Friday, April 25, 2014

kocha wa zamani wa Barca Vilanova afariki dunia

Kocha wa zamani wa Barcelona Tito Vilanova amefariki akiwa na miaka 45, imetangaza Club hiyo.
Katika statement waliyoitoa Barca wamesema: " Club inatoa pole juu ya kifo cha TitoVilanova, ambae amefariki leo hii akiwa na miaka 45, Barcelona.
Vilanova, Midfielder wa zamani, alikuwa akiugua ugonjwa wa saratani ya koo kwa zaidi ya miaka 2, ugonjwa uliomlazimisha kuachia ngazi kama boss wa barca. 

Vilanova alichukua madaraka kwa Guardiola mwanzoni mwa msimu wa 2012/2013, lakini alilazimka kuchukua likizo ya miezi minne kati ya December 2012 na April 2013 kwa ajili ya matibabu nchini Marekani, na kutibiwa.
Vilanova ambae alilazwa katika hospitali iliyoko Barcelona wiki iliyopita ameacha mke na watoto wawili

Baada ya kukutana kwa siku 67,Bunge maalum la katiba kuahirishwa leo.

bungeeeBunge maalum la katiba leo April 25 linahairishwa bila kupitisha ibara hata moja kati ya 240 ambazo zimo katika rasimu ya katiba bunge hili linahairishwa mpaka mwezi Agosti mwaka huu huku likiendelea kujadili sura ya kwanza na ya sita yenye jumla ya ibara 19 zinazohusu masuala yanayojega msingi wa aina ya muungano unayopendekezwa.
Tume ya mabadiliko ya katiba katika rasimu ya katiba iliyowasilishwa bungeni na aliyekua Mwenyekiti wake Jaji Warioba ilipendekezwa muundo wenye shirikisho la serikali 3,pendekezo ambalo bado limeleta mtafaruku bungeni baada ya kutengeneza pande mbili bungeni kutokana na mgawanyiko huo kauli zenye utata,kejeli,matusi,dhihaka na ubaguzi ni mambo yanayojitokeza sana kwenye sura hizo mbili.
Miongoni mwa vitu vinavyolaumiwa kwa bunge hili la katiba ni matumizi ya lugha zisizofaa kwenye uchangiaji bila kujali kuwa bunge hilo linatazamwa na watu wa rika mbalimbali.

Hii ni kali nyingine kutoka Kenya,Cheki ugumu wa sheria hii mpya inayotaka kuundwa.

Kenya's Supreme Court judges file into the chamber during the opening of the 11th Parliament in NairobiSheria mpya inatengenezwa Kenya sheria hiyo itawataka wanaowazungumzia wakuu wa serikali kufanya mazoezi ya kutosha kwani sheria hii ikipitishwa basi inamaana kwamba Rais,Naibu wake na wake zao pekee ndiyo watakao pewa jina Mtukufu au His/Her Excellency.
Unaambiwa yeyote atakaye kosa kuzingatia hilo adhabu yake atafungwa mwaka mmoja Gerezani au kutozwa faini ya shilingi milioni moja pesa za Kenya sawa na dola elfu 12 za Marekani.
Yeyote atakaye vunja sheria ya kukosa kumuita Mbunge kwenye bunge la kitaifa Mheshimiwa au Honorable atafungwa mwaka mmoja au faini ya shilingi milioni mbili pesa za Kenya.
Kwenye mpangilio Rasmi wa Itifaki ama pecking order Rais atafatiwa na Naibu wake kisha Spiker wa bunge la taifa,Jaji mkuu,Seneta,Mbunge wa Jimbo na wa mwisho ni Gavana.
Sheria hiyo pia inapendekeza kwamba spika wa bunge la taifa kuitwa Right honourable ama Mheshimiwa mkuu na Jaji mkuu kuitwa his/herloadship,itakua kosa vile vile kumuita mwakilishi wa Jimbo Mheshimiwa hilo ni jina la Mbunge wa Bunge la Taifa peke yake.
Muswada huo uliotungwa na kuwasilishwa Bungeni na Mbunge Mheshimiwa Aden keynan anaye sema kwamba sheria hiyo itasaidia kutoa mpangilio wa vyeo kwa Taifa pia anapendekeza kwamba watumishi wa umma watakao jilimbikizia vyeo watatozwa faini ya Dola milioni mbili.
Mswada huo unajadiliwa Bungeni wakati magavana serikali ya kitaifa, wabunge na mahakama wako kwenye vita vya kubaini ni nani anauwezo wa kutekeleza majukumu na mamlaka ya kutoa muelekeo kwenye maswala mbali mbali yanayo husu usimamizi.

Okwi: Simba SC imenipa magari sita


Okwi huyo akiondoka!
Shakoor Jongo na Musa Mateja
MSHAMBULIAJI wa Yanga, Emmanuel Okwi, kwa sasa yupo nchini Uganda, aliondoka juzi Jumatano na kuzungumza na Gazeti la Championi Ijumaa pekee huku akiitaja Simba.
Okwi ambaye aligoma kucheza mechi za mwishoni mwa Ligi Kuu Bara, msimu uliomalizika hivi karibuni kutokana na kile kilichoelezwa kuwa alikuwa hajamaliziwa malipo ya usajili wake, amefunguka kuwa Simba ndiyo ambayo imemfanya kuwa vizuri kiuchumi.
Okwi akiingia ndani ya uwanja kwa ajili ya ukaguzi.
Raia huyo wa Uganda ambaye alisajiliwa ‘bure’ Étoile du Sahel ya Tunisia akitokea Simba, kabla ya baadaye kutua AS Villa ya Uganda na kisha Yanga, ameishukuru Simba kuwa ndiyo iliyochangia neema nyingi na kumfanya ajiweke vizuri kiuchumi kwa kuwekeza zaidi nchini kwao Uganda.
Okwi amesema kuwa alipokuwa Simba ni wakati ambapo aliweza kufanya mambo mengi ya kukuza pato lake ikiwemo kununua magari sita aina ya Fuso kwa ajili ya biashara, magari mengine binafsi pamoja na nyumba ya kifahari.
“Naipenda sana Tanzania na nina mambo yangu mengi tu huku,” alisema Okwi muda mfupi kabla ya kuondoka nchini, juzi, aliendelea kufunguka:
“Siyo mshahara pekee wa Simba lakini nilipokuwa pale nilikuwa nikipata vitu vingi, mfano kuna mwanachama mmoja mwanamke alinipa gari, mashabiki nao walikuwa wakinipa vitu vingi, nawashukuru sana kwa yote.”
Okwi akienda kupanda ndege.
Okwi aliongeza kuwa anarejea Uganda kwa kuwa Ligi Kuu Bara imemalizika lakini akatoa kauli kuwa atarejea baada ya wiki tatu kwa ajili ya kukamilisha mambo yake binafsi.
“Kuna vitu fulani nitakuja kuvifanya, siwezi kuvizungumza kwa kuwa ni vyangu binafsi, lakini nafikiri muda ukifika nitazungumza mengine mengi, Watanzania watajua, huu siyo wakati sahihi,” alisema Okwi.
Wakati akiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar, Okwi alisindikizwa na watu wawili waliokuwa wamebeba mabegi yake, alipofuatwa na mwandishi wa habari (siyo wa Championi) akaweka simu sikioni na kutotaka kuzungumza chochote.
Lakini baada ya kuachwa iligundulika baadaye kuwa simu ilikuwa imezimwa na alikuwa haongei na mtu yeyote.

CHUCHU NA RAY KAMA KIM NA KANYE

KUKOPI na kupesti bila kuboresha! Mastaa wenye mapenzi kama ya njiwa kutoka kiwanda cha filamu za Kibongo, Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray The Greatest’ wamekuwa wakitupia swaga za picha kama zile za Kim Kardashian na mwandani wake, Kanye West.
Wasanii wa filamu za Kibongo, Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray The Greatest’ wakijiachia.
Kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii, Chuchu na Ray ambao majina yao yameunganishwa na kuwa Chura wamekuwa wakichukua sampo za picha za akina Kim nao kujifotoa kisha kuzisambaza.
“He! Mmewaona Chuchu na Ray? Eti wanakopi na kupesti swaga kama zile za Kim na Kanye kisa mapenzi yamekolea,” alisema mdau mmoja baada ya kuziona picha hizo mtandaoni.

WEMA: NAJUTA KUMLIPIA KAJALA MIL 13!

Stori:Na Shakoor Jongo KAMA kuna kitu kinakukwaza ndani ya moyo wako, siku zote ukikaa nacho kitazidi kukuumiza lakini ukiamua kumtafuta mtu ambaye umeshibana naye na kumsimulia, moja kwa moja utakuwa umeutua mzigo!
Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akiwa Kajala Masanja.
Hicho ndicho amekifanya Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ kwa kuweka kweupe chanzo cha ugomvi wake na staa mwenzake, Kajala Masanja huku akijuta kumlipia mwanadada huyo zile Sh. milioni 13 za faini ili asiende jela miaka saba.
Akizungumza na Ijumaa katika exclusive interview Jumanne iliyopita, Wema ambaye pia ni staa mkubwa wa sinema za Kibongoalisema kuwa kuna mambo mazito ambayo yamesababisha yeye kuingia kwenye gogoro kubwa na Kajala.Wema au Beautiful Onyinye alisema kwamba mambo hayo ndiyo yamemsababishia maumivu ya moyo na kutokwa machozi kila wakati.
“Leo (anataja jina la mwandishi), ngoja nikuelezee kila kitu kinachohusiana na mimi na Kajala juu ya tofauti zetu.“Naamini baada ya kusimulia kisa na mkasa nitakuwa nimeutua huu mzigo mkubwa nilionao ndani ya moyo wangu.
“Baada ya hapo sitapenda tena kuzungumzia ishu inayonihusu mimi na Kajala,” alianza kufunguka Wema.
UZINDUZI WA KIGODORO
Katika maelezo yake, cha kwanza, Wema ni uzinduzi wa Filamu ya Kigodoro uliofanyika hivi karibuni kwenye Ukumbi wa Dar Live, Mbagala-Zakhem jijini Dar ambapo yeye alisema kuwa alianza kuyaamini yale yaliyokuwa yakisemwa na watu kuhusiana na Kajala.
Wema alisema kabla ya tukio, akiwa saluni akijiandaa kwa ajili ya uzinduzi huo, ghafla Kajala alimharibia ‘mudi’. “Unajua ile Saluni ya (anataja jina la saluni) pale Kinondoni, ina sehemu mbili, juu na chini, sasa mimi nilikuwa juu na Aunt (Ezekiel) tunatengeneza nywele.
“Niliposhuka kwa ajili ya kuosha nywele, nikamuona Kajala, kwa kuwa nilikuwa sijaonana naye siku nyingi na tayari maneno yalishaanza kuwa mimi na Kajala tuna bifu, nikaona nioneshe kuwa sina bifu naye.
“Kweli nilipiga makelele ya furaha nilivyomuona K, nikawa nakimbia kwenda kumkumbatia, kiukweli niliishiwa nguvu baada ya kunikwepa na kusema nooo...Wema usinikumbatie na kuanza kutoa maneno ya dharau eti nitamchafua.
“Kusema kweli niliishiwa nguvu na kuona kama vile kizunguzungu huku aibu ikinijaa ghafla kwani pale kulikuwa na watu wengi, basi huwezi kuamini, nilishindwa kujizuia nikajikuta namtukana, sikumbakisha.
“Wakati namtukana alikuwa amekaa kwenye kiti cha kuoshwa, nikaenda nikamsukuma na kumfukuza pale kwenye kiti ili nikae nioshwe, huwezi amini hali ya hewa iliharibika ghafla kwani sikuwa na mudi tena,” alitiririka Wema.
SAFARI YA ARUSHA KATIKA SHOO YA MIRROW
Wema alisema kuwa baada ya kutofautiana pale saluni, hakuwa na kinyongo, safari ya Arusha ilipofika walikwenda kumsapoti msanii wao wa Bongo Fleva anayesimamiwa na Kampuni ya Endles Fame Production.
Wakiwa njiani, kwa mujibu wa Wema, yeye alikuwa hana fedha taslimu za kutosha zaidi ya kubeba kadi zake saba za ATM tofauti hivyo alimwambia Kajala ampe shilingi laki tatu kwa ajili ya watu kula na kunywa njiani pamoja na matumizi madogomadogo.
Alisema Kajala hakuwa na shilingi laki tatu akampa shilingi laki mbili na elfu themanini.
Aliendelea kutoa ya moyoni: “Tulipofika Arusha Kajala alimwita ndugu yake mmoja anayeitwa Doli kisha akamwambia achukue fedha alizokuwa nazo akamuwekee benki kwa sababu sikuwa na fedha na nilianza kukopa eti nilijishaua kuandaa shoo nikitegemea fedha zake.
“Wakati K anazungumza hivyo kulikuwa na watu watatu, mimi sina hili wala lile nikamuuliza mtu mmoja mbona siwaoni, wamekwenda wapi?
“Ndipo nikafungukiwa kuwa wananikimbia kisa nimemkopa K hizo laki mbili na elfu themanini, kiukweli iliniuma sana, Kanalalamikia laki mbili? Tena hakunipa bali alinikopesha?
“Nilijiuliza amesahau mimi nilitoa Sh. milioni 13 kumlipia faini asiende jela miaka saba? Nguo nikinunua nanunua sare, nywele sare, viatu sare, mapochi sare, ninachokula na kunywa mimi ndicho hichohicho.
“Siku zote wakati akiwa gerezani nguo, viatu, hereni yaani kila kitu nilikuwa ni mimi, leo laki mbili na elfu themanini, niliyomuazima ananitangazia kwa watu (anataja jina la mwandishi)?
“Iliniuma sana basi palepale, nikaenda benki nikatoa Sh. milioni mbili, nikamlipa fedha zake, nikakaa kimya nikijifanya sijui chochote kinachoendelea kwani ningefanya chochote ningeharibu shoo na isingekuwa na maana yoyote ya sisi kwenda Arusha.”
WAREJEA DAR, MAANDALIZI YA FILAMU YAKE YAANZA
Wema alisema waliporejea Dar, alimwambia Kajala kuwa kuna mtu aliyekuwa amempa stori hivyo alimuomba wafanye filamu wawili.
Alisema kwamba Kajala alikubali na kusema kuwa atachangia Sh. milioni tano katika bajeti ya filamu hiyo.Baada ya kusikia hivyo, Wema alisema alifarijika, alipokwenda kumweleza ‘bebi’ wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, naye Diamond akasema atatoa Sh. milioni tano hivyo jumla itakuwa Sh. milioni kumi ikapita bajeti iliyokuwa imepangwa ya Sh.milioni nane.
Anaendelea: “Tukiwa katika maandalizi ya mwisho tuanze ku-shoot, K alinipigia simu akaniambia hawezi ku-shoot kwani alikuwa na safari ya kwenda China labda wa-shoot vipande vyake, nikamwambia basi aende akirudi tutatengeneza nyingine.
“Baada ya kuona hivyo ndipo nikamchukua Aunt tutengeneze filamu. K alipoona nimemchukua Aunt, akanipigia simu na kuanza kuongea shiti.“Nilijiuliza mbona mwenzangu amesahau ghafla wema wangu niliomtendea au kwa kuwa tangu aanze vijisafari vyake vya kwenda China anapata