Thursday, February 14, 2013

KWA WAPENDANAO: MAMBO MUHIMU YA KUFAHAMU KUHUSU VALENTINE'S DAY!


LEO ni Sikukuu ya Wapendanao. Siku maalumu kwa ajili ya kuoneshana mapenzi ya dhati. Ni siku muhimu sana yenye maana kubwa kwa kila mtu, maana upendo hauchagui.

Maana halisi ya siku yenyewe inaharibiwa na watu wanaotumia fursa ya Valentine’s Day kufanikisha matakwa ya misukumo ya tamaa za miili yao. Kama unabisha nenda gesti ukaulizie chumba leo, kila mahali utakuta kumejaa!


ASILI YAKE NI NINI?
Asili yake hasa ni Roma. Ni siku ya kumkumbuka mtakatifu Padre Valentino ambaye alifungwa na kuhukumiwa kunyongwa katika Utawala wa Dola ya Warumi alipokuwa akitetea vijana waoane badala ya kuzini.

Mtakatifu Valentino aliuawa siku na tarehe kama ya leo, ndiyo maana ikatangazwa rasmi kuadhimishwa kwa ajili ya kumkumbuka kama Baba wa Upendo – mtetezi wa wanandoa.

Aliyetangaza rasmi kuadhimisha siku hiyo ni Papa Gelasius.

SIYO NGONO, ANASA!
Baadhi ya watu wameibadilisha maana ya siku hii muhimu kwa wapendanao. Wenyewe wanahisi kuwa ni siku ya kufanya mambo yasiyofaa. Kwao, wapendanao ni ngono. Kuna ambao huanzisha uhusiano siku hiyo kwa lengo la kupata mtu wa kustarehe naye, hili ni kosa.

Kama mtazamo wako ni kutafuta mpenzi mpya na kwenda kustarehe naye utakuwa unakosea sana. Haina maana ya ngono wala anasa na kuharibu fedha kwenye ulevi. Yapo mengi ambayo unaweza kuyafanya kwa lengo la kuifanya siku yako kuwa nzuri.

KUMBUKA NDUGU
Inawezekana unaishi kwenye mji mwingine, kazi zinakubana kila siku na hupati muda wa kuwasiliana mara kwa mara na ndugu zako. Siku ya leo ni nzuri kwako kuwakumbuka na kuwaonesha kwamba unawapenda.

Wapo watu muhimu zaidi katika maisha, wazazi. Mpigie simu mama/baba yako, mwambie unavyompenda na kuthamini malezi aliyokupa hadi kufikia umri ulionao. Kama unaweza watumie hata zawadi kwa ajili ya kuonesha mapenzi yako kwake.

Ondoa fikra mbaya kichwani mwako rafiki yangu. Waza kuhusu mema na kupendana kwa dhati, hapo utakuwa umekwenda sawa na maana ya sikukuu yenyewe.

WAKUMBUKE WAHITAJI
Katika jamii yetu kuna watoto wanaoishi katika mazingira magumu, wazee na wahitaji wengine. Tumia ulichojaliwa kushiriki nao. Siyo lazima iwe fedha, hata chakula na mavazi. Inawezekana una nguo unazodhani hazifai, wape wenzako ambao wanahitaji hapo utakuwa umeonesha namna unavyotambua na kuiadhimisha kwa usahihi.

Ifanye siku hii kuwa ya tofauti zaidi kwa kudumisha uhusiano wako na mpenzi wako na kuzungumzia changamoto mbalimbali za uhusiano wenu kuliko kuwaza starehe na anasa ambazo hupoteza fedha.
Happy Valentine’s Day!




BABA KANUNBA AFUNGUKIA DHAMANA LULU!


KAMA ilivyodhaniwa na wengi kwamba baba wa staa wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kusekwa atazungumzia dhamana ya Elizabeth Michael ‘Lulu’, kweli ameibuka na kusema yupo makini kufuatlia mwenendo mzima wa kesi hiyo ya kuua bila kukusudia.


Hivi karibuni, Baba Kanumba alipiga simu kwenye dawati la Amani na kusema dhamana hiyo ya Lulu haimuumizi kichwa kwa sababu kila mtu ana haki ya kupewa dhamana kutokana na sheria ila yupo makini kufuatilia mwenendo wake.

VAZI LA SHYROSE BANJI FULL UTATA

VAZI alilotinga Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji limezua utata kufuatia kuonesha sehemu yake ya tumboni (kitovu).

Utata huo umekuja mara baada ya picha inayomuonesha mbunge huyo akiwa amejipara (tazama pichani) na kuvalia vazi hilo ambalo linamuonesha sehemu hiyo nyeti na kutupiwa mtandaoni.

“Jamani huu ni utata sasa, inakuwaje mheshimiwa anatinga vazi kama hili? Haya mambo bora angewaachia mastaa wadogo, umri wake haufanani na mambo haya!” aliandika mdau…


Utata huo umekuja mara baada ya picha inayomuonesha mbunge huyo akiwa amejipara (tazama pichani) na kuvalia vazi hilo ambalo linamuonesha sehemu hiyo nyeti na kutupiwa mtandaoni.
“Jamani huu ni utata sasa, inakuwaje mheshimiwa anatinga vazi kama hili? Haya mambo bora angewaachia mastaa wadogo, umri wake haufanani na mambo haya!” aliandika mdau mtandaoni.


sijutii --- Joh makini ft Dunga


STORI YA KISA CHA MWANAMKE KUCHOMWA NA PASI YA MOTO NA MUMEWE IKO HAPA

 
Taarifa ikufikie kwamba jeshi la Polisi Singida linamshikilia mwanaume mmoja aitwae Baltazary Mushi maarufu kama Sumayuni mwenye umri wa miaka 33 kwa tuhuma za kumuunguza mkewe usoni kwa kutumia pasi ya umeme wakati mke huyo akiwa kalala usiku.
Japo chanzo hakijajulikana, kaimu kamanda wa Polisi Singida Thobias Sedoyeka amesema hilo tukio limetokea nyumbani kwa wanandoa hao Singida na mtuhumiwa tayari wanae na atafikishwa Mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
Mwanamke alieunguzwa ambae ana umri wa miaka 30 amesema ndoa yao imedumu kwa miaka sita na nusu mpaka sasa na kwa kipindi chote hicho amekua akikumbana na vipigo vya mara kwa mara.
Namkariri akisema “siku ya tukio alirudi saa nane nikamfungulia mlango akaingia ndani akalala, aliamka majira ya saa kumi usiku wakati nimelala akawasha pasi ya umeme, ilivyopata moto akaja kuniunguza usoni nikiwa niko usingizini kwa hiyo sikuweza kujitetea kwa lolote nilishtuka nikiwa nimeshaunguzwa, alishanivunja mkono kipindi cha nyuma yakaisha…. mpaka tukio hili la kuniunguza na pasi inaonyesha dhahiri kwamba ni mtu anaweza kutoa hata uhai wangu, nataka sheria inisaidie niweze kupata haki za watoto wangu na niweze kurudi kwetu”
 

sorry - barnaba


nashukuru umerudi --- recho


AZMA Ft KITA KIPIMO CHA PENZI

 
 
 

JARIDA LA MARAHA LA MZUKA LIPO MTAANI... WAHI NAKALA YAKO


Vichwa vya habari vya magazeti

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

Wednesday, February 13, 2013

TAZAMA JINSI WATOTO WALIVYOVAA KAMA BEYONCE NA RIHANNA KWENYE REDCARPET YA TUZO ZA GRAMMY 2013

 
 
 
 
 
 
 
 

matumaini anahitaji msaada zaidi

 afya ya msanii wa vichekesho nchini, Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’ kuonekana kuendelea vyema na kuruhusiwa kutoka katika hospitali ya Amana jijini Dar, Mwenyekiti wa Chama cha Waigizaji nchini, Michael Sangu ‘Mike’ amewataka wadau kumsaidika ili afanyiwe uchunguzi zaidi.

Mike aliyasema hayo hivi karibuni alipoongea na Tollywood Newz na kubainisha kuwa Matumaini anatakiwa afanywe uchunguzi wa figo na ini ili aweze kupona kisawasasawa.
“Ingekuwa vyema kama tungejitolea kumsaidia apate vipimo kwenye hospitali kubwa, kwani amerudishwa nyumbani lakini siyo mtu mwenye hali ya kuridhisha, anayetaka kumsaidia atumie namba 0718 951 355,” alisema Mike.



Saturday, November 10, 2012

DIAMOND AFANYA NGOMA MPYA NA DULLY "UTAMU"

DIAMOND AFANYA NGOMA MPYA NA DULLY "UTAMU"
Msanii wa Bongo Fleva almaarufu kama Diamond wa wasafi baada ya kuachia ngoma yake mpya inayofahamika kwa jina la Nataka kulewa sasa
Latest info kutoka kwa msanii huyu ni kwamba ameweza kufanya ngoma nyingine ambayo amepewa collabo na Dully Skyes chini ya Producer P funk kutoka Bongo Records.Baada ya kumaliza kufunguka kuhusiana na collabo hiyo mpya alisema kwamba ni moja kati ya collabo ambayo alikuwa anaisubiri sana na hatimaye wameshamaliza ku record na siku za hivi karibuni inaweza ikatoka.
Check out hapo Diamond akiwa zake ndani ya Bongo Record akifanya vitu vyake sasa hii ni nomaa!!!!!

A.Y AONGELEA KUHUSU MAFANIKO YAKE MWAKANI

A.Y AONGELEA KUHUSU MAFANIKO YAKE MWAKANI
Msanii wa Bong Fleva almaarufu kama A.Y baada ya kutoa ngoma yake inayofahamika kwa jina la Money Money aliyofanya na mwanadada Vanessa Mdee na kupeleka mpaka mashabiki kuendelea kumkubali katika tasnia hii ya muziki sasa
Latest info kutoka kwa A.Y aliweza kueleza focus yake katika mwaka unaokuja alisema kwamba anachotaka kukifanya yeye ni ku focus zaidi kazi zake ziweze kufika mbali Hapa Africa hata nje ya Africa baada ya kusema hivyo alisema kwamba kuna baadhi ya ngoma zake ambazo ameziandaa kwa ajili ya mwaka unaokuja kama kuna collabo aliyofanya na P Funk,Fid Q,Chid Benz na wengineo.@info by A.Y

SUMA LEE ASEMA ATAANZA KUPANDA DALADALA

SUMA LEE ASEMA ATAANZA KUPANDA DALADALA
Msanii wa Bongo Fleva almaarufu kama Suma Lee anayekubalika na ngoma nzuri anazozitoa kwa mashabiki wake kama
Hakunanga,Chungwa,Utanikumbuka na nyinginezo mpaka kupelekea mashabiki wa hapa Tzee kumkubali katika tasnia hii ya muziki sasa kama unakumbuka wiki kadhaa zilizopita msanii huyu aliibiwa gari lake maeneo ya Coco Beach sasa
Latest info kutoka kwa msanii huyu asema kwamba kuanzia sasa ataanza rasmi kupanda Daladala baada ya kusema hivyo aliweza kufunguka na kutoa sababu na kusema kwamba maisha ni popote si lazima mtu au msanii achukue Bajaji au Tax usafiri ni usafiri tu.Hivyo ndivyo alivyoamua kutiririka baada ya kuweka wazi kwamba ataanza kupanda Daladala.

WALTER CHILAMBO AIBUKA KUWA MSHINDI WA EBSS 2012

WALTER CHILAMBO AIBUKA KUWA MSHINDI WA EBSS 2012
Mshindi wa shindano la Epiq Bongo Star Search 2012(EBSS),Walter Chilambo akikabidhiwa sanduku lake lenye kitita cha Sh. milioni 50 usiku wa kuamkia leo ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee,pia katika shindano hilo lililovuta hisia za watu wengi sana,mshindi wa pili amechukua mwanadada Salma Abushir(Zanzibar) na watatu ni Wababa Mtuka(Dar).





Saturday, November 3, 2012

C PWAA AMEACHIA NGOMA MBILI KWA WAKATI MMOJA

 
Here are the two new fresh songs from Tanzania’s finest “CPwaa”. CPwaa hasn’t release any records since last year 2011 November when he released “Hhmm”. Now to please his fans, he is releasing double tracks!!. One a commercial song and one a bonus song for his royal “Crunk Customers” Here is the line up and the songs.
1. Mission 12 O’Oclock - Ft. Anto’Neyo{The Artists}, Godzilla, One Incredable, Lord Eyez and Mabeste.
Production: Middle Class Beats,St.Louis,USA
Vocals: Classic Sounds, TANZANIA (Mona Gangstar)
2. Mambo – ft. Anto’Neyo{The Artists}
Production: Classic Sounds
Producer: Mona Gangstar

CHRIS BROWN KUPIGA SHOW KWENYE TUZO ZA KORA MWAKA HUU

CHRIS BROWN KUPIGA SHOW KWENYE TUZO ZA KORA MWAKA HUU

 
Msanii mahiri kutoka marekani almaarufu kama Chris Brown baada ya kutamba na ngoma zake kadhaa hapa Africa kama Don't judge me,Strip,Yeah 3x. Sasa latest info nilizozipata baada ya kukuta hii picha katika mitandano na kusema kwamba inawezekana Chris brown akapiga show nchini Ivory Coast katika tuzo za kora baada ya kupiga picha na Ernest Adjovi ambaye ni mratibu wa tuzo KORA.

PIGA KURA KWA A.Y NA C.P

SASA WATANZANIA TUMEAMKA
TUNATAKA TUPATE TUZO ZOTE ZA CHANNEL O
TUONESHE UPENDO WETU WA DHATI KUTOKA MOYONI
TUWAPIGIE KURA A.Y NA C.P ILIWAWEZE KURUDI NA TUZO
 
MIMI KAMA C.E.O WA BLOG HII NIMEANZA KWA KUWAPIGIA KURA
SASA NA WAOMBA WATANZANIA WENZANGU NANYI MUWEZE KUWAPIGIA KULA
NI GARAMA NDOGO UNATUMIA ILA USHINDI NA UPENDO UTADUMU MILELE 
 
PIGA KURA KWA A.Y NA C.P

SASA NI ZAMU YA TEMBA: AIBIWA VIFAA VYA GARI LAKE WEZI WADAI WATAENDELEA KWA KUIBA KWA WASANII NA WATANGAZAJI



Alfajiri ya kuamkia leo, Mh Temba ameibiwa vifaa vya gari lake aina ya verossa akiwa amelipaki nyumbani kwake.Temba amesema vifaa vilivyoibiwa ni pamoja na power window, side mirror zote taa za nyuma, radio leseni,na vinginevyo ambavyo thamani yake hajaijua kwa sasa.

"jamaa siwajui ila wamekuja na wameniibia power window, taa za nyuma, sidemirror vitu vya ndani wameiba radio, leseni hadi madaftari yangu ya shule, makaratasi, sasa sijui atakua ametumwa au anafanya maksudi yaani anaiba mpaka madaftari" amesema temba

lakini baada ya wizi huo temba alipiga simu polisi na kati ya info alizopewa na washkaji zake walio central si unajua jamaa likua mwanajeshi kitambo sasa baada ya kuongea na watu wa usalama alipewa ripoti kuwa kuna watu wameamua kuwakomoa wasanii pamoja na watangazaji, kwa kuwaibia mpaka mwenzao alieshikiliwa aachiwe

" kituoni sasa hivi mishe mishe zilizokuwepo ni kwamba kuna jamaa wametangaza kwamba wanaibia wasanii wote magari na mapresenter nao watakoma mpaka mtu wao wakaribu aachiwe, naskia kuna mtu wao ambae wanafanya nae kazi amekamatwa yuko ndani wamesema kwamba wataibiwa wasanii wote na vitu vya magari kwasababu ndio wamesababisha mtu wao amewekwa ndani..." amesema temba

weekend iliyipiya msanii Suma lee aliibiwa gari lake aina ya Land cruser VX yenye thamani ya shilingi milioni 70 maeneo ya coco beach alipokuwa amelipaki na mpaka leo hii halijapatikana tukio lililotokea wiki kadhaa baada ya gari la Ommy Dimpoz kuibiwa vifaa pia

Temba alimalizia kwa kusema, kama angepata nafasi ya kuwakamata wezi hao basi angewatembezea vipara raaaaaah


Friday, November 2, 2012

BE UPDATED


Kwa habari za kijanja kutoka kwenye SIASA,MUSIC,FILAMU,FASHION,UDAKU ndani na nje ya Tanzania usikose kutembelea blog yako daily ili uzidi kuwa mjanja,na pia usisahau kuacha comment,,"KUWA WA KWANZA KUPATA HABARI

DIAMOND - show-niliyofanya-jana-kwenye-uzinduzi WA JIJI LA ARUSHA

CLICK HAPO CHINI KWA HABARI ZAIDI

KUTOKA BONGO 5,,exclusive-sikiliza-nataka-kulewa-ya-h-baba-anayodai-diamond-ameiba-idea-11-2012/


H.Baba ameileta Bongo5 cd yenye demo ya wimbo wake 'Nataka Kulewa' ambayo anadai ameibiwa idea na Diamond. Wengi walikuwa hawaamini na kusema H.baba anatafuta pa kutokea. Kama bado huamini usikilize mwenyewe hapa: http://www.bongo5.com/exclusive-sikiliza-nataka-kulewa-ya-h-baba-anayodai-diamond-ameiba-idea-11-2012/

hivi ndivyo hali ilivyokuwa Mahakama ya Kisutu jijini Dar leo

hivi ndivyo hali ilivyokuwa Mahakama ya Kisutu jijini Dar jana 


Kiongozi wa Askari magereza, akiwaongoza Sheikh Ponda na wenzake, kutoka mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, baada ya kuahirishwa kwa kesi yao

Kiongozi huyo mwenye msimamo mkali, alifikishwa kwa mara ya pili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu pamoja na wafuasi wake ambapo hakimu anayesikiliza kesi dhidi yake, Victoria Nongwa, ya kuvamia eneo la Markaz, Chang'ombe jijini Dar es Salaam, ambapo waliharibu  na kuiba mali mbali mbali zenye  thamani ya shilingi milioni 59, madai ambayo washtakiwa wote waliyakanusha.

Hakimu huyo alikubali kutoa dhamana kwa washtakiwa wote isipokuwa kiongozi huyo ambaye ni mshtakiwa namba 1 kwa madai kuwa bado Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), hajaondoa pingamizi lake la kuzuia dhamana kwa mshtakiwa namba moja.

Ulinzi katika mahakama hiyo ulikuwa ni mkali na haujawahi kutokea katika miaka ya hivi karibuni, ambapo pamoja na mambo mengine, palifungwa CCTV Cameras, vifaa vya kugundua vitu vyenye asili ya chuma, polisi wa kutuliza ghasia magereza na wale wa FFU, polisi wa farasi na mbwa, pamoja na askari kanzu waliotapakaa kila kona ya maeneo ya jirani na mahakama hiyo kubwa jijini Dar es Salaam.

Kikundi kidogo cha wafuasi wa Sheikh Ponda, kilijaribu kuleta rabsha, lakini polisi walitumia busara na kuwaelekeza kilichoamuliwa mahakamani ambapo pamoja na kusuasua kuondoka eneo hilo la mahakama, lakini hatimaye waliondoka huku  polisi wa kutuliza ghasia wakiwafuata kwa nyuma hadi eneo la makutano ya barabara za Bibi Titi na ile ya Morogoro nao wakatawanyika.

Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika vya habari, kulikuwepo taarifa kuwa wafuasi hao walipanga kutega milipuko kwenye eneo la mahakama na pia walisambaza vipeperushi vyenye vitisho kadhaa, ikiwa ni pamoja na kufanya maandamano makubwa ya kulazimisha kiongozi huyo aachiliwe.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 15 mwaka huu itakapotajwa tena
 



Wafuasi wa Ponda, wanbaoshatakiwa pamoja naye, wakifunguliwa pingu mahakamani

Mshtakiwa akiwa amebebwa na mwenzake baada ya kudondoka mahakamani na kupoteza fahamu

Askari wa kutuliza ghasia magerezani, nao walikuwepo kikamilifu


Askari wa kutuliza ghasia magereza, akiwa ameshika lindo mbele ya mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Alhamisi Novemba 1, 2012

 
Polisi wa Mbwa nao walichukua nafasi yao


Huiingii mahakama ya Kisutu bila ya kukaguliwa na mashine za kugundua vitu vya asili ya chuma hapo.


Farasi wa polisi wakiwafukuza wafuasi wachache wa Sheikh Ponda, waliojikusanya nje ya uzio wa mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Alhamisi Novemba 1, 2012


Polisi wa Mbwa wakisubiri amri ndani ya gari lao nje ya mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam, Novemba 1, 2012


Polisi wa Mbwa akifanya doria kwenye barabara ya Bitbi Titi mbele ya jengo la mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam


Askari Magereza wa kutuliza ghasia, aliyejihami kwa silaha na vifaa vingine akiwa makini kulinda usalama


Sheikh Ponda na pingu zake mikononi, akirejeshwa rumande.


introducing “MONEY” by AY Feat.V(BrAnD NeW TrAcK)

introducing “MONEY” by AY Feat.V(BrAnD NeW TrAcK)


His name is Ambwene Yessayah.But to his fans and even close people, he is just AY. He became a household name in the music industry of Tanzania a while ago and became  even more popular when, with other big names, established The East Coast Team with their HQ in Upanga area of Dar-es-salaam. It is the same “gang” that brought up MwanaFA, one of AY’s closest friends, music partner and collaborator in a number of hits.

From way back then to now he is also known as “Mzee wa Commercial”…for him,apart from everything else, commerce first and that means Money…just as the song bearing the same title that I am about to introduce to you. It is also not a secret that he is well known to be the HARDEST WORKING HIP HOP ARTIST IN TANZANIA.
AY works hard and party hard as well. He has so far collaborated with a good number of internationally hitting artists and he is not showing any signs of getting even close to become tired.
Here is another club anthem from him featuring V. This is a production of Marco Chali at MJ Records in Masaki.


GARI LA JACKLYN WOLPER LACHOMWA MOTO

GARI LA JACKLYN WOLPER LACHOMWA MOTO



Jacqline ameandika kwenye blog yake na namkariri akisema “kiukweli mimi kama Jacquline Wolper sina ubaya na mtu yeyote, ila nmeshangaa kuona watu nisiyo wajua kuja usiku wa manane na kunichomea gari yangu. Kiukweli siwezi kumuhisi mtu ila najua ni lazima atakua mtu asiependa maendeleo yangu ni ni mtu mbaya sana kwangu. Na inawezekana kabisa alipanga kunia lakni kwa bahati nzuri siku hiyo sikua nyumbani nilikua nimesafiri. Tukio lilitokea usiku wa tarehe 23/10/2012 ambapo mtu alitumia matambara yaliyo na mafuta ya taa au Petrol akiwa kwa nje ya ukuta wa nyumba yangu akiwa anarusha kwa ndani. Nimepeleka taarifa kituo cha Polisi kawe kwa kutaka msaada wa kiupelezi na nitakua nawapa taarifa za kila kinachoendelea. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwani niko salama”