Friday, March 29, 2013

DIVA: AJUTA TENA KUMPA PENZI MO RACKA

Mtangazaji wa Kipindi cha Ala za Roho cha Clouds Radio, Loveness Malinzi ‘ Diva’ juzikati amefunguka kuwa, kosa kubwa alilowahi kulifanya kwenye maisha yake ni kummegea penzi mwanamuziki anayefahamika kwa jina la Mo Racka.

Diva alifunguka hayo ikiwa ni mara ya pili baada ya kufanya hivyo mwaka jana kupitia mtandao wa Twitter ambapo aliandika : “Kutoka kimapenzi na Mo Racka ni kosa kubwa ambalo nimelifanya, nilikuwa mdogo na nilitokea kumpenda mvulana mtanashati Dar, na kila msichana aliyekuwa akituona aliishia kusema ‘Mungu wangu’, ilikuwa balaa. Hata hivyo, sasa hivi tuko poa na ni marafiki sana.”

Diva aliwahi kuwa kwenye uhusiano na kijana huyo na inasemekena kila mmoja alikuwa kamzimia mwenzake ndiyo maana haupiti muda mrefu mmoja kati yao lazima atakumbushia enzi zao.


HIVI NDIVYO GHOROFA LILIVYOANGUKA POSTA JIJINI DAR

Hiki ndicho kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15.

  Winchi likiokoa mabaki ya moja ya gari lililoangukiwa na kifusi.


  Rais Jakaya Kikwete (katikati) akiangalia hali ya uokoaji inavyoendelea.

Mkuu wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, akitoa maelekezo ya jinsi ya kuondoa kifusi eneo la tukio.

  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki (katikati) akifuatilia shughuli ya uokoaji.

 Watu mbalimbali wakiondoa kifusi.

  Askari aliyejuu ya farasi akihakikisha usalama eneo hilo.

 Baadhi ya watu wakilisukuma gari ambalo pia lilikuwa kwenye ajali hiyo.

 Mama Salma Kikwete (kulia) na Rais Kikwete wakiangalia kifusi.

Kijana aliyenusurika katika ajali hiyo akinywa kahawa.

LEO majira ya saa mbili na nusu asubuhi Watanzania wameingia kwenye vilio baada ya jengo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es Salaam, kuanguka na kuwafunika watu waliokuwa eneo hilo na kusababisha wengine kupoteza maisha. Mpaka sasa haijajulikana idadi kamili ya watu waliokuwemo ndani yake, ila watu wawili wamethibitishwa kuwa wamekufa na wengine 19 kujeruhiwa.


siku ya Pasaka Dar Live inakuletea mpambano wa mwaka kati ya TMK wanaume HALISI na TMK wanaume FAMILY


Kajala afanya toba nzito





Friday, March 22, 2013

MASOGANGE AKIMBIA BONGO KISA MAKALIO YAKE!

‘VIDEO Queen’ maarufu Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ ambaye muda mwingi amekuwa akiishi Afrika Kusini ameelezea jinsi maisha ya Bongo yalivyomchosha huku usumbufu anaopata kutokana na makalio yake makubwa ikiwa moja ya sababu.

Akipiga stori na Ijumaa juzikati, Masogange alisema umbile lake hilo limekuwa likimfanya akose amani anapokatiza mitaani, tofauti na Sauzi ambako wanawake wengi wamefungashia huku yeye akionekana ‘cha mtoto’.
“Muda mwingi niko Sauzi, Bongo miyeyusho na hili umbo langu nimekuwa nikisumbuliwa sana na wanaume lakini Sauzi hili langu la kawaida, wengi wamefungashia ile mbaya, kwa hiyo muda mwingi nitakuwa huko, huku nitakuwa nakuja na kuondoka,” alisema Masogange.

Ney ft Diamond --- Mziki gani

Ney ft Diamond --- Mziki gani

Thursday, March 14, 2013

DIAMOND: PENNY SASA SIO TU MPENZI WANGU, ANAELEKEA KUWA MAMA WATOTO WANGU


AMNUNULIA GARI LENYE THAMANI YA SHILINGI MILLIONI 15.
NI KWAAJILI YA MIZUNGUKO YA KLINIK, OFFISIN, NA KWINGINEKO.
ASEMA SI VIZURI KUGOMBANIA PRADO AU GARI LA MAMA NASEE.

Baada ya kukana kutokuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtangazaji wa Tv Penny katika moja ya interview aliyoifanya na kipindi xha xxl, leo hii kupitia kwa Gossip Cop wa u heard ya xxl Diamond amekubali kuwa ni kweli Penny ndio mpenzi wake na anatarajia mtoto nae (Penny ni mja mzito), na ameamua kumnunulia gari kwa ajili ya kumsaidia kwenye mizunguko ya kliniki ofisini na shughuli zingine

" yaaa thatsssssss, unajuaaaaaa, mmmmhhhhh, yah thats true thats true unajua sa sio tu ni mpenzi wangu, anaelekea kuwa mama watoto wangu, kwasababu ya mizunguko ya kwenda clinik na nini ikawa sio vizuri kujitia kwenye madaladala au kuanza kugombania prado  hiyo hiyo au achukue gari ya mama Naseeb au nini unajua, kwahiyo nikaona nivizuri nikimnunulia gari yake yeye ambayo atakua anaendea clinik na sehem zingine"

kama unakumbuka 23 Feb 2013, tukupa story kuhusiana na kile alichokisema Diamond kuhusu uhusiano wake wa sasa na mtangazaji wa DTV Penny, ambapo alisema si kweli hawana uhusiano wowote na picha zilizokuwa zikionekana ni picha kutoka kwenye movie ambayo wanaifanya...

DIAMOND ATANGAZA KUJENGA MSIKITI


SIKU chache baada ya kuwachefua Waislamu wenzake kwa kutimba kwenye Maulid na kuomba dua akiwa amevaa hereni na mkufu, msanii wa Bongo Fleva mpenda totoz, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametangaza kujenga msikiti jijini Dar es Salaam, kwani ni jambo alilolipanga kwa muda mrefu.



Kwa mujibu wa staa huyo ambaye kwa sasa anaminya kimapenzi na mtangazaji wa DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’, msikiti huo utakuwa kumbukumbu yake kwa watakaoutumia kama sehemu ya kurudisha kwa jamii inayompa sapoti kubwa.
Diamond ambaye amemjengea mama yake, Sanura Kassim ‘Sandra’ nyumba ambayo hadi sasa imegharimu Sh. milioni 260 alifunguka: “Ninajitahidi sana kununua viwanja au vinyumba vidogovidogo maeneo tofauti. Nipo kwenye plan (mpango) ya kujenga msikiti japo sijapanga sehemu hasa hadi nipate eneo la kutosha.
“Nataka iwe kumbukumbu ili hata kesho na keshokutwa nikifa, vizazi vijavyo wawe wanaswali kwenye msikiti uliojengwa na Diamond.
“Kwa kufanya hivyo itanipa baraka kubwa sana na soon tu nina imani mwenyezi Mungu atanisaidia nijenge huo msikiti.”

Sunday, March 10, 2013

ACHARANGWA MAPANGA KISA MKE WA MTU


CPWAA TO BE ONE OF THE SPEAKERS FOR THE IMPACT OF ICT IN TANZANIA ENTERTAINMENT INDUSTRY AT MOMODAR‏

A Tanzanian Music Artist Ilunga Khalifa a.k.a CPwaa who has 3 Tanzanian Kilimanjaro Music Awards and multiple International Music Awards nominations including "The Channel O Africa Music Video Awards" will be one of the key speakers at MobileMonday (MoMo) in Dar es salaam this Monday of 11th March 2013. CPwaa who is one of Tanzanian International Bongoflava Artists is also an  ICT specialist with over 7 years of work in Tanzania Telecommunication Industry. Started working in 2006 immediately after graduating from college CPwaa is a professional IT Engineer and Technical Project Manager. Currently working as IT consultant for different companies and a Music stakeholder.





At this Mobile Monday CPwaa will share his experience, success and challenges in the entertainment industry and how technology has impact on it.The event will take place at KINU Innovation offices  and other speakers include: 1. Rashid Shamte - Head of Group Strategy, 6Telecoms.
2. Luca Neghesti - Enterpreneur and founder of Bongo5.
3. Charles Motadane - Head of value Added Services and Internet, Vodacom Tanzania.
4. Hussein Mkwazi - Final year student at IFM, Part-time programmer.

Saturday, March 2, 2013

FAMILIA SASA YA CHARUKA PATI YA LULU






Kulipuka kwa habari kuwa staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefanyiwa sherehe na kigogo baada ya kutoka Segerea, Dar kwa dhamana, familia yake imecharuka na kudai kuwa hakukuwa na jambo kama hilo wala haifikirii kufanya hivyo, Risasi Jumamosi lina kila kitu.

Habari za uhakika zilidai kuwa Lulu ambaye anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba, mara baada ya kuachiwa kwa dhamana Januari 26, mwaka huu, kuliibuka minong’ono kutoka kwa marafiki zake mbalimbali walioelezwa kuwa walitaka kumfanyia pati lakini ndugu walikataa.



SHEREHE FEKI ZATAJWA
Ilielezwa kuwa licha ya ndugu hao kukataa kumfanyia sherehe ndugu yao (Lulu), bado kuna kikundi cha watu kiliendelea kueneza taarifa za kizushi kwamba lazima kuwe na sherehe ya kumpongeza baada ya kutoka gerezani.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana ndani ya familia ya Lulu zilieleza kuwa taarifa zilizosambaa mwishoni mwa wiki iliyopita kwamba alifanyiwa bonge la pati na kikundi hicho kama madai ya awali yalivyokuwa, hazikuwa na ukweli wowote na mbaya zaidi zililenga kumjengea Lulu mazingira magumu ya kisheria.
 
 DADA WA LULU ANENA
Akizungumza na paparazi wetu kwa sharti la kutochorwa jina gazetini, dada wa Lulu alisema kuwa familia ilikerwa kupita maelezo na kuwepo kwa taarifa hizo huku akisisitiza kwamba hazina ukweli wowote.
“Sisi kama familia hatujamfanyia wala hatufikirii kumfanyia sherehe ya aina yoyote kwa ajili ya kumpongeza. Tunaomba ieleweke hivyo na hao wanaoeneza habari za uongo waache haraka, hatuzipendi,” alisema dada huyo.

LULU ANASEMAJE?
Zoezi la paparazi wetu kutaka kumsikia Lulu anazungumziaje juu ya ishu hiyo liligonga mwamba baada ya kuelezwa kuwa kwa sasa amezuiwa kuzungumzia ishu yoyote hasa inayohusu maisha yake katika kipindi hiki anachosubiri kesi yake kuendelea kuunguruma.

CHEKA NA KATUNI ZA GPL LEO












MAKUNDI YA WANAWAKE NA MITAZAMO YAO KWA WANAIME- 5

 Tunaendelea na mada ya kuyachambua makundi ya wanawake na mitazamo yao kwa wanaume.
Tunaendelea kuanzia pale tulipoishia, sasa endelea...




Wale wenye vipato vidogo au wanaume wachumi, hawakubaliki kwa wanawake wanaounda kundi hili. Mara nyingi wanawake wa kundi hili huwa hawaivi na wanaume werevu, wenye kupenda kujiuliza mara mbilimbili kwa kila jambo.
Kwa kawaida, wanaume werevu hutaka zaidi kuwekeza mapenzi yao kwa wanawake wasiosukumwa na kitu ndiyo wapende. Kwa maana hiyo, mabadiliko ya mwanamke kipindi cha fedha na pale zinapokata, huwashtua, hivyo kuwatia kasoro.
Mara nyingi huachana, zaidi wanaume ndiyo huacha, mara chache wanawake hukimbia. Kama wewe unadhani chako ni chenu na chake ni chenu, utakuwa umeambulia sifuri.
Tambua kuwa chako ni chenu na chake ni chake, kama unabisha hebu mjaribu kumuomba fedha uone kama atakupa. Akikupa lazima ataandika deni.
Na atakuwa anakudai mpaka umlipe hata kama fedha zenyewe alizitoa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Hata kama yeye ndiye atakuwa na
kipato kikubwa zaidi, bado hawezi kukubali kuhudumia familia wakati wewe upo.
Bora fedha zake ziende kununua nguo na kufanya mambo
mengine binafsi lakini familia lazima ihudumiwe na wewe.

TATHMINI YAO KIMAPENZI
Kuwa na mwanamke wa kundi hili ni kujitafutia maradhi ya moyo. Kwa maana tafsiri ya mapenzi ya dhati wao huichakachua kutoka kwenye uhalisia mpaka kusomeka “fedha ndiyo mapenzi.” Hata ukiwa nazo na ukajitwisha mzigo kumuoa na kumweka ndani, kuna siku utajuta, utalia machozi. Vilevile yanaweza yasikutokee lakini moyoni ikawa mateso.
Umeshawahi kuona mateso ya mtu anayeumia kwa ajili ya mapenzi? Hebu omba uendelee kusimuliwa yasikukute.
Ila ukitaka nawe uwe mfano wa wanaume wanaolia mchana kweupe, jiweke kwa mwanamke
wa kundi hili halafu thubutu kuwekeza moyo wako wote. Utakonda bila kuumwa, utapoteza hamu ya kula ilhali tumboni hakuna kitu.
Leo utakuwa na fedha na unampa, atakupenda sana.
Kesho ukiishiwa utapata matokeo matatu ambayo yote ni mabaya mno kufanyiwa na umpendaye.
Mosi; anaweza kukukimbia na kutua kwa mwanaume mwingine anayeonekana ana fedha zaidi.
Hawezi kuendelea na wewe, atakwenda kuchuma kule zinapopatikana kwa urahisi. Pili; kama mmeshaoana, atakunyanyasa ndani ya nyumba.
Anaweza kutoka nyumbani bila kukutaarifu ratiba zake, vilevile atarudi muda autakao.
Akifanya hivyo ni bora ukae kimya, kwa maana ukimuuliza au kumkosoa unaweza kukumbana na majibu ya kuumiza sana. Usishangae akakuuliza: “Katika wanaume na wewe umo?” Kabisa, tena atakapokuuliza hivyo atakuwa anajiona yupo sahihi kwa asilimia 100.
Hawezi kujiona anakosea kwa sababu tafsiri yake ndiyo inamuongoza hivyo. Anaamini ili uwe mwanaume timilifu, sharti uwe na fedha, tena zisiishie mfukoni kwako, badala yake muwe ‘mnashea’. Zako ni zenu, zake ni zake, tena usithubutu kufikiri zake ni zenu.
Tatu; atakuingiza kwenye madeni. Atakufanya ukope ili kumtimizia mahitaji yake. Naye atakopa halafu atakuhimiza ulipe. Maisha yako hayatakuwa na amani. Kwa vile muda wote anawaza fedha, atatoka nje ya ndoa wakati wowote.
 Yeyote atakayejitokeza mbele yake ambaye atamfanya awe na fedha, hatasita kumpa kilichopo ndani ya mwili wake.
Anaweza kuutoa mwili wake kwa muuza duka au genge kwa sababu hupata mahitaji bure, hivyo kuweka kibindoni fedha ambazo humwachia za matumizi nyumbani.
Wanawake wa kundi hili ni hatari mno, kwani unawezakupona maradhi ya moyo kutokana na usugu wako kihisia lakini ukapata maambukizi ya magonjwa zinaa, kwa maana hawachagui pa kujiweka.
Itaendelea wiki ijayo.