Saturday, January 4, 2014

MASHABIKI WAMPONGEZA SCHUMACHER HOSPITALINI BIRTHDAY YAKE YA MIAKA 45

Michael Schumacher.
MASHABIKI wa Michael Schumacher leo walimtumia salamu za kuadhimisha kutimiza mwaka wa 45 tangu kuzaliwa kwake wakati akiwa amelazwa hospitalini kutokana na kujeruhiwa vibaya kichwani wakati alipokuwa akishiriki mchezo wa kuteleza kwenye barafu maeneo ya Alps nchini Ufaransa.
Schumacher ambaye ni mshindi wa mara kadhaa wa mbio za kuendesha magari  za Formula One (F1) hivi sasa anapata matibabu akiwa hajitambui baada ya kufanyiwa operesheni ya kichwa ambapo alikipigiza kwa bahati mbaya kwenye jiwe.
Schumacher ambaye mashabiki wake humwita Schumi, ndiye dereva mwenye  mafanikio zaidi katika mashindano ya  F1 akiwa ameshinda mara 91 kabla ya kustaafu mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment