Friday, March 14, 2014

Unaamini huyu mshkaji kafanana na Marehemu Ngwea kwa asilimia 100?


ngwea2Tamasha la Xxl Afta xkul Bash ndio sehemu ambayo nilimuona huyu jamaa baada ya kujitokeza kwenye mashindano ya kumtafuta Mtu anaefanana na Star.
Nikaona si mbaya tukafahamu hata kwa uchache historia yake na anamjua vipi Marehemu Ngwea.
ngwea‘Mi naitwa Mohamed au Junior weezy, junior weezy kwa sababu imekua Talk of Town gumzo Town kila mtu Ngwea Ngwea,mi Ngwea namfaham kama artist so nimeonana nae mara ya mwisho nikiwa mdogo lakini Jay Moe alimwambia Ngwea unafanana sana na jamaa pale ndo ilikua mara yangu ya kwanza naya mwisho kuonana na Ngwea’.
ngweaaa‘Yeah ilikua mwaka 2003 baada ya Jay Moe kumwambia unafanana sana na dogo alisema ndio kweli nafanana nae lakini mtu aliekuja kunifahamisha zaidi ni Dully,Dully alisema unafanana sana na Ngwea na mpaka leo huwa ananiita Ngwea.watu walinishawishi kulingana na hii sura nliyonayo watu wamenishawishi taratibu naanza kuingia kwenye game bado sijafanya track nipo njiani,nakutana na vituko vingi wengine wananikimbia wanasema nimefufuka na vitu vingine vya ajabu nakutana navyo mtaani muda mwingine nasisimka nahisi kama Mangwea yuko ndani ya mwili wangu,naweza kuimba baadhi ya ngoma za Ngwea kama tupo juu..na baadhi ya ngoma zingne.
ngweeeeaaa
ngwea na mox
ngweaaa

Picha za Ommy Dimpoz akiwa chini ya ulinzi wa polisi Uingereza.. making the video


Screen Shot 2014-03-13 at 4.02.45 PMOmmy Dimpoz amethibitisha kufanya video yake mpya nchini Uingereza chini ya director ambae amehusika kuzifanya video za mastaa kama Fuse ODG, Wizkid na Davido ‘skelewu’
Leo Dimpoz ameshea picha za sehemu ya video yenyewe ambazo inamuonyesha akiwa kwenye ulinzi wa askari wa Uingereza.
Screen Shot 2014-03-13 at 4.03.03 PM

Rihanna na Drake tena, hizi ni za jana usiku Manchester.


article-0-12804583000005DC-500_634x416Kwa muda mrefu kumekuwa na tetesi za mastaa wa muziki Drake na Rihanna kwamba wamerudisha uhusiano wao wa kimapenzi.
Ingawa wawili hao waliopachikwa jina la ‘AubRih’ (Kwa maana ya Aubrey na Rihanna) mpaka sasa wamekuwa wakisisitiza bado ni marafiki wa kawaida, headlines zao za hivi karibuni zinaonyesha kuna kitu zaidi ya urafiki kati yao.
Rihanna amekuwa akionekana na Drake wakiongozana kwenye ziara ya kimuziki ya Drake Ulaya ambapo kwa mara ya kwanza walionekana pamoja nchini Ufaransa, kisha Ujerumani na jana usiku walionekana pamoja jijini Manchester – England.
Na hizi ni picha za ushahidi wa wawili hao walivyokuwa wakijiachia kwenye mitaa ya jiji la Manchester usiku jana.
article-2579060-1C3C049300000578-520_634x434
Drake na Rihanna kwenye mitaa ya Manchester jana usiku
article-2579493-1C3BAD6900000578-472_634x389

Weekend hii unaweza kuitumia kwa kuangalia hizi movie kwenye theater tofauti.


movieni300 Rise of an Empire ni movie ambayo inategemewa kuangaliwa sana na watu wengi kuanzia kesho kwenye theaters za hapa Tanzania.
Movie hii ambayo itaonyeshwa kwenye 3D imetoka kwa director wa 300 na Man of Steel. Pamoja na hiyo kuna movie nyingine zitakazoonyeshwa kwenye muda tofauti.
Cheki hizi ratiba na uchagua movie yako ya kwenda kuangalia kuanzia kesho 14/3/2014
1932722_518380071615403_998529629_o
1977464_10152082969808842_1854562348_n
1262536_518379108282166_178997219_o
1921189_518379384948805_551108562_o

Taarifa za Mtumbwi uliozama Mtwara March 13 ukiwa na kina mama wauza samaki..

Screen Shot 2014-03-13 at 10.13.49 PMTaarifa kutoka Mtwara ambazo zimethibitishwa na jeshi la Polisi ni kuhusu Mtumbwi ambao umezama wakati ukivuka kutoka kitongoji cha Ng’wale kwenda ng’ambo ya pili ambapo ndiyo sehemu waliyokuwa wanashukia abiria waliokuwepo.
Tayari watu 21 wamefikishwa katika hospital ya mkoa wa Mtwara kwa matibabu ambao wote ni wakina mama pamoja na mtoto mmoja wa kiume wa mwaka 1 huku waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo wakiwa ni wakina mama 3.
Mtumbwi huo unahisiwa ulikuwa na abiria 24 ambapo pamoja na wahusika wawili wa mtumbwi huo kwa pamoja, jumla ya watu waliokua kwenye mtumbwi ni 26 ambapo Polisi wanasema kina mama hao walikua wanatoka kutafuta samaki kwa ajili ya biashara.
Jeshi la polisi bado linamtafuta aliekua anauendesha huo Mtumbwi ambae inasemekana aliogelea na kutoweka baada ya mtumbwi kuzama.
Chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika ingawa baadhi ya abiria wanadai ni upepo mkali na mvua iliyokuwa inanyesha kwenye eneo hilo.

Kurasa za mwanzo na mwisho magazetini leo March 14 2014


.
.
Ni utaratibu wa millardayo.com kila siku kukupa nafasi ya kusoma kurasa za mwanzo na mwisho za magazeti mbalimbali ya Tanzania.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.