Saturday, November 9, 2013

TUNAMJUA ZAIDI JAY Z, HATUMUELEWI KIDA WAZIRI

TUNAMJUA ZAIDI JAY Z, HATUMUELEWI KIDA WAZIRI

Mambo vipi maanko?
Awali ya yote, ninaomba kuomba radhi kwamba katika makala iliyopita, kwa bahati mbaya, niliandika kwa makosa kwamba Chonya alipatikana katika kitabu cha Kuli. Usahihi ni kwamba huyu jamaa alipatikana katika kitabu cha Shida na ninawashukuru wote walionikosoa!
Mimi ni shabiki wa Arsenal. Nina furaha kwamba timu yangu ilishinda mechi yake ya Jumatano dhidi ya Borussia Dortmund ya Ujerumani katika michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya na nadhani kesho Jumapili, tunaweza kuwakalisha chini Man United pale kwao Old Trafford katika Ligi Kuu England!
Ni shabiki wa vitu vingi sana, napenda soka, muziki, filamu na kila aina ya burudani. Ninafurahishwa na baadhi ya watu katika michezo tofauti kwa jinsi ambavyo wamekuwa wakifanya vizuri. Ninapopenda kitu cha Ulaya, ujue na hapa nyumbani kipo kama kile ninachokishabikia na kama sina, basi ni lazima niwe na sababu.
Nimesema ninapenda soka na ni shabiki wa Arsenal kule Ulaya, hapa nyumbani, kiasili ni shabiki wa Simba, lakini niliachana na ushabiki wa kupenda kupindukia baada ya kugundua mambo mengi ya ajabu yanayofanyika katika klabu zetu hizi mbili za Kariakoo wakati ule nikiwa Mwandishi wa michezo.
Nikakataa ushabiki huo, sisi tunalia kwa uchungu tunapofungwa, kumbe viongozi wanashangilia, wanajua nini walichofanya. Nina miaka mitatu sijakanyaga uwanjani na hata msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara sijui ulivyo!
Unajua kwa nini nimeanza hivi? Ni kwa sababu wanafunzi wengi wako hivi. Wanapenda sana vitu vya Ulaya, wenyewe wakisema mbele, lakini hawana wanachojua hapa nyumbani. Wanatumia muda mwingi kujifunza mambo ya Kimarekani kuliko kujiuliza kuhusu Tanzania na Afrika.
Leo hii ukifika katika shule zetu na vyuo, wanamuziki, wacheza filamu na wanamichezo wa nje wanafahamika zaidi kuliko watu kama hao wa hapa nyumbani. Watakuambia kuhusu Justin Bieber, kazaliwa wapi, kapiga nyimbo gani, anapenda nini na kila kinachomhusu, ikiwa ni pamoja na girlfriend wake, lakini hawana wanachojua kuhusu Abdalah Gama!
Sio vibaya kushabikia vitu vya nje, lakini basi kwa nini hatupendi kuhoji kuhusu vya kwetu? Shule ni sehemu ya kujifunza, hasa utamaduni, ujasiri na uzalendo wetu. Tunao watu waliofanya vizuri sana katika kuufikisha utamaduni wetu hapa ulipo, lakini hakuna mtu anayehangaika kutaka kuwajua.
Utashangaa wanafunzi wanaweza kumgundua mwanamuziki mkongwe wa Marekani, Jeniffer Lopez katika picha, lakini mtaani wakashindwa kumtambua Kida Waziri. Tunawapenda mastaa wetu kwa mfano akina Diamond, AY, Profesa Jay, H Baba, Ray C, Jay Dee, Linah, Barnaba na wengineo, lakini ni nadra sana kusikia wanafunzi wakiuliza kwa nini Sinza jijini Dar es Salaam kuna eneo linaitwa Kwa Remmy!
Nadhani tunakosea sana. Tunadharau sana vyetu na kuvisifu, hata kama havina ubora vile vya nje. Siyo kila kitu chetu kinafundishwa shule, vitu vingine vinataka udadisi tu wa sisi wenyewe. Kwa mfano ukiachana na akina Kinjekitile, Mkwawa, Munyigumba, Mirambo, Songea na wenzao walio katika historia, nani anatufundisha kuhusu akina Moris Nyunyusa, Mzee Makongoro na hata Mbaraka Mwishehe?
Tunatakiwa kuwa wadadisi wa kupenda sana kujua vya kwetu. Ni jambo la kushangaza kwamba kuna wazungu wanaijua nchi yetu kuliko baadhi yetu, maana sisi muda wote tupo Facebook, Twitter na Instagram ili kujua mambo ya kina Jay Z, badala ya kujiuliza kwa nini Nyerere anaonekana katika televisheni leo, miaka zaidi ya 25 baada ya kufariki kwake?

Makosa 10 wanawake huyafanya wakiwa faragha-9

Makosa 10 wanawake huyafanya wakiwa faragha-9

Tunaendelea na mada yetu ya Makosa 10 wanawake huyafanya wakiwa faragha kutoka pale tulipoiishia wiki iliyopita.
Endelea...
Nilishaeleza huko nyuma kwamba ni vizuri kuzungumza wakati wa tendo. Hata kama wewe ni mvivu, jibidishe katika kuulainisha ulimi wako ili uwe unatamka maneno matamu, yanayoongeza hamu na mzuka wa kuendelea kuwajibika shughulini.
Unaweza kudhani ni kitu kidogo lakini ukweli ni kwamba wengi wamepata alama nyingi na kuonekana bora zaidi kwa sababu ya maneno yao faragha, matamshi na ubunifu wa kusifia. Kitaalamu, maneno matamu hunogesha tendo kwa kuongeza mshawasha.
Dunia imechafuka, usaliti umekuwa mkubwa na watu hawaogopi. Tafakari; unasalitiwa na mwenzi wako ambaye anatenda dhambi kwa kutoka na mkali wa maneno yenye kutia ‘wazimu’ kunako eneo mahsusi. Akirudi kwako, anabaini wewe upoupo tu, kazi yako kuhema kwa nguvu na kufumba macho.
Anakosa msisimko, zaidi unamkata stimu kwa sababu kwa yule anayekusaliti hukutana na manjonjo mengi. Mwisho unajikuta unapigwa kibuti bila kupenda. Tafadhali sana, yapo mambo ambayo unaweza kusema huwezi na ukavumiliwa lakini siyo hili la kumfikisha mwenzi wako kwenye kilele cha ‘maraha’.
Narudia tena, usiseme mwenzi wako anatosheka kwa sababu anakwambia amefika kileleni, la hasha! Kitu ambacho unatakiwa kuzingatia kila siku ni kama raha unazompa zina kiwango stahiki. Hakikisha huoneshi udhaifu kwenye kipengele chochote.
Mpaka hapo, bila shaka tumekubaliana kuzungumza ni muhimu, jukumu ulilonalo ni kuangalia aina ya mazungumzo. Yale ambayo hayachombezi, hayana mshawasha, hayahusu tendo, maana yake hayana mashika katika kipengele ambacho wewe nay eye mpo.
Haiwezekani katikati ya tendo unaongea: “Jana ulichelewa kurudi nyumbani.” Kuzungumza hivyo ni kujikosea wewe mwenyewe, kwani utamfanya mwenzi wako akatike stimu, kwa hiyo hata kiwango chake cha uwajibikaji kitapungua, hivyo hatakuhudumia kwa kiwango bora.
Nyongeza hapa ni kujiepusha na makelele. JJifunze kunong’ona, tena unong’onaji wenyewe ufanye masikioni mwake. Pata picha umemkumbatia mwenzi wako, hisia zake zipo juu na mshawasha (orgasm), unasomeka kwa asilimia 100, halafu wewe unamnong’oneza maneno matamu.
Kufanya hivyo, utamfanya mwenzio achanganyikiwe. Kama hujui, huo ndiyo uchawi ambao unaweza kumsababishia mpenzi wako awe anakuwaza kila anapokuwa mbali na wewe. Picha yako itamjia kichwani mwake kwa utamu, kila atakapokuwa anafikiria tendo.
Sasa basi, kuhusu kuzungumza na kutozungumza, nakushauri ujibiidishe kuzungumza kwa kunong’ona. Lainisha ulimi ili sauti yako iwe inatoka ikiwa imejaa mahaba. Nong’ona sikioni kwake, hapo ndipo utapatia. Hili siyo jukumu la kihisia, mwanaume na mwanamke, wote ni wajibu wao.

DHIBITI MAYOWE
Miguno ya mahaba na zile sauti tamu za malalamiko, zinaruhusiwa. Mayowe ambayo yanaleta kelele kwa kawaida hayaruhusiwi. Unashauriwa kuyadhibiti ili usigeuke kero kwa mwenzi wako, ukamnyima uhuru wa kufurahia tendo, kadhalika naye aweze kukuhudumia inavyotakiwa.
Busara hapa ni kwamba kwa nyumba zetu za Uswahilini, huwezi kupiga mayowe halafu ukakwepa kusikika nje. Hivyo basi, mayowe yako yanaweza kumfanya mwenzi wako ashindwe kujiamini, aamue kupunguza dozi ili kukufanya usiendelee kupiga makelele.
Atakapopunguza, itakufanya ukose uhondo uliostahili kutoka kwake. Vilevile hali hiyo, itamfanya mwenzi wako kupoteza umakini wa tendo, kwani badala ya kwenda nawe sawa, mkipanda na kushuka, anaweza kukutegea na kusikilizia zaidi makelele yako.
Msimamo wako ni mmoja tu, kuacha makelele! Kama kuna kungwi alikufundisha uwe ‘unabweka’ hovyo, kwamba ndiyo utamkosha roho mwenzi wako, huyo naye hajui. Badili mtazamo, fuata mwongozo huu ili ukuweke kisasa, vilevile ukujenge kimahaba zaidi.
HITIMISHO
Pitia vipengele 10 ambavyo nimevibainisha katika makala haya, vifanyie kazi, nakuhakikishia kwamba utakuwa mpya kimahaba, mwenye mtazamo wa kisasa. Wewe ni bora sana, ni suala la kujibiidisha tu na utaona matunda yake.

AKATWA NYETI KWENYE MAPIGANO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

AKATWA NYETI KWENYE MAPIGANO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Dustan Shekidele, Morogoro
MBALI na mtu mmoja kufariki dunia na wengine 24 kujeruhiwa na kulazwa kwenye Hospitali ya Bwagala, Turiani mkoani hapa, mwanaume mmoja amekatwa nyeti zake katika mapigano ya wakulima na wafugaji Jumanne iliyopita.
Mapigano hayo yaliyoshuhudiwa na mwandishi wetu yalipoteza amani iliyokuwa  kwenye Kijiji cha Dihombo Kata ya Hembeti Wilaya ya Mvomero.
Mashuhuda kadhaa walimwambia mwandishi wetu kwamba, mtu aliyekatwa  nyeti alikutana na wakulima hao wenye hasira waliokuwa wakimvamia mgeni yeyote waliyemuona  mbele yao.
“Wakulima walikuwa na silaha za jadi kama vile mapanga, mishale ya sumu na marungu, walimkuta mtu huyo aliyekuwa akipita na kumvamia kisha kumpiga na alipoanguka chini mkulima mmoja alimkata nyeti zake,” alisema shuhuda aliyejitambilisha kwa jina la Kibwana.
Mtu aliyekatwa nyeti (angalia picha ukurasa wa mbele) hakufahamika jina lake mara moja, lakini baadhi ya watu walioshuhudia tukio hilo walisema kwamba alikimbizwa hospitali ili kunusuru maisha yake.
Hata hivyo, baadhi ya wakulima nao waliumizwa vibaya katika tukio hilo lililosababisha kifo cha mfugaji Yusuf Mdutu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile amethibitisha kutokea kwa mapigano hayo huku akisema kuwa msako mkali unaendelea kuwakamata wahusika.

ALLY CHOKI AVUTA MKOKO KULINDA HESHIMA

ALLY CHOKI AVUTA MKOKO KULINDA HESHIMA

Stori: Shakoor Jongo
ILI kulinda heshima ya ukurugenzi, Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo, Ally Choki amevuta mkoko Toyota Prado yenye thamani ya shilingi milioni 52.
Mkoko mpya wa Ally Choki aina ya Toyota Prado ofisi za GPL.
Choki amenaswa na ndinga hiyo juzikati jijini Dar ambapo paparazi wetu alipomuuliza sababu za kuongeza ndinga hiyo ilihali ana magari mengine likiwemo Toyota Noah, Choki alitaja kigezo cha heshima kuwa sababu iliyomfanya anunune ndinga hiyo.
Muonekano wa mbele wa Toyota Prado.
“Unajua kila kitu kinakwenda na mipango lakini wakati mwingine heshima ya mtu inajengwa na vitu vidogovidogo hivyo niliona angalau ndinga kama hii inaendana na mimi, siyo kwamba nimenunua kuonesha jeuri, hapana lakini heshima nayo inahusika barabarani,” alisema Choki.
Kuhusu suala la kujipendelea kununua magari yeye kama mkurugenzi, Choki alisema yeye na bendi yake huwa hawana matatizo ya magari ya kusafiria ndiyo maana wana magari zaidi ya saba yanayotumika kwa shughuli za bendi.
Choki kama mkurugenzi na muimbaji, anakuwa mwanamuziki wa kwanza kumiliki gari la thamani katika wanamuziki wa dansi Bongo.

MTOTO ANYOFOLEWA JICHO

MTOTO ANYOFOLEWA JICHO

HAKIKA ni mateso na inauma kusikiliza maelezo yake.
MTOTO Khalidi Juma mwenye umri wa miaka minne, mkazi wa Vingunguti jijini Dar es Salaam, yuko katika mateso makali baada ya jicho lake moja kutolewa katika harakati za kumnusuru na ugonjwa wa Kansa, huku lingine nalo likilegea.
Mama wa mtoto huyo Hadija Kilindo.
Akizungumza na gazeti hili, mama wa mtoto huyo Hadija Kilindo, alisema alimzaa mtoto huyo akiwa na afya njema, lakini alipofikisha umri wa miezi tisa ndipo alipogundua kitu cheupe kwenye mboni ya jicho lake.
Baada ya hali hiyo, alisema alimpeleka katika hospitali inayotibu watu wenye ulemavu mbalimbali ya CCBRT iliyopo Msasani jijini Dar, ambako baada ya kupimwa, aliambiwa mwanaye alikuwa na kansa.
Mtoto Khalidi Juma  jicho lake moja limetolewa katika harakati za kumnusuru na ugonjwa wa Kansa.
“Baada ya kuambiwa mtoto wangu ana ugonjwa wa kansa sikuwa na jinsi, nilikubali afanyiwe upasuaji kwa ajili ya kuliondoa jicho hilo ili kuokoa maisha yake,” alisema.
Mama huyo alisema ilipofika mwaka 2012, jicho lingine lilianza kumuuma huku likiwa linavimba, lakini alipompeleka katika Hospitali ya Muhimbili, aliambiwa kansa imeshaenea mpaka kwenye ubungo, hivyo arudi naye nyumbani kwani hawezi kuishi kwa muda mrefu.
“Kwa kweli nilivyoambiwa hivyo nilinyong’onyea mwili mzima nikawa sina jinsi kabisa na nikapoteza matumaini kabisa ya mwanangu kuendelea kuishi tena,”alisema.
Alisema alirudi nyumbani huku maumivu ya kijana wake yakiendelea na mwishoni, jicho lake likawa halioni tena. Kuhusu jicho lililotolewa, mama huyo alisema alikuwa akilitoa na kulirudisha kwa ajili ya kulisafisha, lakini hivi sasa hawezi kulitoa tena kwa vile kuna nyama zilizolishika na hivyo kumsababishia maumivu makali mno mwanaye hasa kichwani.
“Unavyotuona hapa usiku hatulali kabisa, mtoto ni kulia kwa maumivu, amefikia wakati hawezi kula vizuri na anatumia muda mwingi kulia,” alisema.
Mama huyo aliongeza kueleza kuwa kutokana na hali ya mwanaye, anakosa muda wa kufanya chochote cha kujiingizi kipato, hivyo kuwa katika wakati mgumu mno kimaisha, hasa kwa vile baba mzazi wa mtoto huyo alimkimbia tokea alivyoanza kuumwa.
“Mimi naamini kabisa labda nikipata msaada nikienda hata kwa wachina nitapata hata dawa ya kumpunguzia mtoto wangu maumivu anayoyapata kwa hivi sasa,” alisema.
Kwa ye yote ambaye ataguswa na habari hii na angepeta kutoa msaada wa aina yo yote, anaweza kuwasiliana na mama mzazi anayetumia simu nambari 0656 042017.

MZEE WA UPAKO:NILIKAMATWA KWA MADAWA YA KULEVYA

MZEE WA UPAKO:NILIKAMATWA KWA MADAWA YA KULEVYA

LITOKEA lakini haikuandikwa kwa sababu haikudakwa! Mchungaji wa Kanisa la Maombezi jijini Dar es Salaam (GRC), Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako’ amekiri kuwa aliwahi kukamatwa na kuwekwa lupango katika Gereza la Keko, Dar kwa siku 14 akituhumiwa kujihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya ‘unga’, Risasi Jumamosi lina sauti yake.

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi, Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako’.
Akizungumza kwa uso wenye majonzi na siha ya huzuni mwishoni mwa wiki iliyopita kanisani kwake Ubungo- Kibangu, Dar, Mzee wa Upako alisema hawezi kuisahau siku hiyo ambayo shetani aliamua kukunjua kucha zake kumwelekea yeye.
Alisema ishu hiyo ilimkuta mwaka 2005 akiwa tayari mtumishi wa Mungu aliye hai, lakini anachomshukuru Mungu ni kwamba alimsimamia kwa nguvu zote.

MCHEZO MZIMA ULIVYOKUWA
Akizungumzia mchezo mzima ulivyokuwa, Mzee wa Upako alisema siku ya tukio (hakuitaja) akiwa kanisani hapo na waumini wake ghafla walitokea askari polisi ambao idadi yao haikumbuki.
Alipotaka kujua shida yao, walisema wao wanatokea Polisi Central, Dar na walikwenda pale kufanya naye mahojiano na kumpekua kwani alikuwa akihisiwa anajishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya.“Polisi walikuja kanisani wakafanya upekuzi, wakaenda nyumbani  nako wakafanya hivyohivyo kisha wakaondoka zao baada ya kutokuona chochote,” alisema Mzee wa Upako.
                                                                               Kamanda Nzowa.

POLISI WA INTERPOL WATUMIKA
Mzee wa Upako anaendelea kufunguka: Siku mbili mbele  wakaja wengine, wakasema wao ni Polisi wa Kimataifa (Interpol). Nao wakasema wamekuja kunipekua, lakini wao licha ya kutokukuta chochote walinikamata na kunipeleka Mahabusu ya Gereza la Keko, Dar ambapo nilikaa kwa muda wa kama wiki mbili.

AZITAJA SIKU ZA MAJARIBU
Mzee wa Upako: Hakika zilikuwa ni siku za majaribu kwangu kukamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, lilikuwa ni jambo ambalo sijawahi kulifanya achilia mbali kuliwaza.
Licha ya kukaa kwa wiki mbili kule mahabusu, Polisi wa Interpol nao walijiridhisha kwamba mimi sifanyi biashara hiyo, wakaniachia huru niendelee kumtumikia Mungu wangu.
                                                                 Madawa ya kulevya.

AWAGUNDUA WABAYA WAKE
Mchungaji huyo maarufu kwa msemo wake WATASHINDANA, LAKINI HAWATASHINDA aliendelea kusema kuwa aligundua kukamatwa kwake kulitokana na mpango wa siri uliofanywa na baadhi ya wachungaji wenzake (hakuwataja majina) kwa ajili ya kumdhoofisha kiimani.
“Zilikuwa ni mbinu chafu za kunidhoofisha kiimani kutoka kwa baadhi ya wachungaji wenzangu wenye wivu na huduma yangu. Lakini kwa jina la Yesu aliye hai walishindwa, watashindana lakini hawatashinda,” alisema Mzee wa Upako.

AHISI KUONDOLEWA HADHI
Mzee wa Upako alisema tukio hilo aliliona kama la kumwondelea hadhi katika jamii, hususan kwa waumini wake lakini kwa kuwa yeye ni ‘super charge’ kamwe hawezi kuruhusu imani yake iyumbishwe na hila za muovu shetani.

ANACHOMSHUKURIA MUNGU
Mchungaji huyo alisema baada ya kutoka Keko alimshukuru Mungu kwa vile hakuna chombo chochote cha habari kilichofuatilia juu ya sakata hilo na kwamba gazeti hili (Risasi Jumamosi) linakuwa la kwanza kuandika.
“Nashukuru hakuna chombo chochote cha habari kilichogundua juu ya habari hiyo, ninyi mnakuwa wa kwanza kuijua na hata kuiandika kama mtapenda,” alisema Mzee wa Upako.

APINGA DHANA YA WATUMISHI WA MUNGU KUUZA UNGA
Akizungumzia kwa undani sakata la watumishi wa Mungu kujihusisha na biashara ya unga, Mzee wa Upako alisema:
“Siamini kama kweli kuna watumishi wa Mungu wa hapa Tanzania wanafanya biashara hiyo. Kinachotokea ni kwamba, watu wamekuwa wakiwasingizia watumishi kwa sababu zao.”

WAUMINI WAKE SASA
Juzi Alhamisi, Risasi Jumamosi liliwasiliana na baadhi ya waumini wa kanisa hilo ambapo walisema mtumishi wao huyo amekuwa akionewa kijicho kutokana na mafanikio yake ya kiroho na kimwili.
“Sisi waumini wa GRC tukisikia lolote baya kuhusu Mzee wa Upako huwa hatushtuki kwa sababu wapo baadhi ya watumishi wa Mungu wanamuonea kijicho kwa sababu ana mafaniko ya kiroho na kiimani,” alisema muumini mmoja bila kutaja jina.
Mwingine alisema nguvu kubwa ya kiroho aliyonayo mtumishi huyo imemfanya aibue maadui wasio na hofu ya Mungu kwa kumpakazia skendo mbalimbali wakiamini akichafuka waumini watamkimbia.
Jumatano iliyopita, paparazi wetu alifika Kituo Kikuu cha Polisi (Police Central), Dar na kuulizia ishu hiyo ambapo afande mmoja alisema anayeweza kujua ni IGP Mstaafu, Omary Mahita ambaye wakati huo alikuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania.
Hata hivyo, juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa ziligonga mwamba kufuatia simu yake ya kiganjani kutokupatikana hewani.

VICTORIA HAMMAH: SIACHI SIASA HADI NIPATE DOLA MILIONI 1

VICTORIA HAMMAH: SIACHI SIASA HADI NIPATE DOLA MILIONI 1

Victoria Hammah amekuwa akisema amekuwa na shinikizo la kuiba pesa za umma.
Naibu waziri wa mawasiliano nchini Ghana Victoria Hammah ameachishwa kazi baada ya kunukuliwa akisema kuwa atasalia katika siasa hadi atakapo pata fedha kiasi cha dola milioni moja.

Anaonekana katika kanda ya video akisema kuwa ukiwa na pesa unaweza kuwashawishi watu. Bi Hammah bado hajatoa tamko lolote kuhusiana na mkanda huo wa video au hatua ya kufutwa kazi. Mwandishi wa BBC mjini Accra anasema Bi Hammah alikuwa na ushawishi mkubwa katika uchaguzi wa rais John Mahama mwaka jana.

Baada ya uteuzi wake baadhi ya wadadisi walionya kuwa ana umri mdogo sana kuweza kuhudumu katika serikali.Mwezi Agosti alinukuliwa akisema kuwa kuna shinikizo za kumtaka aibe fedha za umma kwa kuwa watu hudhani kwamba yeye ni tajiri kwa sababu ya wadhifa wake wa uwaziri.Katika kanda hiyo alisikika akisema kuwa hatatoka katika siasa hadi atakapopata dola milioni moja.Pia alisikika akimkosoa waziri mwenzake akisema hana akili,ana sura mbaya na anapenda sana kujigamba na kuwafokea watu. Chanzo ni BBC Swahili.