawson, Vertonghen, Rose; Capoue (Sandro 74), Paulinho; Townsend (Lamela 74), Dembele (Defoe 68), Chadli; Soldado





DIAMOND AFUNGUKA KUTENGENEZA NUMBER ONE AFRIKA KUSINI



Msanii Mahiri wa Muziki wa Kizazi Kipya nchini, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' amefunguka na kuelezea sababu za kuamua kufanya video ya ngoma yake mpya ya Number One nchini Afrika Kusini. Diamond aliyetumia kiasi cha Dola za Kimarekani 30,000 zaidi ya shilingi milioni 48 za Kitanzania kutengeneza video hiyo, ameeleza hayo katika video aliyoiweka kwenye Blog yake inayoonyesha maandalizi ya utengenezaji wake. Diamond anasemaa ameamua kuifanyia nchini Afrika Kusini ili kuwa na kitu tofauti, kupata mandhari, washiriki na radha tofauti.
ANGALIA BEHIND THE SCENE NA DIAMOND MWENYEWE AKIELEZEA KUHUSU VIDEO YA NUMBER ONE HAPA CHINI:



Wednesday, April 10, 2013

lava lava ---- shaa (0fficial video)


EXCLUSIVE PHOTO OF PM ODINGA, MOSES WETANGULA AND KALONZO MUSYOKA IN SOUTH AFRICA

Exclusive photo of the big three from left Moses Wetangula, Raila Odinga and Kalonzo Musyoka at the Sundown Savanna in South Africa.


The CORD Summit of the Rt Hon Raila Odinga, Hon Kalonzo Musyoka and Hon Moses Wetangula share a laugh while on holiday in South Africa after a grueling campaign period.
The Principals are taking a few days off to recharge their batteries before returning to push the Reform agenda for the benefit of all Kenyans regardless of political affiliation.
They remain keen to see the faithful implementation of devolution as prescribed in the Constitution of the Republic and urge Kenyans not to lose sight of this.



SHILOLE ANASWA NA BWANA MZUNGU

SIKU chache baada ya kuripotiwa akijiachia kimalavidavi na ‘lejendari’ wa Bongo Fleva, Aboubakar Katwila, staa wa muziki na filamu za Kibongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amenaswa hotelini na bwana Mzungu aliyetajwa kwa jina moja la George, kamera za Risasi Mchanganyiko ni noma.

Shilole akiwa katika pozi na mzungu wake aitwaye George.

Kwa mujibu wa shushushu wetu, tukio hilo lilijiri hivi karibuni katika hoteli moja maarufu jijini hapa ambapo Shilole alikuwa kwenye ziara ya shoo yake.
Ilidaiwa kuwa mara tu baada ya kumaliza ziara ya shoo, Shilole hakuondoka jijini hapa na badala yake alionekana sehemu tofauti akijivinjari na jamaa huyo ambaye uchunguzi wetu ulibaini kuwa ni bosi wa klabu moja maarufu ya usiku Kanda ya Ziwa

akiwa dukani.

Kabla ya kuondoka katika jiji hili la sangara na sato, Alhamisi iliyopita na ndege ya jioni, Shilole alinaswa kimalavidavi na Mtasha huyo Jumatano katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere wa Gold Crest kulipokuwa na maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Syria.
Shilole alishuhudiwa akifanyiwa ‘shopping’ ya kufuru na bwana huyo ambapo gazeti hili lilinasa mpango mzima ambapo lilipotaka kujua kama ni wapenzi, Mtasha huyo alijibu kwa kifupi sana: “No comment” (sina la kusema).

...Shilole na mzungu wake wakijiachia.


..Wakikatiza mitaani.




HIVI NDIVYO UHURU KENYATA ALIVYOAPISHWA NCHINI KENYA

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, akiapishwa.

Uhuru Kenyatta (kulia) akisalimiana na rais aliyemaliza muda wake, Mwai Kibaki.

Uhuru Kenyatta wakati akijiandaa kula kiapo.


 Jaji Mkuu wa Kenya, Willie Mutunga, amtambulisha rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta.

 Rais Uhuru Kenyatta akikabidhiwa upanga na nakala ya katiba ya Kenya kutioka kwa rais mstaafu, Mwai Kibaki ikiwa ni ishara kuwa amekuwa amiri jeshi mkuu wa Kenya.

 Rais Uhuru Kenyatta na 'First lady', Margaret Kenyatta.

 Rais mpya wa awamu ya nne nchini Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta, akisoma hotuba yake mbele ya maelfu ya watu waliofika kushuhudia kuapishwa kwake.

 William Ruto makamu wa Rais wa Kenya akisaini.

Kibaki akiwasili.

Rais Mwai Kibaki anayeondoka madarakani akikagua gwaride la heshima.





MWAKA MMOJA KIFO CHA KANUMBA: LULU MACHOZI MPAKA BASI


STADI wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ (pichani) ameibua upya simanzi, machozi na huzuni ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kifo cha staa aliyeijengea Tanzania heshima kubwa, Steven Charles Kanumba.STADI wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ (pichani) ameibua upya simanzi, machozi na huzuni ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kifo cha staa aliyeijengea Tanzania heshima kubwa, Steven Charles Kanumba.

Msanii Elizabeth Michael 'Lulu' (katikati) akijiandaa kuweka shada la maua kwenye kaburi la Kanumba, kulia ni mama mzazi wa Kanumba, Flora Mtegoa na kushoto ni mama yake mzazi, Lucresia Kalugira.

Gazeti lenye hadhi ya nyota tano, Risasi Mchanganyiko lina mkusanyiko wa matukio ya kuhuzunisha kama yalivyonaswa na timu ya mapaparazi wetu, Jumapili Aprili 07, mwaka huu katika siku maalum ya kumkumbuka, iliyopewa jina la Kanumba Day.
Lulu ambaye aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na marehemu Kanumba, yupo nje kwa dhamana akikabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia msanii huyo mwenye mashabiki lukuki ndani na nje ya Bongo.

DAR ES SALAAM
Shughuli hiyo maalum ambayo ililenga kumuombea dua marehemu Kanumba na kumuenzi kwa mema aliyoyafanya iliambatana na uzinduzi wa Filamu ya After Death ambayo inaelezea maisha ya vijana wadogo aliowahi kuigiza nao katika za Sinema za Uncle JJ, This is It na Big Daddy.
Kanumba Day iliandaliwa na staa wa kike wa kiwanda hicho, Jacquline Wolper ambaye pia ndiye muandaaji wa filamu ya After Death.
Katika hafla hiyo, pia ilizinduliwa sinema ya mwisho kutayarishwa na marehemu Kanumba iitwayo Power & Love ambayo iko chini ya Kampuni ya Kanumba The Great.

KWANZA KANISANI
Awali, mishale ya saa 4:00 asubuhi, familia ya marehemu Kanumba, wasanii, ndugu, jamaa na marafiki walijumuika katika Kanisa la KKKT Usharika wa Temboni katika ibada.
Katikati ya ibada hiyo ya kawaida ya Jumapili usharikani hapo, kulikuwa na sala maalum ya kumuombea marehemu Kanumba.
Utulivu ulikuwa mkubwa kanisani hapo, huku Lulu akiwa katikati ya mama Kanumba, Flora Mtegoa na mama yake mzazi, Lecresia Kalugira wakiwa wamevalia sare ya magauni meupe yenye mchanganyiko kidogo wa rangi na vitambaa vyenye mchanganyiko wa rangi ya pinki na nyeupe vichwani mwao.
Wakati sala ikiendeshwa, Lulu alishindwa kujizuia na kujikuta akimwaga machozi – kazi kubwa kwa wazazi hao ikawa kumtuliza.
Baadhi ya mastaa walionaswa na kamera ya Risasi Mchanganyiko kanisani hapo ni pamoja na Jacob Steven ‘JB’, Vincent Kigosi ‘Ray’, Sabrina Rupia ‘Cathy’, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, Jokate Mwegelo, Irene Uwoya na wengineo.

Wasanii wakiwa katika kaburi la Kanumba.

SAA 6:30 MCHANA
Ibada ilifikia kikomo saa 6:30 mchana ambapo msafara wa kwenda nyumbani kwa mama Kanumba, jirani kidogo na kanisa hilo ulianza.
Utulivu ulikuwa wa hali ya juu nyumbani hapo ambapo wageni wote walipata chakula cha mchana kabla ya safari ya kuelekea katika Makaburi ya Kinondoni....


Saturday, April 6, 2013

KAJALA AANIKA YA JELA


MSANII AFA AKIJIDUNGA

Stori: Denis Mtima
MSANII chipukizi wa muziki wa kizazi kipya aliyetambulika kwa jina moja la Rocky mkazi wa Kawe, Dar amefariki dunia baada ya kujidunga madawa ya kulevya 
   


Ray C
Kwa mujibu wa chanzo kilichoshuhudia tukio hilo na kuomba hifadhi ya jina lake, marehemu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23-27, alipatwa na mauti Machi 27, mwaka huu baada kunywa vidonge kumi vya dawa za kulevya aina ya Valium kisha kujidunga sindano tatu za Cocaine.



Langa
Chanzo hicho kilidai, marehemu alikuwa akionywa mara kwa mara na ndugu zake lakini alikuwa akikaidi hali ambayo ilisababisha akamatwe na kuswekwa jela kwa miezi kadhaa kabla ya kuachiwa.
“Marehemu alitoka Segerea juzi Jumatatu (Machi 25) na Jumanne akaanza kutumia tena dawa za kulevya kama kawaida, akajidunga vidonge kumi kwa mpigo.



Aisha Madinda
“Akaweka kete tatu kwenye bomba la sindano tayari kwa kujidunga ndipo alipozidiwa na kupatwa na umauti akiwa bado hajakamilisha zoezi hilo,’’ kilidai chanzo hicho.
Kabla ya marehemu hajazikwa katika makaburi ya Kawe, askari walifika katika eneo hilo ambapo walibainisha kuwa kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kutumia madawa ya kulevya katika eneo hilo.




Lord Eyez

“Vijana wengi hapa Kawe wamejiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya. Tunawashauri hasa hawa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao walitangaza kuacha basi waache kweli maana wakirudia basi kifo kinawaita.



Msafiri Diof
“Historia inaonesha kuna wimbi kubwa la wasanii ambao wamekuwa wakitumia madawa ya kulevya kwa siri kubwa,” alisema afisa mmoja wa polisi aliyeomba hifadhi ya jina kwa kuwa siyo msemaji.

Thursday, April 4, 2013

SHILOLE, Q-CHILLAH LAIVU!


MWANAMUZIKI wa miondoko ya mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ na muimba Bongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’ hivi karibuni waliawaacha midomo wazi wasafiri ndani ya ndege kufuatia tukio lao la kufanya ‘malavidavi’ bila kujali.

Aibu hiyo ilitokea Machi 29, mwaka huu ambayo ilikuwa Ijumaa Kuu ambapo wasanii hao walikuwa wakitoka Dar kwenda Mwanza kwa ajili ya kufanya shoo siku ya Pasaka.
Akilisimulia gazeti hili, shuhuda wetu aliyekuwemo ndani ya ndege hiyo (jina tunalo) alisema aliwaona Shilole na Q-Chillah wakiwa katika ‘malovee’ ambapo mara kwa mara walikuwa wakipigana mabusu kitendo kilichowafanya abiria wengine kuwakodolea macho yenye kuwashangaa.

“Tunakubaliana na kazi zao, lakini kusema ule ukweli, sisi abiria wenzao tulishangaa sana, unajua kuonesha vitendo vya mahaba ndani ya ndege si utamaduni wetu Wabongo,” alisema abiria huyo aliyekuwa akienda Mwanza kikazi.
Aliongeza kuwa, ilifika mahali baadhi ya abiria walitaka kuwafungukia ukweli kwamba wanachokifanya si adabu hasa ikizingatiwa kuwa wao wana majina makubwa katika burudani za Bongo.
Kufuatia taarifa hizo na kudakwa kwa picha zao, Amani liliwasaka watuhumiwa hao kila mmoja kwa wakati wake ili kusikia kutoka kwao juu ya kufanya madudu ndani ya ‘pipa’.

Kwa upande wake, Shilole alisema kuwa mabusu ni vitu vya kawaida kwake ikizingatiwa Q-Chillah ni mwanamuziki mwenzake kwa hiyo hakuna tatizo.
“Jamani kwani mabusu yana shida gani, yule (Q-Chillah) ni mwanamuziki mwenzangu na tumezoeana. Yale yalikuwa ni mambo ya kawaida tu na utani, si vinginevyo,” alisema Shilole.
Q-Chillah simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita muda mwingi bila kupokelewa, lakini baadhi ya watu wake wa karibu walisema mwanamuziki huyo hana kawaida ya kupokea simu kama namba hazijui.