Sunday, September 28, 2014

WAKAZI WA MBEYA WAFURIKA KWENYE SEMINA YA KAMATA FURSA

Msanii Mrisho Mpoto akiongea na wakazi wa Mbeya waliojitokeza kwenye Semina ya Kamata Fursa mapema leo ndani ya Ukumbi wa Benjamini Mkapa.Msemaji kutoka GS One, Pius Mkongoti akiongea na wakazi wa Mbeya waliokuwa wamefurika kwenye Semina ka Kamata Fursa, tayari kwa kuwapa mbinu za kutomia huduma ya Bar code. Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego akisalimiana na wakazi wa Mbeya waliokuwa kwenye Semina ya Kamata Fursa muda mfupi baada ya kupewa nafasi ya kujitambulisha kwao na kuwaambia namna alivyojipanga kulishambulia jukwaa la Fiesta usiku wa leo ndani ya Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.Ofisa Utekelezaji wa NSSF, Ally Mkulembo, akwapatia mbinu  za kujikwamua kimaisha wakazi wa Jiji la Mbeya kupitia mafao na huduma mbalimbali za NSSF.Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, akiongea jambo wakati wa ufunguzi wa Semina ya Kamata Fursa ndani ya Ukumbi wa Benjamini Mkapa uliyopo Mbeya mjini.Msanii wa Bongo Fleva Godzilah, akishusha mistari kwa wakazi wa Mbeya waliokuwa kwenye Semina ya Kamata Fursa muda mfupi baada ya kupewa nafasi ya kusalimiana nao.Baba Levo, akiwaambia wakazi wa Mbeya namna ambavyo yeye aliweza kutumia Fursa kupitia huduma mbalimbali zitolewazo na NSSF.
Msemaji wa SSRA Stewart Bisanda akiwapatia mbinu mbadala za kujikwamua kwa kutumia fursa mbalimbali zilizopo mkoani Mbeya.Msanii wa Bongo Fleva Hamad Ally 'Madee', akiongea jambo mbele ya wakazi wa Mbeya waliokuwa wamefurika katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa mapema leo kwa ajili ya kujifunza mbinu mbalimbali za kutumia fursa zilizopo mjini hapo.Baadhi ya umati wa wakazi wa Mbeya mjini wakifuatilia kwa makini Semina ya Kamata Fursa iliyokuwa ikiendelea mapema leo ndani ya Ukumbi wa Benjamin Mkapa.Mwanadada Recho ambaye ni msanii wa Bongo Fleva akicheka baada ya kupokelewa kwa shangwe na wakazi wa Mbeya mara baada ya kuingia kwenye Ukumbi wa Benjamin Mkapa ambapo kulikuwa na Semina ya Kamata Fursa.Chipukizi wa Bongo Fleva Baraka Da Prince akisalimiana na baadhi ya wakazi wa Mbeya Mjini waliokuwa wamefurika kwenye semina ya Kamata Fursa ndani ya Ukumbi wa Benjamin Mkapa.Estelina Sanga 'Linah', akiimba moja ya mstari uliopo kwenye wimbo wake wa Ole Themba, mara tu baada ya kupewa nafasi ya kusalimiana na wakazi wa Mbeya waliokuwa wamejitokeza kwenye semina ya Kamata Fursa.Meza kuu ya wazungumzaji wa Semina ya Kamata Fursa ikifuatilia baadhi ya mambo yaliyokuwa yakiendelea ukumbini humo kabla ya wazungumzaji hao kukaribishwa kwa kutoa mafunzo na mbinu mbalimbali za kuwawezesha wakazi wa Mbeya kutumia Fursa zipatikanazo mkoani hapo.

No comments:

Post a Comment